Yobu 26:1-14
26 Yobu akajibu:
2 “Mumesaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa!
Mumeokoa mukono wenye hauna nguvu kabisa!+
3 Kwa kweli mumemupatia mutu mwenye hana hekima mashauri ya muzuri sana!+
Na mumefunua kwa wingi hekima yenu yenye kutenda!*
4 Munajaribu kusema na nani,Na ni nani aliwaongoza kusema mambo kama hayo?*
5 Wale wenye hawana uwezo katika kifo wanatetemeka;Wako chini hata kuliko maji na viumbe vyenye kukaa ndani yake.
6 Kaburi* liko uchi mbele ya Mungu,*+Na mahali pa uharibifu hapajafunikwa.*
7 Anatandika anga la kaskazini* mahali kwenye hakuna kitu,*+Ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu;
8 Anafunga maji katika mawingu yake,+Ili mawingu yasipasuke kwa sababu ya uzito wa maji;
9 Anafunika kiti chake cha ufalme kisionekane,Na anatandika wingu lake juu yake.*+
10 Anachora mwisho* kwenye uso wa maji;+Anaweka mupaka kati ya mwangaza na giza.
11 Nguzo za mbingu zinatikisika;Na zinashangaa sana kwa sababu ya kukemea kwake.
12 Anavuruga bahari kwa nguvu zake,+Na kwa uelewaji wake anavunja vipande-vipande munyama mukubwa wa bahari.*+
13 Kwa pumuzi yake* anasafisha anga;Mukono wake unatoboa nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza.
14 Angalia! Hizo ni sehemu za pembeni-pembeni tu za njia zake;+Ni sauti ya chini-chini tu ndiyo tumesikia juu yake!
Basi ni nani anaweza kuelewa mungurumo wake wenye nguvu?”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “akili.”
^ Tnn., “Na ni pumuzi (roho) ya nani yenye imetoka ndani yenu?”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Tnn., “yeye.”
^ Ao “Na Abadoni hajafunikwa.”
^ Tnn., “kaskazini.”
^ Tnn., “eneo tupu.”
^ Ni kusema, juu ya kiti chake cha ufalme.
^ Tnn., “muviringo.”
^ Tnn., “Rahabu.”
^ Tnn., “upepo wake.”