Kulingana na Luka 4:1-44

  • Ibilisi amjaribu Yesu (1-13)

  • Yesu aanza kuhubiri huko Galilaya (14, 15)

  • Yesu akataliwa huko Nazareti (16-30)

  • Yesu akiwa katika sinagogi huko Kapernaumu (31-37)

  • Mama mkwe wa Simoni na wagonjwa wengine waponywa (38-41)

  • Umati wampata Yesu katika eneo lisilo na watu (42-44)

4  Basi Yesu, akiwa amejaa roho takatifu, akaondoka Yordani, naye akaongozwa na roho kwenda nyikani+  kwa siku 40, akijaribiwa na Ibilisi.+ Kipindi hicho chote hakula chakula, basi muda huo ulipokwisha, akahisi njaa.  Ndipo Ibilisi akamwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.”  Lakini Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu hataishi kwa mkate tu.’”+  Basi akampeleka juu na kumwonyesha mara moja falme zote za dunia inayokaliwa.+  Kisha Ibilisi akamwambia: “Nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa,+ nami humpa yeyote ninayetaka.  Kwa hiyo, ukifanya tendo la ibada mbele yangu, yote itakuwa yako.”  Yesu akamjibu: “Imeandikwa, ‘Yehova* Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’”+  Kisha akampeleka Yerusalemu, akamsimamisha juu ya mnara wa* hekalu na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa,+ 10  kwa maana imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe, ili wakulinde,’ 11  nao, ‘Watakubeba mikononi mwao, ili mguu wako usigonge jiwe.’”+ 12  Yesu akamjibu: “Imesemwa, ‘Usimjaribu Yehova* Mungu wako.’”+ 13  Kwa hiyo Ibilisi, alipomaliza majaribu yote, akamwacha mpaka wakati mwingine unaofaa.+ 14  Basi Yesu akarudi Galilaya+ katika nguvu za roho. Na habari nzuri kumhusu zikaenea katika maeneo yote yaliyo karibu. 15  Pia, akaanza kufundisha katika masinagogi yao, naye akaheshimiwa na watu wote. 16  Kisha akaenda Nazareti,+ mahali alipolelewa, na kulingana na desturi yake siku ya Sabato, akaingia katika sinagogi+ naye akasimama ili kusoma. 17  Basi akapewa kitabu cha kukunjwa cha nabii Isaya, akakifungua na kupata mahali palipoandikwa: 18  “Roho ya Yehova* iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta ili niwatangazie maskini habari njema. Alinituma niwatangazie mateka uhuru na vipofu kuona tena, kuwaweka huru waliopondeka,+ 19  kuhubiri mwaka wa Yehova* unaokubalika.”+ 20  Ndipo akakikunja kitabu hicho na kumrudishia mtumishi, kisha akaketi; na wote katika sinagogi walikuwa wakimtazama kwa makini. 21  Akaanza kuwaambia: “Leo andiko hili ambalo mmetoka kusikia limetimia.”+ 22  Wote wakaanza kutoa ushahidi unaofaa kumhusu na kushangazwa na maneno yenye neema yaliyokuwa yakitoka kinywani mwake,+ nao wakawa wakiambiana: “Huyu ni mwana wa Yosefu, sivyo?”+ 23  Ndipo akawaambia: “Bila shaka mtautumia mfano huu kwangu, ‘Daktari, jiponye mwenyewe. Fanya pia katika eneo la nyumbani kwenu mambo tuliyosikia yamefanywa huko Kapernaumu.’”+ 24  Basi akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia hakuna nabii anayekubaliwa katika eneo la nyumbani kwao.+ 25  Kwa mfano, kwa kweli ninawaambia: Kulikuwa na wajane wengi Israeli siku za Eliya, mbingu zilipofungwa kwa miaka mitatu na miezi sita, kukawa na njaa kubwa katika nchi yote.+ 26  Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote kati ya wanawake hao, bali kwa mjane mmoja huko Sarefathi katika nchi ya Sidoni.+ 27  Pia, kulikuwa na wenye ukoma wengi Israeli siku za nabii Elisha; lakini hakuna hata mmoja wao aliyetakaswa,* ila Naamani Msiria.”+ 28  Ndipo wote katika sinagogi waliokuwa wakisikia mambo hayo wakajawa na hasira,+ 29  wakasimama na kumtoa haraka nje ya jiji mpaka kwenye ukingo wa mlima ambao jiji lao lilikuwa limejengwa, ili wamtupe chini. 30  Lakini akapita katikati yao na kwenda zake.+ 31  Kisha akashuka kwenda jiji la Kapernaumu, huko Galilaya. Naye alikuwa akiwafundisha siku ya Sabato,+ 32  nao wakashangazwa na njia yake ya kufundisha,+ kwa sababu alikuwa akizungumza kwa mamlaka. 33  Basi katika sinagogi kulikuwa na mtu mwenye roho mwovu, naye akapiga kelele akisema:+ 34  “Ah! Kwa nini unatusumbua, wewe Yesu Mnazareti?+ Je, umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani, Mtakatifu wa Mungu.”+ 35  Lakini Yesu akamkemea, akisema: “Nyamaza na umtoke.” Basi baada ya kumwangusha mtu huyo mbele yao, yule roho mwovu akamtoka bila kumuumiza. 36  Wote wakashangaa na kuanza kuambiana: “Anazungumza kwa mamlaka sana! Anawaagiza roho waovu kwa mamlaka na nguvu, nao wanatoka!” 37  Basi habari kumhusu zikazidi kuenea kila mahali katika maeneo yaliyokuwa karibu. 38  Alipotoka katika sinagogi akaenda nyumbani kwa Simoni. Mama mkwe wa Simoni alikuwa na homa kali, wakamwomba Yesu amponye.+ 39  Yesu akasimama kando yake, akaikemea ile homa, ikaisha. Papo hapo akasimama na kuanza kuwahudumia. 40  Jua lilipokuwa likitua, wote waliokuwa na watu wenye magonjwa mbalimbali wakawaleta kwake. Akawaponya kwa kuweka mikono yake juu ya kila mgonjwa.+ 41  Roho waovu pia wakawatoka watu wengi, wakipaza sauti na kusema: “Wewe ndiye Mwana wa Mungu.”+ Lakini aliwakemea na hakuwaruhusu waseme,+ kwa maana walijua yeye ni Kristo.+ 42  Hata hivyo, kulipopambazuka, akaenda mahali pasipo na watu.+ Lakini umati ukaanza kumtafuta* na walipofika mahali alipokuwa, wakajaribu kumzuia asiondoke. 43  Lakini akawaambia: “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika majiji mengine, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”+ 44  Basi akaendelea kuhubiri katika masinagogi ya Yudea.

Maelezo ya Chini

Au “ukuta wa ukingoni wa; sehemu ya juu zaidi ya.”
Au “aliyeponywa.”
Au “kumwinda”