Kulingana na Marko 11:1-33

  • Yesu anaingia kwa ushindi (1-11)

  • Muti wa tini unalaaniwa (12-14)

  • Yesu anasafisha hekalu (15-18)

  • Kujifunza somo kutokana na muti wa tini wenye ulikauka (19-26)

  • Wanataka kujua mamlaka ya Yesu inatoka wapi (27-33)

11  Sasa wakati walikuwa wamekaribia Yerusalemu, Betfage na Betania+ kwenye Mulima wa Mizeituni, akatuma wawili kati ya wanafunzi wake,+ 2  na kuwaambia: “Muende katika kijiji chenye munaona mbele yenu, na wakati tu mutaingia ndani, mutakuta mwana-punda mwenye kufungwa, mwenye mupaka sasa hakuna mutu amekwisha kukaa juu yake. Mumufungue na mumulete hapa. 3  Na kama mutu anawaambia, ‘Sababu gani munafanya hivi?’ museme, ‘Bwana iko* na lazima yake na atamurudisha hapa sasa hivi.’” 4  Basi wakaenda na wakapata mwana-punda amefungwa kwenye mulango, inje karibu na barabara, na wakamufungua.+ 5  Lakini wamoja kati ya watu wenye walikuwa wanasimama pale wakawaambia: “Sababu gani munafungua mwana-punda huyo?” 6  Wakawaambia kama vile Yesu alikuwa amesema, na wakawaacha waende. 7  Wakamupelekea Yesu ule mwana-punda,+ wakaweka nguo zao za inje juu yake, na Yesu akakaa juu yake.+ 8  Pia, wengi wakatandika nguo zao za inje katika barabara, lakini wengine wakakata matawi yenye majani katika mashamba.+ 9  Na watu wenye walikuwa mbele na wale wenye walikuwa wanafuata nyuma wakaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Umuokoe, tunaomba!+ Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!*+ 10  Ubarikiwe Ufalme wenye unakuja wa baba yetu Daudi!+ Umuokoe, tunaomba, wewe mwenye kuwa kwenye nafasi za juu!” 11  Na akaingia Yerusalemu na kuenda katika hekalu, na akaangalia vitu vyote huku na huku, lakini kwa sababu saa ilikuwa tayari imepita, akatoka na kuenda Betania pamoja na wale Kumi na Mbili (12).+ 12  Siku yenye ilifuata, wakati walikuwa wanatoka Betania, akasikia njaa.+ 13  Akiwa mbali, akaona muti wa tini wenye majani, na akaenda kuona kama angepata kitu fulani juu ya muti huo. Lakini, wakati aliukaribia, hakupata kitu isipokuwa majani tu, kwa maana hakikukuwa kipindi cha tini. 14  Basi akauambia: “Mutu yeyote asikule tena matunda kutoka kwako hata siku moja.”+ Na wanafunzi wake walikuwa wanasikiliza. 15  Sasa wakafika Yerusalemu. Akiwa kule akaingia katika hekalu na akaanza kufukuza wale wenye walikuwa wanauzisha na kununua katika hekalu, na akapindua meza za wale wenye walikuwa wanabadilisha feza na viti vya wale wenye walikuwa wanauzisha njiwa,+ 16  na hakumuruhusu mutu yeyote apite katika hekalu akiwa na kitu chochote. 17  Alikuwa anafundisha na kuwaambia: “Je, haikuandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa ajili ya mataifa yote’?+ Lakini ninyi mumeifanya kuwa pango la wanyanganyi.”+ 18  Na wakubwa wa makuhani na waandishi wakasikia hayo, na wakaanza kutafuta namna ya kumuua;+ kwa maana walimuogopa, kwa sababu watu wote walishangazwa na mafundisho yake.+ 19  Wakati ilifika mangaribi, wakatoka katika muji. 20  Lakini wakati walikuwa wanapita asubui sana, wakaona ule muti wa tini tayari umekauka kuanzia kwenye mizizi yake.+ 21  Petro, akakumbuka maneno ya Yesu, akamuambia: “Rabi, ona! ule muti wa tini wenye ulilaani umekauka.”+ 22  Yesu akajibu na kuwaambia: “Mukuwe na imani katika Mungu. 23  Kwa kweli ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye anaambia mulima huu, ‘Ondoka na utupwe katika bahari,’ na hana mashaka katika moyo wake lakini iko* na imani kwamba mambo yenye anasema yatafanyika, ni vile yatafanyika.+ 24  Ndiyo sababu ninawaambia ninyi, mambo yote yenye munaomba katika sala, mukuwe na imani kwamba mumekwisha kuyapokea, na mutayapata.+ 25  Na wakati munasimama ili kusali, musamehe watu makosa yote yenye waliwatendea, ili Baba yenu wa mbinguni awasamehe ninyi pia makosa yenu.”+ 26 *⁠ —— 27  Wakakuja tena Yerusalemu. Na wakati alikuwa anatembea katika hekalu, wakubwa wa makuhani na waandishi na wazee wakakuja 28  na kumuambia: “Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani? Ao ni nani alikupatia mamlaka hii ya kufanya mambo haya?”+ 29  Yesu akawaambia: “Nitawauliza ulizo moja. Munijibu, na mimi nitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani. 30  Ubatizo wa Yohana+ ulitoka mbinguni ao kwa wanadamu? Munijibu.”+ 31  Kwa hiyo wakaanza kuambiana kati yao, na kusema: “Kama tunasema, ‘Ulitoka mbinguni,’ atasema, ‘Basi, sababu gani hamukumuamini?’ 32  Lakini je, tupime kusema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’?” Waliogopa watu, kwa maana wote waliona kwamba kwa kweli Yohana alikuwa nabii.+ 33  Basi wakamujibu Yesu: “Hatujue.” Yesu akawaambia: “Na mimi pia sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “eko.”