Yobu 26:1-14

  • Jibu la Yobu (1-14)

    • “Mumemusaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa!” (1-4)

    • ‘Mungu ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu’ (7)

    • ‘Sehemu za pembeni-pembeni tu za njia za Mungu’ (14)

26  Yobu akajibu:   “Mumesaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa! Mumeokoa mukono wenye hauna nguvu kabisa!+   Kwa kweli mumemupatia mutu mwenye hana hekima mashauri ya muzuri sana!+ Na mumefunua kwa wingi hekima yenu yenye kutenda!*   Munajaribu kusema na nani,Na ni nani aliwaongoza kusema mambo kama hayo?*   Wale wenye hawana uwezo katika kifo wanatetemeka;Wako chini hata kuliko maji na viumbe vyenye kukaa ndani yake.   Kaburi* liko uchi mbele ya Mungu,*+Na mahali pa uharibifu hapajafunikwa.*   Anatandika anga la kaskazini* mahali kwenye hakuna kitu,*+Ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu;   Anafunga maji katika mawingu yake,+Ili mawingu yasipasuke kwa sababu ya uzito wa maji;   Anafunika kiti chake cha ufalme kisionekane,Na anatandika wingu lake juu yake.*+ 10  Anachora mwisho* kwenye uso wa maji;+Anaweka mupaka kati ya mwangaza na giza. 11  Nguzo za mbingu zinatikisika;Na zinashangaa sana kwa sababu ya kukemea kwake. 12  Anavuruga bahari kwa nguvu zake,+Na kwa uelewaji wake anavunja vipande-vipande munyama mukubwa wa bahari.*+ 13  Kwa pumuzi yake* anasafisha anga;Mukono wake unatoboa nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza. 14  Angalia! Hizo ni sehemu za pembeni-pembeni tu za njia zake;+Ni sauti ya chini-chini tu ndiyo tumesikia juu yake! Basi ni nani anaweza kuelewa mungurumo wake wenye nguvu?”+

Maelezo ya Chini

Ao “akili.”
Tnn., “Na ni pumuzi (roho) ya nani yenye imetoka ndani yenu?”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “yeye.”
Ao “Na Abadoni hajafunikwa.”
Tnn., “kaskazini.”
Tnn., “eneo tupu.”
Ni kusema, juu ya kiti chake cha ufalme.
Tnn., “muviringo.”
Tnn., “Rahabu.”
Tnn., “upepo wake.”