Yobu 36:1-33
-
Elihu anatukuza ukubwa wa Mungu wenye hauwezi kuchunguzwa (1-33)
36 Elihu akaendelea kusema:
2 “Univumilie kidogo wakati ninaendelea kueleza,Kwa maana ningali na maneno ya kusema kwa ajili ya Mungu.
3 Nitasema mingi juu ya mambo yenye ninajua,Na nitamutangaza Mutengenezaji wangu kuwa mwenye haki.+
4 Kwa kweli maneno yangu hayako ya uongo;Ule Mwenye kuwa mukamilifu katika ujuzi+ iko* hapa mbele yako.
5 Kwa kweli, Mungu ni mwenye nguvu+ na hakatae mutu yeyote;Yeye ni mukubwa katika nguvu zake za uelewaji;*
6 Hatalinda uzima wa watu waovu,+Lakini anapatia watu wenye kuteseka haki.+
7 Yeye haondoe macho yake juu ya watu wenye haki;+Anawaweka juu ya viti vya ufalme pamoja na wafalme,*+ nao wanatukuzwa milele.
8 Lakini kama wamefungwa kwa pinguNa kukamatwa katika kamba za mateso,
9 Anawafunulia mambo yenye wamefanya,Makosa yenye walitenda kwa sababu ya kiburi chao.
10 Anafungua masikio yao ili yasikie karipioNa anawaambia waache kutenda maovu.+
11 Kama wanatii na kumutumikia yeye,Wataishi siku zao zote katika hali ya muzuri,Na miaka yao itakuwa yenye kupendeza.+
12 Lakini kama hawatii, wataharibiwa kwa upanga*+Na watakufa bila ujuzi.
13 Watu wenye hawamuogope Mungu* katika moyo wao wataweka kinyongo.
Hawalilie musaada hata wakati anawafunga.
14 Wanakufa* wakati wangali vijana,+Wanapitisha* maisha yao kati ya makahaba wanaume wa hekalu.+
15 Lakini Mungu* anaokoa watu wenye kuteseka katika mateso yao;Anafungua sikio lao wakati wanakandamizwa.
16 Anakuokoa wakati unakaribia kuingia katika taabu+Na kukupeleka mahali kwenye nafasi kubwa, kwenye hakuna kizuizi,+Kwenye meza yenye chakula kingi kizuri ili kukufariji.+
17 Kisha utatosheka na hukumu yenye itapata watu waovu,+Wakati hukumu itatolewa na haki kutetewa.
18 Lakini ukuwe muangalifu ili kasirani isikufanye ukuwe na chuki,*+Na usiruhusu rushwa* kubwa ikupotoshe.
19 Je, kilio chako cha kuomba musaadaAo bidii yako nyingi inaweza kukuzuia usipatwe na taabu?+
20 Usitamani usiku,Wakati watu wanaangamia kutoka mahali pao.
21 Ukuwe muangalifu kwamba usigeuke ili kufanya maovu,Kwa kuchagua maovu pahali pa mateso.+
22 Angalia! Mungu ni mwenye kuinuliwa katika nguvu zake;Ni mufundishaji gani iko* kama yeye?
23 Ni nani ameongoza* njia yake+Ao kumuambia, ‘Jambo lenye umefanya ni kosa’?+
24 Usisahau kutukuza matendo yake,+Yenye wanadamu wameimba.+
25 Wanadamu wote wameyaona,Mwanadamu mwenye anaweza kufa ameyaangalia kwa mbali.
26 Ndiyo, Mungu ni mukubwa kuliko namna tunaweza kujua;+Hatuwezi hata kidogo kuelewa* hesabu ya miaka yake.+
27 Anakusanya juu matone ya maji;+Yanagandamana katika kunguku yake na kufanyiza mvua;
28 Kisha mawingu yanamwanga maji hayo chini;+Yananyesha kwa wingi juu ya wanadamu.
29 Je, mutu anaweza kuelewa namna mawingu yametandikwa,*Mungurumo wa radi kutoka katika hema yake?*+
30 Ona namna anasambaza juu yake umeme wake wa radi*+Na kufunika sehemu za chini kabisa za* bahari.
31 Kupitia njia hizo anatunza* vikundi vya watu;Na kuwapatia chakula kwa wingi.+
32 Anafunika umeme wa radi kwa mikono yake,Na anaiongoza ili ipige shabaha yake.+
33 Mungurumo wa radi yake unaeleza habari juu yake,Hata mifugo inaeleza mwenye anakuja.*
Maelezo ya Chini
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “moyo wake.”
^ Ao pengine, “Anaweka wafalme juu ya viti vya ufalme.”
^ Ao “kwa silaha.”
^ Ao “Waasi-imani.”
^ Ao “Nafsi zao zinakufa.”
^ Ao pengine, “Wanamalizia.”
^ Tnn., “Yeye.”
^ Ao “kata-midomo.”
^ Ao “upige mikono kwa zarau.”
^ Ao “eko.”
^ Ao pengine, “amemulaumu; amemuomba atoe hesabu kuhusu.”
^ Ao “kuchunguza.”
^ Ao “tabaka za mawingu.”
^ Tnn., “kibanda chake.”
^ Tnn., “mwangaza wake.”
^ Tnn., “mizizi ya.”
^ Ao pengine, “anatetea kesi ya hukumu ya.”
^ Ao pengine, “kitu chenye kinakuja.”

