Isaya 4:1-6
4 Siku hiyo, wanawake saba watamkamata mwanamume mmoja,+ wakisema:
“Tutakula mkate wetu wenyeweNa kuvaa nguo zetu wenyewe;Lakini turuhusu tu tuitwe kwa jina lakoIli kuondoa aibu yetu.”*+
2 Siku hiyo kile ambacho Yehova atachipusha kitakuwa kizuri sana na chenye utukufu, na mazao ya nchi yatakuwa kitu cha kujivunia na urembo kwa ajili ya waokokaji wa Israeli.+
3 Yeyote atakayebaki Sayuni na kuachwa Yerusalemu ataitwa mtakatifu, wale wote walio Yerusalemu walioandikwa kwa ajili ya uzima.+
4 Yehova atakapoosha uchafu wa* mabinti wa Sayuni+ na kusafisha umwagaji wa damu wa Yerusalemu kutoka ndani yake kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza,*+
5 Yehova pia ataumba juu ya eneo lote la Mlima Sayuni na juu ya mahali pa makusanyiko yake wingu na moshi wakati wa mchana na moto mwangavu unaowaka wakati wa usiku;+ kwa maana juu ya utukufu wote kutakuwa na mahali pa kujificha.
6 Na kutakuwa na kibanda chenye kivuli cha kujikinga na joto wakati wa mchana,+ nacho kitakuwa kimbilio na ulinzi wakati wa dhoruba na mvua.+
Maelezo ya Chini
^ Yaani, aibu ya kutoolewa na kutokuwa na watoto.
^ Tnn., “kinyesi cha.”
^ Au “kuondoa.”