Mwanzo 1:1-31

  • Uumbaji wa mbingu na dunia (1, 2)

  • Siku sita za kuitayarisha dunia (3-31)

    • Siku ya 1: nuru; mchana na usiku (3-5)

    • Siku ya 2: anga (6-8)

    • Siku ya 3: nchi kavu na mimea (9-13)

    • Siku ya 4: mianga ya mbinguni (14-19)

    • Siku ya 5: samaki na ndege (20-23)

    • Siku ya 6: wanyama wa nchi kavu na wanadamu (24-31)

1  Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.+  Sasa dunia haikuwa na umbo nayo ilikuwa tupu,* na giza lilikuwa juu ya kilindi cha maji,*+ na nguvu ya utendaji ya Mungu*+ ilikuwa ikienda huku na huku juu ya maji.+  Na Mungu akasema: “Kuwe na nuru.” Basi kukawa na nuru.+  Baada ya hayo, Mungu akaona kwamba nuru ilikuwa nzuri, na Mungu akaanza kuitenganisha nuru na giza.  Mungu akaiita nuru Mchana, lakini giza akaliita Usiku.+ Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.  Kisha Mungu akasema: “Na kuwe na anga+ katikati ya maji, na anga liyatenganishe maji na maji.”+  Ndipo Mungu akatengeneza anga na kuyatenganisha maji yaliyo chini ya anga na maji yaliyo juu ya anga.+ Na ikawa hivyo.  Mungu akaiita anga Mbingu. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.  Kisha Mungu akasema: “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, na nchi kavu itokee.”+ Na ikawa hivyo. 10  Mungu akaiita nchi kavu Dunia,+ lakini mkusanyiko wa maji, akauita Bahari.+ Na Mungu akaona kuwa ni vyema.+ 11  Kisha Mungu akasema: “Dunia na ichipushe majani, mimea inayozaa mbegu na miti ya matunda inayozaa matunda kulingana na aina zake, miti inayozaa matunda yenye mbegu duniani.” Na ikawa hivyo. 12  Dunia ikaanza kuchipusha majani, mimea inayozaa mbegu+ na miti inayozaa matunda yenye mbegu, kulingana na aina zake. Kisha Mungu akaona kuwa ni vyema. 13  Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tatu. 14  Kisha Mungu akasema: “Na kuwe na mianga*+ katika anga la mbingu ili itenganishe mchana na usiku,+ nayo itakuwa ishara ya kuonyesha majira na siku na miaka.+ 15  Itakuwa mianga katika anga la mbingu ili kuangazia dunia.” Na ikawa hivyo. 16  Ndipo Mungu akatengeneza mianga miwili mikubwa, mwanga mkubwa zaidi wa kutawala mchana+ na mwanga mdogo wa kutawala usiku, na pia nyota.+ 17  Basi Mungu akaiweka katika anga la mbingu ili iangazie dunia 18  na kutawala wakati wa mchana na wakati wa usiku na kutenganisha nuru na giza.+ Mungu akaona kuwa ni vyema. 19  Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne. 20  Kisha Mungu akasema: “Maji na yajae viumbe walio* hai, na viumbe wanaoruka waruke juu ya dunia katika anga la mbingu.”*+ 21  Mungu akaumba viumbe wakubwa* wa baharini na viumbe wote walio hai waendao na waliojaa majini kulingana na aina zao na kila kiumbe mwenye mabawa anayeruka, kulingana na aina yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. 22  Basi Mungu akawabariki akisema: “Zaeni, muwe wengi na kujaza maji ya bahari,+ na viumbe wanaoruka wawe wengi duniani.” 23  Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya tano. 24  Kisha Mungu akasema: “Dunia na itokeze viumbe walio* hai kulingana na aina zao, wanyama wa kufugwa na wanyama wanaotambaa* na wanyama wa mwituni kulingana na aina zao.”+ Na ikawa hivyo. 25  Kisha Mungu akaumba wanyama wa mwituni kulingana na aina zao na wanyama wa kufugwa kulingana na aina zao na wanyama wote wanaotambaa kulingana na aina zao. Mungu akaona kuwa ni vyema. 26  Kisha Mungu akasema: “Na tufanye+ mtu kwa mfano+ wetu, kulingana na sura+ yetu, nao watawale samaki wa baharini na viumbe wanaoruka angani na wanyama wa kufugwa na dunia yote na kila mnyama anayetambaa duniani.”+ 27  Basi Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimuumba; mwanamume na mwanamke aliwaumba.+ 28  Zaidi ya hilo, Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: “Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia+ na kuitiisha,+ na mtawale+ samaki wa baharini na viumbe wanaoruka angani na kila kiumbe aliye hai anayetembea duniani.” 29  Kisha Mungu akasema: “Tazama nimewapa kila mmea duniani pote unaozaa mbegu na kila mti unaozaa matunda yenye mbegu. Itakuwa chakula chenu.+ 30  Na kila mnyama wa mwituni na kila kiumbe anayeruka angani na kila kiumbe mwenye uhai* anayetembea duniani, nimempa mimea yote ya kijani iwe chakula+ chake.” Ikawa hivyo. 31  Baada ya hayo Mungu akaona kila kitu alichoumba, na tazama! kilikuwa chema sana.+ Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya sita.

Maelezo ya Chini

Au “ukiwa.”
Au “maji yenye nguvu.”
Au “roho ya Mungu.”
Au “taa.”
Au “nafsi zilizo.”
Au “angani.”
Au “wanyama wakubwa sana.”
Au “nafsi.”
Au “wanyama waendao,” inaonekana wanatia ndani wanyama wanaotambaa na jamii nyingine za wanyama zilizo tofauti na jamii nyinginezo.
Au “ambaye ni nafsi hai.”