Yobu 38:1-41
38 Kisha Yehova akamujibu Yobu katika zoruba yenye upepo mukali:+
2 “Ni nani huyu mwenye kutia giza mashauri yanguNa kuzungumuza bila ujuzi?+
3 Tafazali, ujitayarishe kama mwanaume;Nitakuuliza maulizo, na wewe uniambie.
4 Ulikuwa wapi wakati niliweka misingi ya dunia?+
Uniambie, ikiwa unawaza kama unajua.
5 Ni nani aliweka vipimo vyake, kama unajua,Ao ni nani mwenye alinyoosha kamba ya kupimia kutoka upande wake mumoja mupaka upande wake mwingine?
6 Vikalio vyake vimeingizwa ndani ya nini,Ao ni nani aliweka jiwe lake la pembe,+
7 Wakati nyota za asubui+ zilipiga pamoja vigelele vya shangwe,Na wana wote wa Mungu*+ walianza kupandisha sauti za shangwe?
8 Na ni nani alifungia bahari nyuma ya milango+Wakati ilitoka kwa nguvu katika tumbo la uzazi,
9 Wakati niliivalisha mawinguNa kuifunika* katika giza nzito,
10 Wakati niliiwekea mupaka wanguNa kutia mapingo* yake na milango mahali pake,+
11 Na nilisema, ‘Unaweza kufika mupaka hapa, na usiende mbali na hapa;Ni hapa mawimbi yako yenye majivuno yatasimamia’?+
12 Je, kuko siku umepatia asubui amriAo kuonyesha mapambazuko* mahali pake,+
13 Ili yashike miisho ya duniaNa kutikisa watu waovu watoke ndani yake?+
14 Dunia inabadilishwa kama vile udongo wa mufinyanzi* chini ya muhuri,Na vitu vyenye kuwa ndani yake vinangaa kama vile mapambo ya nguo.
15 Lakini mwangaza wa watu waovu unaondolewa juu yao,Na mukono wao wenye kuinuliwa unavunjwa.
16 Je, umeshuka kwenye chemchemi za bahariAo umechunguza maji yenye kuenda chini sana?+
17 Je, umeonyeshwa milango mikubwa ya kifo,+Ao umeona milango mikubwa ya giza nzito?*+
18 Je, umeelewa ukubwa wa eneo la dunia?+
Uniambie, kama unajua mambo hayo yote.
19 Mwangaza unakaa upande gani?+
Na mahali giza linakaa ni wapi,
20 Ili ulipeleke kwenye eneo lakeNa kuelewa njia zenye kuenda kwenye nyumba yake?
21 Je, unajua mambo hayo kwa sababu ulikuwa umekwisha kuzaliwaNa kwa sababu hesabu ya miaka yako* ni kubwa?
22 Je, umeingia ndani ya madepo ya teluji,*+Ao umeona madepo ya mvua ya majiwe,+
23 Yenye nimeweka kwa ajili ya siku ya taabu,Kwa ajili ya siku ya mapigano na vita?+
24 Mwangaza* unasambazwa kutoka upande gani,Na upepo wa mashariki unavuma juu ya dunia kutoka wapi?+
25 Ni nani ametengeneza mufereji kwa ajili ya mafurikoNa kutengeneza njia kwa ajili ya wingu la zoruba yenye kunguruma,+
26 Ili kufanya mvua inyeshe mahali kwenye mwanadamu haishi,Juu ya jangwa kwenye hakuna watu,+
27 Ili kushibisha maeneo yenye yameharibiwa ambayo yameachwaNa kufanya majani yaote tena?+
28 Je, mvua iko na baba,+Ao ni nani alizaa matone ya umande?+
29 Barafu ilitoka katika tumbo la uzazi la nani,Na ni nani alizaa barafu nyembamba ya mbinguni+
30 Wakati maji yanakuwa kama vile yamefunikwa na jiwe,Na uso wa maji yenye kuenda chini sana unagandamana?+
31 Unaweza kufunga kamba za kundi la nyota la Kima*Ao kufungua kamba za kundi la nyota la Kesili?*+
32 Je, unaweza kuleta kundi la nyota* katika wakati wakeAo kuongoza kundi la nyota la Ashi* pamoja na wana wake?
33 Je, unajua sheria zenye zinaongoza mbingu,+Ao unaweza kuzilazimisha zikuwe na mamlaka juu ya dunia?
34 Je, unaweza kupandisha sauti yako mupaka kwenye mawinguIli kufanya mafuriko ya maji yakufunike?+
35 Je, unaweza kutuma miali ya umeme wa radi?
Je, itakuja na kukuambia, ‘Sisi tuko hapa!’?
36 Ni nani alitia hekima ndani ya mawingu*+Ao kupatia maajabu ya anga* uelewaji?+
37 Ni nani mwenye kuwa na hekima ya kutosha ili kuhesabia mawingu,Ao nani mwenye anaweza kumwanga mitungi ya maji ya mbinguni+
38 Wakati mavumbi yanakuwa rundo la udongo wenye kugandamanaNa madonge ya udongo yanakamatana pamoja?
39 Je, unaweza kumuwindia simba mawindoAo kutosheleza hamu ya kula ya wana-simba+
40 Wakati wanashutama katika mashimo yaoAo kuvizia katika mapango yao?
41 Ni nani mwenye anatayarisha chakula kwa ajili ya kunguru+Wakati watoto wake wanamulilia Mungu awasaidieNa kutanga-tanga kwa sababu hakuna chakula?
Maelezo ya Chini
^ Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.
^ Ao “kuifunga kwa kitambaa.”
^ Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “kivuli cha kifo.”
^ Tnn., “siku zako.”
^ Ao “neige.”
^ Ao pengine, “Umeme wa radi.”
^ Pengine ni nyota zenye kuitwa Pleiadesi katika kundi la nyota la Taurusi, ao Ngombe.
^ Pengine ni kundi la nyota la Orioni.
^ Tnn., “Mazaroti.” Kwenye 2Fa 23:5, neno hilo linatumiwa ili kuzungumuzia makundi ya nyota ya zodiaki.
^ Pengine ni kundi la nyota la Dubu Mukubwa (Kundi Kubwa la Ursa).
^ Ao pengine, “ndani ya mwanadamu.”
^ Ao pengine, “akili.”