Kulingana na Mathayo 28:1-20

  • Yesu afufuliwa (1-10)

  • Askari wapewa rushwa ili waseme uwongo (11-15)

  • Agizo la kufanya watu kuwa wanafunzi (16-20)

28  Baada ya Sabato, kulipokuwa kukipambazuka siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene na yule Maria mwingine wakaenda kulitazama kaburi.+  Na tazama! tetemeko kubwa la ardhi lilikuwa limetokea, kwa maana malaika wa Yehova* alikuwa ameshuka kutoka mbinguni akaja na kuliviringisha lile jiwe, naye alikuwa amelikalia.+  Alikuwa aking’aa kama radi, na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.+  Ndiyo, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu kwa sababu ya kumwogopa.  Lakini malaika akawaambia wale wanawake: “Msiogope, kwa maana ninajua mnamtafuta Yesu aliyeuawa kwenye mti.+  Hayupo hapa, kwa maana amefufuliwa kama alivyosema.+ Njooni, tazameni mahali alipokuwa amelala.  Basi nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba alifufuliwa kutoka kwa wafu, na tazama! anawatangulia kwenda Galilaya.+ Mtamwona huko. Tazama! Nimewaambia ninyi.”+  Basi, wakaondoka upesi kwenye kaburi la ukumbusho wakiwa na hofu na shangwe kubwa. Wakakimbia kwenda kuwajulisha wanafunzi wake.+  Na tazama! Yesu akakutana nao na kuwaambia: “Siku njema!” Wakamkaribia, wakamshika miguu na kumsujudia.* 10  Ndipo Yesu akawaambia: “Msiogope! Nendeni, mkawajulishe ndugu zangu ili waende Galilaya, na huko wataniona.” 11  Walipoondoka na kwenda, baadhi ya walinzi+ wakaenda jijini na kuwajulisha wakuu wa makuhani mambo yote yaliyotokea. 12  Baada ya wakuu wa makuhani na wazee kukutana na kushauriana, wakawapa wale wanajeshi kiasi kikubwa cha fedha 13  wakawaambia: “Semeni, ‘Wanafunzi wake walikuja usiku wakamwiba tulipokuwa tumelala usingizi.’+ 14  Na gavana akisikia, sisi tutamwelezea jambo hilo,* nanyi hamtahitaji kuwa na wasiwasi.” 15  Basi wakachukua zile fedha na kufanya kama walivyoagizwa, na hadithi hiyo imeenea miongoni mwa Wayahudi mpaka leo hii. 16  Hata hivyo, wale wanafunzi 11 wakaenda Galilaya+ kwenye mlima ambao Yesu alikuwa amepanga kukutana nao.+ 17  Walipomwona wakasujudu,* lakini baadhi yao walikuwa na shaka. 18  Yesu akakaribia na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.+ 19  Basi, nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,+ mkiwabatiza+ katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, 20  na kuwafundisha kushika mambo yote niliyowaamuru.+ Na tazama! mimi nipo pamoja nanyi sikuzote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”*+

Maelezo ya Chini

Au “kumwinamia.”
Tnn., “tutamshawishi.”
Au “wakamwinamia.”
Angalia Kamusi.