Kulingana na Marko 6:1-56

  • Yesu anakataliwa katika muji wa kwao (1-6)

  • Wale Kumi na Mbili wanapewa maagizo juu ya utumishi (7-13)

  • Kifo cha Yohana Mubatizaji (14-29)

  • Yesu analisha watu elfu tano (30-44)

  • Yesu anatembea juu ya maji (45-52)

  • Yesu anaponyesha watu katika Genesareti (53-56)

6  Akatoka pale na kuingia katika eneo la kwao,+ na wanafunzi wake wakamufuata.  Wakati siku ya Sabato ilifika, akaanza kufundisha katika sinagogi, na wengi kati ya wale wenye walimusikiliza wakashangaa na kusema: “Mutu huyu alipata wapi mambo haya?+ Na sababu gani alipewa hekima hii, na matendo haya yenye nguvu ili yafanyike kupitia mikono yake?+  Huyu ni ule seremala,+ mwana wa Maria+ na ndugu ya Yakobo,+ Yosefu, Yuda, na Simoni,+ haiko vile? Na dada zake, je, hawako hapa pamoja na sisi?” Basi wakaanza kukwazika kwa sababu yake.  Lakini Yesu akawaambia: “Nabii anaheshimiwa kila mahali isipokuwa katika eneo la kwao na kati ya watu wa jamaa yake na katika nyumba yake mwenyewe.”+  Basi, hakuweza kufanya tendo lolote lenye nguvu kule, isipokuwa kuweka mikono yake juu ya wagonjwa kidogo na kuwaponyesha.  Kwa kweli, alishangaa kuona walikosa imani. Na akaenda kuzunguka katika vijiji, akifundisha.+  Sasa akaita wale Kumi na Mbili (12) na akaanza kuwatuma wawili-wawili,+ na akawapatia mamlaka juu ya roho wachafu.+  Pia, akawaagiza wasibebe kitu chochote kwa ajili ya safari isipokuwa fimbo​—wasibebe mukate, wala mufuko wa chakula, wala feza* kwenye mikaba* yao+​—  lakini wavae viatu na wasivae nguo mbili.* 10  Pia, akawaambia: “Kila mahali kwenye mutaingia katika nyumba, mukae mule mupaka wakati mutatoka katika eneo hilo.+ 11  Na kila mahali watu hawawapokee ninyi wala kuwasikiliza, wakati munatoka pale, mukungute mavumbi yenye kuwa kwenye miguu yenu ili kuwa ushahidi kwao.”+ 12  Kisha wakatoka na kuhubiri kwamba watu wanapaswa kutubu,+ 13  na wakafukuza pepo wachafu wengi+ na kupakaa mafuta wagonjwa wengi na kuwaponyesha. 14  Sasa Mufalme Herode akasikia habari hizo, kwa sababu jina la Yesu lilijulikana sana, na watu walikuwa wanasema: “Yohana Mubatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu, na ndiyo sababu anafanya matendo yenye nguvu.”+ 15  Lakini wengine walikuwa wanasema: “Ni Eliya.” Pia, wengine walikuwa wanasema: “Ni nabii kama mumoja wa manabii wa zamani.”+ 16  Lakini wakati Herode alisikia jambo hilo, akasema: “Ule Yohana mwenye nilikata kichwa amefufuliwa.” 17  Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu wamukamate Yohana, akamufunga katika gereza kwa sababu ya Herodia, bibi ya Filipo ndugu yake, kwa kuwa Herode alikuwa amemuoa.+ 18  Kwa maana Yohana alikuwa anamuambia Herode: “Hauruhusiwe kuwa na bibi ya ndugu yako.”+ 19  Basi Herodia alimuwekea Yohana kinyongo* na alitaka kumuua, lakini hakuweza. 20  Kwa maana Herode alikuwa anaogopa Yohana, na alimujua kuwa mwenye haki na mutakatifu,+ na alikuwa anamulinda. Kisha kumusikiliza, alikosa kabisa afanye nini, lakini aliendelea kumusikiliza kwa furaha. 21  Lakini, siku yenye kufaa ilifika wakati Herode alitayarisha chakula cha mangaribi kwenye sikukuu ya kuzaliwa kwake,+ kwa ajili ya maofisa wakubwa na makamanda wa jeshi na watu wenye kujulikana sana wa Galilaya.+ 22  Na binti ya Herodia akaingia, akacheza dansi na kumufurahisha Herode na wale wenye walikuwa wanakula* pamoja naye. Mufalme akamuambia huyo mutoto mwanamuke: “Niombe kila kitu chenye unataka, na nitakupatia.” 23  Ndiyo, akamuapia: “Kila kitu chenye utaniomba, nitakupatia, hata nusu ya ufalme wangu.” 24  Akaondoka na kuenda kumuuliza mama yake: “Niombe nini?” Akamuambia: “Kichwa cha Yohana Mubatizaji.” 25  Mara moja akaingia mbio kwa mufalme na kutoa ombi lake, na kusema: “Ninataka unipatie sasa hivi kwenye sahani kichwa cha Yohana Mubatizaji.”+ 26  Jambo hilo lilimuhuzunisha sana mufalme, lakini hakutaka kuzarau ombi lake, kwa sababu alikuwa ameapa mbele ya wageni wake.* 27  Basi mufalme akamutuma mara moja mulinzi na kumuamuru alete kichwa cha Yohana. Kwa hiyo akaenda na kumukata kichwa katika gereza 28  na akakileta kwenye sahani. Akakipatia ule kijana mwanamuke, na huyo kijana mwanamuke akakipatia mama yake. 29  Wakati wanafunzi wake walisikia jambo hilo, wakakuja na kubeba mwili wake na kuutia katika kaburi.* 30  Mitume wakakusanyika kumuzunguka Yesu na wakamuelezea mambo yote yenye walikuwa wamefanya na kufundisha.+ 31  Na akawaambia: “Mukuje ninyi wenyewe mahali kwenye hakuna watu ili mupumuzike kidogo.”+ Kwa maana watu wengi walikuwa wanakuja na kuenda, na hawakupata hata wakati wa kula chakula. 32  Basi wakapanda katika mashua* na kuenda mahali kwenye hakuna watu ili wakuwe peke yao.+ 33  Lakini watu wakawaona wakienda, na wengi wakajua jambo hilo. Na watu wakatoka katika miji yote, wakakimbia pamoja kwa miguu na wakawatangulia kufika kule. 34  Basi, wakati alitoka katika mashua,* akaona watu wengi sana, na akawasikilia huruma,+ kwa sababu walikuwa kama kondoo wenye hawana muchungaji.+ Na akaanza kuwafundisha mambo mengi.+ 35  Lakini sasa saa ilikuwa imepita, na wanafunzi wake wakakuja kwenye alikuwa na kusema: “Mahali hapa hakuna watu, na saa imekwisha kupita.+ 36  Waache warudie, ili waende katika eneo la mashamba la pembeni-pembeni na katika vijiji, wajinunulie chakula.”+ 37  Akawajibu: “Ninyi muwapatie chakula.” Halafu wakamuambia: “Je, tuende na kununua mikate ya dinari* mia mbili (200) na kupatia watu waikule?”+ 38  Akawaambia: “Muko na mikate ngapi? Muende muangalie!” Kisha kuhakikisha, wakasema: “Mikate tano (5) na samaki wawili.”+ 39  Akaagiza watu wote wakae vikundi-vikundi kwenye majani ya mubichi.+ 40  Basi wakakaa katika vikundi vya watu mia moja (100) na vya watu makumi tano (50). 41  Akakamata sasa ile mikate tano (5) na wale samaki wawili, akaangalia juu mbinguni na akatoa baraka.+ Kisha akavunja ile mikate na kuanza kuipatia wanafunzi ili waiweke mbele ya watu, na akagawia watu wote wale samaki wawili. 42  Kwa hiyo wote wakakula na kushiba, 43  na wakaokota vipande vyenye vilibakia, wakajaza vitunga kumi na mbili (12), bila kuhesabia samaki.+ 44  Wale wenye walikula mikate hiyo walikuwa wanaume elfu tano (5000). 45  Kisha, bila kukawia, akaambia wanafunzi wake wapande katika mashua* na wamutangulie kuenda ngambo ingine ya bahari kuelekea Betsaida, wakati yeye mwenyewe alikuwa anaaga wale watu wengi.+ 46  Lakini kisha kuwaaga, akaenda kwenye mulima ili kusali.+ 47  Wakati ilikuwa mangaribi, mashua* ilikuwa katikati ya bahari, lakini yeye alikuwa peke yake kwenye inchi kavu.+ 48  Basi, wakati aliwaona wakikazana sana kupiga makasia,* kwa kuwa upepo ulikuwa unawatokea kwa upande wa mbele, akakuja kwenye walikuwa akitembea juu ya bahari. Ilikuwa karibu na kesha la ine (4)* la usiku; lakini yeye alitaka* kuwapita. 49  Wakati walimuona akitembea juu ya bahari wakawaza: “Haya ni maono!” Na wakasema kwa sauti kubwa. 50  Kwa maana wote walimuona na wakavurugika. Lakini mara moja akasema nao na kuwaambia: “Mukuwe hodari! Ni mimi; musiogope.”+ 51  Kisha akapanda katika mashua* kwenye walikuwa, na upepo ukatulia. Halafu wakashangaa sana, 52  kwa maana hawakukuwa wameelewa maana ya ile mikate, lakini mioyo yao iliendelea kuwa mizito kuelewa. 53  Wakati walivuka mupaka kwenye inchi kavu, wakafika Genesareti na kutia nanga* pale karibu.+ 54  Lakini wakati tu walitoka katika mashua,* watu wakamutambua. 55  Wakakimbia kila mahali katika eneo hilo na wakaanza kuleta wagonjwa kwenye vitanda* na kuwapeleka mahali ­walisikia Yesu iko.* 56  Na kila mahali alikuwa anaingia katika vijiji, ao miji, ao katika eneo la mashamba, watu waliweka wagonjwa kwenye soko, na walikuwa wanamuomba awaruhusu waguse tu sehemu ya chini ya nguo yake ya inje.+ Na wote wenye waliigusa walipona.

Maelezo ya Chini

Tnn., “shaba.”
Ao “mishipi.”
Ao “nguo ingine.”
Ao “alimuwekea Yohana uchungu katika moyo.”
Ao “wale wenye walikuwa wanakaa kwenye meza.”
Ao “wale wenye walikuwa wanakaa kwenye meza.”
Ao “kaburi la ukumbusho.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Kasia ni chombo chenye kufanana na mwiko chenye kinatumiwa kuendesha mashua.
Ni kusema, karibu saa 9 ya usiku (3:00) mupaka karibu saa 12 ya asubui (6:00) wakati jua linatokea.
Ao “alikuwa karibu.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Nanga ni jiwe ao chuma chenye kufungwa kwa kamba ao kwa munyororo na kuingizwa ndani ya maji ili mashua isibebwe na maji.
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ni kusema, vitanda vya kubebea wagonjwa.
Ao “eko.”