Kulingana na Marko 13:1-37

  • UMALIZIO WA MUPANGILIO WA MAMBO (1-37)

    • Vita, matetemeko ya inchi, upungufu wa chakula (8)

    • Lazima habari njema ihubiriwe (10)

    • Taabu kubwa (19)

    • Kuja kwa Mwana wa binadamu (26)

    • Mufano wa muti wa tini (28-31)

    • Muendelee kukesha (32-37)

13  Wakati alikuwa anatoka katika hekalu, mumoja wa wanafunzi wake akamuambia: “Mwalimu, ona namna majiwe na majengo haya ni ya ajabu!”+  Lakini, Yesu akamuambia: “Unaona majengo haya makubwa? Hakuna jiwe lenye litaachwa hapa juu ya jiwe bila kuangushwa chini.”+  Wakati alikuwa amekaa kwenye Mulima wa Mizeituni, akiangalia hekalu, Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea wakamuuliza akiwa peke yake:  “Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama wakati mambo haya yote yatafika kwenye umalizio?”+  Kwa hiyo, Yesu akaanza kuwaambia: “Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwapotoshe.+  Wengi watakuja wakitumia jina langu, na kusema, ‘Mimi ndiye,’ na watapotosha watu wengi.  Zaidi ya hayo, wakati mutasikia juu ya vita na habari za vita, musiogope; mambo hayo lazima yatokee, lakini ule mwisho bado.+  “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme;+ kutakuwa matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine; pia kutakuwa upungufu wa chakula.+ Mambo hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.+  “Lakini ninyi mukuwe waangalifu. Watu watawapeleka ninyi kwenye tribinali ya kidogo,+ na mutapigwa katika masinagogi+ na kusimamishwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu, ili kuwatolea ushahidi.+ 10  Tena, katika mataifa yote, lazima habari njema ihubiriwe kwanza.+ 11  Na wakati watawakamata ninyi ili kuwapeleka, musianze kuhangaika juu ya mambo yenye mutasema; lakini mambo yenye mutapewa saa ile, muyaseme, kwa sababu haiko ninyi munasema, lakini ni roho takatifu.+ 12  Zaidi ya hayo, ndugu atatoa ndugu yake ili auawe, na baba atatoa mutoto wake, na watoto wataasi wazazi wao na kufanya wauawe.+ 13  Na mutachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu.+ Lakini ule mwenye atavumilia* mupaka mwisho+ ataokolewa.+ 14  “Hata hivyo, wakati mutaona lile chukizo lenye linaleta uharibifu+ likiwa limesimama mahali halipaswe kuwa (musomaji atumie utambuzi), basi wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.+ 15  Mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba asishuke wala asiingie ndani ili kukamata kitu chochote katika nyumba yake; 16  na mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma ili kukamata nguo yake ya inje. 17  Ole wao wanamuke wenye mimba na wale wenye kunyonyesha watoto katika siku hizo!+ 18  Muendelee kusali kwamba mambo hayo yasifike katika kipindi cha baridi; 19  kwa maana siku hizo zitakuwa siku za taabu+ yenye haijatokea tangu mwanzo wa uumbaji wenye Mungu aliumba, mupaka wakati huo, na haitatokea tena.+ 20  Kwa kweli, kama Yehova* hangefupisha siku hizo, hakuna mwili wowote wenye ungeokolewa. Lakini kwa sababu ya wale wenye amechagua, amefupisha siku hizo.+ 21  “Basi, pia kama mutu yeyote anawaambia ninyi, ‘Muone, Kristo iko* hapa,’ ao, ‘Muone, iko* pale,’ musiamini jambo hilo.+ 22  Kwa maana Makristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea+ na watafanya alama na maajabu ili kudanganya,* ikiwezekana, wale wenye kuchaguliwa. 23  Basi ninyi, mufanye angalisho.+ Nimewaambia mambo yote mbele ya wakati. 24  “Lakini katika siku hizo, kisha taabu hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake,+ 25  na nyota zitakuwa zinaanguka kutoka mbinguni, na nguvu zenye kuwa mbinguni zitatikiswa. 26  Na kisha wataona Mwana wa binadamu+ akikuja katika mawingu akiwa na nguvu nyingi na utukufu.+ 27  Na kisha atatuma malaika na kukusanya watu wake wenye kuchaguliwa kutoka pande ine (4) za dunia,* kutoka mwisho wa dunia mupaka mwisho wa mbingu.+ 28  “Sasa mujifunze mufano huu kuhusu muti wa tini: Wakati tu matawi yake machanga yanakuwa teketeke na kutoa majani, munajua kwamba kipindi cha joto kinakaribia.+ 29  Vilevile ninyi pia, wakati mutaona mambo hayo yanatokea, mujue kwamba iko* karibu kwenye milango.+ 30  Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapita hata kidogo mupaka mambo haya yote yatokee.+ 31  Mbingu na dunia zitapita,+ lakini maneno yangu hayatapita hata kidogo.+ 32  “Kuhusu siku ile ao saa ile hakuna mutu mwenye anajua, ikuwe malaika mbinguni wala Mwana, lakini Baba tu.+ 33  Mufanye angalisho, muendelee kukesha,+ kwa maana hamujue wakati wenye uliwekwa utafika wakati gani.+ 34  Ni kama mutu mwenye alisafiri na kuenda katika inchi ingine, akaacha nyumba yake na akapatia watumwa wake mamlaka,+ kila mumoja kazi yake, na akaamuru mulinzi wa mulango aendelee kukesha.+ 35  Kwa hiyo, muendelee kukesha, kwa maana hamujue bwana wa nyumba atakuja wakati gani,+ kama ni mangaribi, ao katikati ya usiku, ao mbele ya mapambazuko,* ao asubui sana,+ 36  ili wakati atafika kwa kushitukia, asiwakute mumelala usingizi.+ 37  Lakini kile ninawaambia ninyi, ninaambia watu wote: Muendelee kukesha.”+

Maelezo ya Chini

Ao “anavumilia.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “kupotosha.”
Tnn., “pepo ine za dunia.”
Ao “eko.”
Tnn., “wakati jogoo anawika.” Mapambazuko ni wakati mwangaza wa Asubui unaanza kutokea.