Kulingana na Marko 16:1-8

  • Yesu anafufuliwa (1-8)

16  Basi wakati Sabato+ iliisha, Maria Magdalene, Maria+ mama ya Yakobo, na Salome wakanunua manukato ili wakuje na kuyapakaa kwenye mwili wa Yesu.+ 2  Na asubui sana, siku ya kwanza ya juma, wakati jua lilikuwa limetokea, wakakuja kwenye kaburi.*+ 3  Walikuwa wanaulizana: “Ni nani atatuviringishia jiwe kutoka kwenye muingilio wa kaburi?” 4  Lakini wakati waliinua macho, wakaona lile jiwe lilikuwa limeviringishwa, hata kama lilikuwa kubwa sana.+ 5  Wakati waliingia katika kaburi, wakamuona kijana mwanaume amekaa upande wa kuume, akiwa amevaa kanzu nyeupe, na wakashangaa sana. 6  Akawaambia: “Musishangae.+ Munamutafuta Yesu Munazareti mwenye aliuawa kwenye muti. Amefufuliwa;+ haiko hapa. Muangalie mahali walimulalisha.+ 7  Lakini muende, muambie wanafunzi wake na Petro, ‘Yesu anawatangulia kuingia Galilaya.+ Mutamuona kule, kama vile aliwaambia.’”+ 8  Basi wakati walitoka inje ya kaburi, wakakimbia, wakitetemeka na kushangaa sana. Na hawakumuambia mutu yeyote jambo lolote, kwa sababu walikuwa na woga.*+

Maelezo ya Chini

Ao “kaburi la ukumbusho.”
Kulingana na maandishi ya zamani yenye kutegemeka, Injili ya Marko inamalizikia kwenye maneno ya mustari wa 8. Angalia Nyongeza A3.