Ayubu 33:1-33
33 “Lakini sasa, Ayubu, tafadhali sikiliza maneno yangu;Sikiliza kila jambo nitakalosema.
2 Tazama, tafadhali! Ni lazima nifumbue kinywa changu;Ni lazima ulimi wangu uzungumze.*
3 Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+Na midomo yangu inasema kwa unyoofu mambo ninayojua.
4 Roho ya Mungu mwenyewe iliniumba,+Na pumzi ya Mweza-Yote mwenyewe ilinifanya niwe hai.+
5 Nijibu ikiwa unaweza;Niambie hoja zako; jitayarishe kujitetea.
6 Tazama! Mimi ni kama wewe mbele za Mungu wa kweli;Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+
7 Kwa hiyo usiniogope,Na uzito wa maneno yangu usikulemee.
8 Lakini nilisikia ukisema,Naam, niliendelea kusikia maneno haya,
9 ‘Mimi ni safi, sina dhambi;+Mimi ni safi, sina kosa.+
10 Lakini Mungu anatafuta sababu za kunipinga;Ananiona kuwa adui yake.+
11 Anaitia miguu yangu katika mikatale;Anavichunguza kwa makini vijia vyangu vyote.’+
12 Lakini umekosea kusema hivyo, kwa hiyo nitakujibu:
Mungu ni mkuu sana kuliko mwanadamu anayeweza kufa.+
13 Kwa nini unamlaumu Yeye?+
Je, ni kwa sababu hakujibu hoja zako zote?+
14 Kwa maana Mungu huzungumza mara moja na mara ya pili,Lakini hakuna yeyote anayesikiliza,
15 Huzungumza katika ndoto, maono ya usiku,+Watu wanaposhikwa na usingizi mzitoWanapolala vitandani mwao.
16 Kisha hufungua masikio yao+Na kuyakazia* maagizo yake kwao,
17 Ili kumwepusha mtu asitende dhambi+Na kumlinda mwanadamu asiwe na kiburi.+
18 Mungu huilinda nafsi yake isiingie* shimoni,*+Uhai wake usiangamizwe kwa upanga.*
19 Mtu hukaripiwa pia na maumivu kitandani mwakeNa mateso yasiyo na kikomo mifupani mwake,
20 Hivi kwamba nafsi yake inachukia* mkate,Naye anakataa hata chakula bora.+
21 Nyama ya mwili wake huisha hivi kwamba haionekani,Na mifupa yake iliyokuwa imefichika sasa imechomoza.*
22 Nafsi yake inakaribia* shimoni;*Uhai wake unawakaribia wale wanaoleta kifo.
23 Ikiwa kuna mjumbe* kwa ajili yake,Mtetezi mmoja kati ya elfu moja,Ili amwambie mwanadamu mambo manyoofu,
24 Basi Mungu humhurumia na kusema,‘Mwokoe asishuke shimoni!*+Nimepata fidia!+
25 Mwili wake na uwe na afya zaidi kuliko wakati wa ujana;+Na azirudie siku alizokuwa na nguvu za ujana.’+
26 Atamsihi Mungu,+ naye atamkubali,Naye atauona uso wa Mungu kwa kelele za shangwe,Na Mungu atamrudishia uadilifu Wake mwanadamu anayeweza kufa.
27 Mtu huyo atawatangazia* wanadamu,‘Nimetenda dhambi+ na kupotosha yaliyo sawa,Lakini sikupokea niliyostahili.*
28 Ameikomboa nafsi yangu isiingie* shimoni,*+Na uhai wangu utaona nuru.’
29 Kwa kweli, Mungu hufanya mambo haya yoteMara mbili, mara tatu, kwa ajili ya mwanadamu,
30 Ili kumrudisha kutoka shimoni,*Ili aweze kuangaziwa nuru ya uzima.+
31 Sikiliza, Ayubu! Nisikilize!
Nyamaza, nami nitaendelea kuzungumza.
32 Ikiwa una jambo la kusema, niambie.
Sema, kwa maana nataka kuthibitisha kwamba uko sahihi.
33 Ikiwa huna la kusema, unapaswa kunisikiliza;Nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Ni lazima ulimi wangu na kaakaa langu vizungumze.”
^ Tnn., “kuyatia muhuri.”
^ Au “kwa silaha.”
^ Au “kaburini.”
^ Au “huulinda uhai wake usiingie.”
^ Tnn., “uhai wake unachukia.”
^ Au “inaonekana waziwazi.”
^ Au “Uhai wake unakaribia.”
^ Au “kaburini.”
^ Au “malaika.”
^ Au “kaburini.”
^ Tnn., “atawaimbia.”
^ Au labda, “Nami sikupata faida.”
^ Au “Ameukomboa uhai wangu usiingie.”
^ Au “kaburini.”
^ Au “kaburini.”