Isaya 29:1-24
29 “Ole kwa Arieli,* Arieli, jiji ambalo Daudi alipiga kambi ndani yake!+
Endelea mwaka baada ya mwaka;Mzunguko wa sherehe+ na uendelee.
2 Lakini nitaliletea taabu Arieli,+Na kutakuwa na kilio na maombolezo,+Nalo litakuwa kwangu kama jiko la madhabahu ya Mungu.+
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako,Nami nitakuzingira kwa ngomeNa kujenga maboma dhidi yako.+
4 Utashushwa chini;Utazungumza kutoka ardhini,Na mambo utakayosema yatakuwa mnong’ono kwa sababu ya mavumbi.
Sauti yako itatoka ardhini+Kama sauti ya mtu anayewasiliana na roho,Na maneno yako yatatoka mavumbini kama sauti ya ndege.
5 Umati wa maadui wako* utakuwa kama ungaunga laini,+Umati wa waonevu kama tu makapi yanayopeperuka.+
Na jambo hilo litatokea haraka, ghafla.+
6 Yehova wa majeshi atawakazia fikiraKwa mngurumo na tetemeko la ardhi na kelele kubwa,Kwa upepo wa dhoruba na tufani na miali ya moto unaoteketeza.”+
7 Kisha umati wa mataifa yote yanayopigana vita na Arieli+—Wale wote wanaopigana vita naye,Minara inayomzingira,Na wale wanaomsababishia taabu—Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.
8 Naam, itakuwa kama mtu aliye na njaa anayeota kwamba anakula,Lakini anaamka akiwa na njaa,*Na kama mtu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa,Lakini anaamka akiwa amechoka na akiwa na kiu.*
Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa umati wa mataifa yoteYanayopigana vita dhidi ya Mlima Sayuni.+
9 Pigweni na butwaa na mshangae;+Jipofusheni na mpofushwe.+
Wamelewa, lakini si kwa divai;Wanapepesuka, lakini si kwa sababu ya kileo.
10 Kwa maana Yehova amewamwagia roho ya usingizi mzito;+Ameyafunga macho yenu, enyi manabii,+Naye amefunika vichwa vyenu, enyi waonaji.+
11 Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu ambacho kimefungwa kwa muhuri.+ Wakimpa mtu anayejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.”
12 Na wakimpa kitabu hicho mtu asiyejua kusoma na kumwambia: “Tafadhali, kisome kitabu hiki,” atasema: “Sijui kusoma hata kidogo.”
13 Yehova anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyaoNao huniheshimu kwa midomo yao,+Lakini mioyo yao iko mbali sana nami;Na hofu yao kunielekea inategemea amri za wanadamu ambazo wamefundishwa.+
14 Kwa hiyo, mimi Ndiye nitakayewatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+Maajabu juu ya maajabu;Na hekima ya watu wao wenye hekima itatoweka,Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+
15 Ole wao wanaojitahidi sana kumficha Yehova mipango yao.*+
Wanatenda matendo yao mahali penye giza,Huku wakisema: “Ni nani anayetuona?
Ni nani anayejua kutuhusu?”+
16 Jinsi mnavyopotosha mambo!*
Je, mfinyanzi anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+
Je, kitu kilichotengenezwa kinapaswa kusema kuhusu yule aliyekitengeneza:
“Hakunitengeneza?”+
Na je, kitu kilichotengenezwa kinasema kuhusu yule aliyekitengeneza:
“Hana uelewaji”?+
17 Katika muda mfupi, Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa msitu.+
18 Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kile kitabu,Na kutoka katika utusitusi na giza macho ya vipofu yataona.+
19 Wapole watashangilia sana katika Yehova,Na maskini miongoni mwa watu watashangilia katika Mtakatifu wa Israeli.+
20 Kwa maana mwonevu hatakuwapo tena,Anayejigamba ataangamia,Na wote wanaokaa macho ili kusababisha madhara wataangamizwa,+
21 Wale ambao kwa neno la udanganyifu wanawafanya wengine wawe na hatia,Wanaotega mitego ili kumnasa mtetezi* katika lango la jiji,+Na wale ambao kwa mashtaka yasiyo na msingi humnyima haki mwadilifu.+
22 Basi Yehova, aliyemkomboa Abrahamu,+ anaiambia hivi nyumba ya Yakobo:
“Yakobo hataona aibu tena,Na uso wake hautabadilika rangi tena.*+
23 Kwa maana anapowaona watoto wake,Ambao ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+Watalitakasa jina langu;Naam, watamtakasa Mtakatifu wa Yakobo,Nao watamwogopa Mungu wa Israeli.+
24 Wale waliopotoka rohoni watapata uelewaji,Na wale wanaolalamika watakubali mafundisho.”
Maelezo ya Chini
^ Huenda jina hili linamaanisha “Jiko la Madhabahu ya Mungu,” inaelekea ni Yerusalemu.
^ Tnn., “wageni wako.”
^ Au “nafsi yake ikiwa tupu.”
^ Au “nafsi yake ikiwa imekauka.”
^ Au “shauri lao.”
^ Au “Jinsi mlivyopotoka!”
^ Tnn., “anayekaripia.”
^ Yaani, kwa sababu ya aibu na kukata tamaa.