Kulingana na Mathayo 5:1-48

  • MAHUBIRI YA MLIMANI (1-48)

    • Yesu aanza kufundisha mlimani (1, 2)

    • Mambo tisa yanayoleta furaha (3-12)

    • Chumvi na nuru (13-16)

    • Yesu alikuja kutimiza Sheria (17-20)

    • Mashauri kuhusu hasira (21-26), uzinzi (27-30), talaka (31, 32), viapo (33-37), kulipiza kisasi (38-42), kupenda adui (43-48)

5  Alipouona umati, akapanda mlimani; na baada ya kuketi wanafunzi wake wakamjia.  Kisha akafungua kinywa chake akaanza kuwafundisha, akisema:  “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho,*+ kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao.  “Wenye furaha ni wale wanaoomboleza, kwa kuwa watafarijiwa.+  “Wenye furaha ni wale walio wapole,+ kwa kuwa watairithi dunia.+  “Wenye furaha ni wale walio na njaa na kiu+ ya uadilifu, kwa kuwa watashibishwa.*+  “Wenye furaha ni wale wenye rehema,+ kwa kuwa wataonyeshwa rehema.  “Wenye furaha ni wale walio safi moyoni,+ kwa kuwa watamwona Mungu.  “Wenye furaha ni wale wanaofanya amani,+ kwa kuwa wataitwa wana wa Mungu. 10  “Wenye furaha ni wale ambao wameteswa kwa ajili ya uadilifu,+ kwa kuwa Ufalme wa mbinguni ni wao. 11  “Wenye furaha ni ninyi, watu wanapowashutumu+ na kuwatesa+ na kuwasingizia kila aina ya uovu kwa sababu yangu.+ 12  Furahini na kushangilia sana,+ kwa kuwa thawabu+ yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwapo kabla yenu.+ 13  “Ninyi ndio chumvi ya dunia, lakini chumvi+ ikipoteza nguvu yake, ladha yake itarudishwaje? Haifai tena, inapaswa kutupwa nje+ na kukanyagwa-kanyagwa na watu. 14  “Ninyi ndio nuru ya ulimwengu.+ Jiji lililo mlimani haliwezi kufichwa. 15  Watu hawawashi taa na kuiweka chini ya kikapu* bali huiweka kwenye kinara cha taa ili iwaangazie wote walio ndani ya nyumba.+ 16  Vivyo hivyo, acheni nuru yenu iangaze mbele ya watu,+ ili waone matendo yenu mema+ na kumtukuza Baba yenu aliye mbinguni.+ 17  “Msifikiri nilikuja kuharibu Sheria au Manabii. Sikuja kuharibu, bali kutimiza.+ 18  Kwa kweli ninawaambia ni rahisi zaidi kwa mbingu na dunia kupitilia mbali, kuliko herufi moja iliyo ndogo zaidi au sehemu yoyote ya herufi kuondolewa katika Sheria mpaka mambo yote yatimie.+ 19  Kwa hiyo, yeyote anayevunja mojawapo ya amri hizi ndogo na kufundisha wengine kufanya hivyo, ataitwa mdogo kuhusiana na Ufalme wa mbinguni. Lakini yeyote anayeshika na kufundisha amri hizi ataitwa mkubwa kuhusiana na Ufalme wa mbinguni. 20  Kwa maana ninawaambia ikiwa uadilifu wenu hauzidi ule wa waandishi na Mafarisayo,+ hamtaingia kamwe katika Ufalme wa mbinguni.+ 21  “Mlisikia kwamba zamani watu waliambiwa: ‘Usiue,+ lakini yeyote anayeua atawajibika mahakamani.’+ 22  Hata hivyo, ninawaambia kila mtu anayeendelea kumkasirikia+ ndugu yake atawajibika mahakamani; na yeyote anayemtukana ndugu yake kwa neno la dharau atawajibika katika Mahakama Kuu; na yeyote anayesema, ‘Wewe mpumbavu usiyefaa kitu!’ atastahili moto wa Gehena.*+ 23  “Basi, ikiwa unaleta zawadi yako kwenye madhabahu+ na hapo unakumbuka kwamba ndugu yako ana jambo fulani dhidi yako, 24  iache zawadi yako hapo mbele ya madhabahu, uende zako. Kwanza fanya amani na ndugu yako, kisha urudi na kutoa zawadi yako.+ 25  “Suluhisha mambo upesi na mtu anayekushtaki, ukiwa naye njiani kwenda mahakamani, ili asikupeleke kwa hakimu, naye hakimu kwa mtumishi wa mahakama, nawe utupwe gerezani.+ 26  Hakika ninakuambia hutatoka humo mpaka utakapolipa sarafu yako ndogo ya mwisho.* 27  “Mlisikia kwamba ilisemwa: ‘Usifanye uzinzi.’+ 28  Lakini ninawaambia kila mtu anayeendelea kumtazama mwanamke+ na kumtamani tayari amefanya uzinzi naye moyoni+ mwake. 29  Basi, ikiwa jicho lako la kulia linafanya ujikwae, ling’oe na kulitupilia mbali.+ Kwa maana ni afadhali upoteze kiungo kimoja kuliko mwili wako wote utupwe katika Gehena.*+ 30  Pia, ikiwa mkono wako wa kulia unakufanya ujikwae, ukate na kuutupilia mbali.+ Kwa maana ni afadhali upoteze kiungo kimoja kuliko mwili wako wote utupwe katika Gehena.*+ 31  “Zaidi ya hayo, ilisemwa: ‘Yeyote anayemtaliki mke wake, anapaswa kumpa cheti cha talaka.’+ 32  Hata hivyo, ninawaambia kila mtu anayemtaliki mke wake kwa sababu nyingine isipokuwa uasherati,* anamweka katika kishawishi cha kufanya uzinzi, na yeyote anayemwoa mwanamke aliyetalikiwa anafanya uzinzi.+ 33  “Tena mlisikia kwamba zamani watu waliambiwa: ‘Usikose kutimiza kiapo chako,+ unapaswa kutimiza nadhiri zako kwa Yehova.’*+ 34  Hata hivyo, ninawaambia: Msiape kamwe+ kwa mbingu kwa sababu ni kiti cha ufalme cha Mungu; 35  wala kwa dunia kwa sababu ni mahali pake pa kuwekea miguu;+ wala kwa Yerusalemu kwa sababu ni jiji la Mfalme mkuu.+ 36  Usiape kwa kichwa chako kwa sababu huwezi kugeuza unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37  Acheni ‘Ndiyo’ yenu imaanishe ndiyo, na ‘Siyo’ yenu, siyo,+ kwa maana linalozidi hayo linatoka kwa yule mwovu.+ 38  “Mlisikia kwamba ilisemwa: ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’+ 39  Hata hivyo, ninawaambia: Msimzuie mtu mwovu, bali yeyote anayekupiga kofi kwenye shavu la kulia, mgeuzie pia shavu la kushoto.+ 40  Na ikiwa mtu anataka kukupeleka mahakamani ili alichukue vazi lako la ndani, mwachie pia vazi lako la nje;+ 41  na mtu mwenye mamlaka akikulazimisha uingie katika utumishi wa kilomita moja,* nenda naye kilomita mbili. 42  Mpe yule anayekuomba, wala usimpe kisogo yule anayetaka umkopeshe.*+ 43  “Mlisikia kwamba ilisemwa: ‘Lazima umpende jirani yako+ na kumchukia adui yako.’ 44  Hata hivyo, ninawaambia: Endeleeni kuwapenda adui zenu+ na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi,+ 45  ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni,+ kwa kuwa yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, na hunyesha mvua juu ya waadilifu na wasio waadilifu.+ 46  Kwa maana mkiwapenda wale wanaowapenda, mnapata thawabu gani?+ Je, wakusanya kodi hawafanyi vivyo hivyo? 47  Na mkiwasalimu ndugu zenu tu, mnafanya jambo gani lisilo la kawaida? Je, watu wa mataifa hawafanyi vivyo hivyo? 48  Basi lazima muwe wakamilifu* kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.+

Maelezo ya Chini

Au “walio na kiu au njaa ya kiroho; ombaomba wa kiroho.”
Au “watatoshelezwa.”
Au “kikapu cha kupimia.”
Mahali pa kuteketezea takataka nje ya Yerusalemu. Angalia Kamusi.
Tnn., “kwadrani ya mwisho.” Angalia Nyongeza B14.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Tnn., “maili moja.” Angalia Nyongeza B14.
Yaani, umkopeshe bila faida au riba.
Au “kamili.”