Kulingana na Marko 13:1-37
13 Wakati alikuwa anatoka katika hekalu, mumoja wa wanafunzi wake akamuambia: “Mwalimu, ona namna majiwe na majengo haya ni ya ajabu!”+
2 Lakini, Yesu akamuambia: “Unaona majengo haya makubwa? Hakuna jiwe lenye litaachwa hapa juu ya jiwe bila kuangushwa chini.”+
3 Wakati alikuwa amekaa kwenye Mulima wa Mizeituni, akiangalia hekalu, Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea wakamuuliza akiwa peke yake:
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama wakati mambo haya yote yatafika kwenye umalizio?”+
5 Kwa hiyo, Yesu akaanza kuwaambia: “Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwapotoshe.+
6 Wengi watakuja wakitumia jina langu, na kusema, ‘Mimi ndiye,’ na watapotosha watu wengi.
7 Zaidi ya hayo, wakati mutasikia juu ya vita na habari za vita, musiogope; mambo hayo lazima yatokee, lakini ule mwisho bado.+
8 “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme;+ kutakuwa matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine; pia kutakuwa upungufu wa chakula.+ Mambo hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.+
9 “Lakini ninyi mukuwe waangalifu. Watu watawapeleka ninyi kwenye tribinali ya kidogo,+ na mutapigwa katika masinagogi+ na kusimamishwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwatolea ushahidi.+
10 Tena, katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe kwanza.+
11 Na wakati watawakamata ninyi ili kuwapeleka, musianze kuhangaika juu ya mambo yenye mutasema; lakini mambo yenye mutapewa saa ile, muyaseme, kwa sababu haiko ninyi munasema, lakini ni roho takatifu.+
12 Zaidi ya hayo, ndugu atatoa ndugu yake ili auawe, na baba atatoa mutoto wake, na watoto wataasi wazazi wao na kufanya wauawe.+
13 Na mutachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ Lakini ule mwenye atavumilia* mupaka mwisho+ ataokolewa.+
14 “Hata hivyo, wakati mutaona lile chukizo lenye linaleta uharibifu+ likiwa limesimama mahali halipaswe kuwa (musomaji atumie utambuzi), basi wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.+
15 Mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba asishuke wala asiingie ndani ili kukamata kitu chochote katika nyumba yake;
16 na mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma ili kukamata nguo yake ya inje.
17 Ole wao wanamuke wenye mimba na wale wenye kunyonyesha watoto katika siku hizo!+
18 Muendelee kusali kwamba mambo hayo yasifike katika kipindi cha baridi;
19 kwa maana siku hizo zitakuwa siku za taabu+ yenye haijatokea tangu mwanzo wa uumbaji wenye Mungu aliumba, mupaka wakati huo, na haitatokea tena.+
20 Kwa kweli, kama Yehova* hangefupisha siku hizo, hakuna mwili wowote wenye ungeokolewa. Lakini kwa sababu ya wale wenye amechagua, amefupisha siku hizo.+
21 “Basi, pia kama mutu yeyote anawaambia ninyi, ‘Muone, Kristo iko* hapa,’ ao, ‘Muone, iko* pale,’ musiamini jambo hilo.+
22 Kwa maana Makristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea+ na watafanya alama na maajabu ili kudanganya,* ikiwezekana, wale wenye kuchaguliwa.
23 Basi ninyi, mufanye angalisho.+ Nimewaambia mambo yote mbele ya wakati.
24 “Lakini katika siku hizo, kisha taabu hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake,+
25 na nyota zitakuwa zinaanguka kutoka mbinguni, na nguvu zenye kuwa mbinguni zitatikiswa.
26 Na kisha wataona Mwana wa binadamu+ akikuja katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.+
27 Na kisha atatuma malaika na kukusanya watu wake wenye kuchaguliwa kutoka pande ine (4) za dunia,* kutoka mwisho wa dunia mupaka mwisho wa mbingu.+
28 “Sasa mujifunze mufano huu kuhusu muti wa tini: Wakati tu matawi yake machanga yanakuwa teketeke na kutoa majani, munajua kwamba kipindi cha joto kinakaribia.+
29 Vilevile ninyi pia, wakati mutaona mambo hayo yanatokea, mujue kwamba iko* karibu kwenye milango.+
30 Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapita hata kidogo mupaka mambo haya yote yatokee.+
31 Mbingu na dunia zitapita,+ lakini maneno yangu hayatapita hata kidogo.+
32 “Kuhusu siku ile ao saa ile hakuna mutu mwenye anajua, ikuwe malaika mbinguni wala Mwana, lakini Baba tu.+
33 Mufanye angalisho, muendelee kukesha,+ kwa maana hamujue wakati wenye uliwekwa utafika wakati gani.+
34 Ni kama mutu mwenye alisafiri na kuenda katika inchi ingine, akaacha nyumba yake na akapatia watumwa wake mamlaka,+ kila mumoja kazi yake, na akaamuru mulinzi wa mulango aendelee kukesha.+
35 Kwa hiyo, muendelee kukesha, kwa maana hamujue bwana wa nyumba atakuja wakati gani,+ kama ni mangaribi, ao katikati ya usiku, ao mbele ya mapambazuko,* ao asubui sana,+
36 ili wakati atafika kwa kushitukia, asiwakute mumelala usingizi.+
37 Lakini kile ninawaambia ninyi, ninaambia watu wote: Muendelee kukesha.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “anavumilia.”
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “kupotosha.”
^ Tnn., “pepo ine za dunia.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “wakati jogoo anawika.” Mapambazuko ni wakati mwangaza wa Asubui unaanza kutokea.