Yobu 33:1-33
33 “Lakini sasa, Yobu, tafazali sikia maneno yangu;Sikiliza kila kitu chenye ninasema.
2 Angalia, tafazali! Ninapaswa kufungua kinywa changu;Ulimi wangu unapaswa* kusema.
3 Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+Na midomo yangu inasema kwa uaminifu mambo yenye ninajua.
4 Roho ya Mungu iliniumba,+Na pumuzi ya Mweza-Yote ilinileta kwenye uzima.+
5 Unijibu basi kama unaweza;Toa mawazo yako mbele yangu; ukuwe tayari kujitetea.
6 Angalia! Mimi niko tu kama wewe mbele ya Mungu wa kweli;Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+
7 Kwa hiyo woga wangu usikuogopesheNa mukazo wowote kutoka kwangu usikulemee.
8 Lakini ulisema katika masikio yangu,Ndiyo, niliendelea kusikia maneno haya,
9 ‘Niko safi, sina zambi;+Niko safi, sina kosa.+
10 Lakini Mungu anapata sababu za kunipinga;Ananiona kuwa adui yake.+
11 Anatia miguu yangu katika mikatale;Anachunguza njia zangu zote.’+
12 Lakini unakosea kwa kusema vile, kwa hiyo nitakujibu;Mungu ni mukubwa kuliko mwanadamu mwenye anaweza kufa.+
13 Sababu gani unamulaumu Yeye?+
Je, ni sababu hajajibu maneno yako yote?+
14 Kwa maana Mungu anasema mara moja na mara ya pili,Lakini hakuna mutu mwenye anasikiliza,
15 Katika ndoto, maono ya usiku,+Wakati wanadamu wanashikwa na usingizi muzitoWakati wanalala kwenye vitanda vyao.
16 Kisha anafungua masikio yao+Na anaingiza* maagizo yake ndani yao,
17 Ili kumuepusha mutu asifanye zambi+Na kulinda mwanadamu ili asikuwe na kiburi.+
18 Mungu anaepusha nafsi yake isiingie ndani ya shimo,*+Na uzima wake usiharibiwe kwa upanga.*
19 Mutu anakaripiwa pia kupitia maumivu kwenye kitanda chakeNa kupitia maumivu yenye kuendelea ya mifupa yake,
20 Kwa hiyo nafsi yake inachukia* sana mukate,Na anakataa* hata chakula kizuri.+
21 Nyama ya mwili wake inakonda hata haitambuliwe,Na mifupa yake yenye ilikuwa haionekane inatoka sasa inje.*
22 Nafsi yake inakaribia* shimo;*Uzima wake unakaribia wale wenye kuleta kifo.
23 Kama kuko mujumbe* kwa ajili yake,Muteteaji mumoja kati ya elfu moja (1 000),Ili amuambie mwanadamu mambo yenye kunyooka,
24 Kisha Mungu anamuonyesha wema na kusema,‘Musiache aingie ndani ya shimo!*+
Nimepata bei ya ukombozi!+
25 Mwili wake ukuwe teketeke* kuliko wakati wa ujana;+Akuwe tena na nguvu za siku za ujana wake.’+
26 Atamulilia Mungu,+ mwenye atamukubali,Na ataona uso Wake na kupiga vigelegele vya shangwe,Na Yeye atamurudishia mwanadamu mwenye anaweza kufa haki Yake.
27 Mutu huyo ataambia* watu,‘Nimefanya zambi+ na kupotosha mambo yenye kuwa sawa,Lakini sikupokea kile chenye nilistahili.*
28 Amekomboa nafsi yangu isiingie* ndani ya shimo,*+Na uzima wangu utaona mwangaza.’
29 Kwa kweli, Mungu anafanya mambo yote hayaMara mbili, mara tatu (3), kwa ajili ya mwanadamu,
30 Ili kumutosha* katika shimo,*Kusudi aweze kuangaziwa na mwangaza wa uzima.+
31 Kaza uangalifu, Yobu! Unisikilize!
Nyamaza, na mimi nitaendelea kusema.
32 Kama uko na jambo la kusema, unijibu.
Sema, kwa maana ninataka kukutetea.
33 Kama hauna jambo la kusema, unisikilize;Nyamaza, na mimi nitakufundisha hekima.”
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Ulimi wangu pamoja na kaakaa langu vinapaswa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
^ Tnn., “anatia muhuri juu ya.”
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “kwa silaha.”
^ Ao “nafsi yake inakataa.”
^ Tnn., “uzima wake unachukia.”
^ Ao “inaonekana waziwazi.”
^ Ao “Uzima wake unakaribia.”
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “malaika.”
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “wenye afya ya muzuri zaidi.”
^ Tnn., “ataimbia.”
^ Ao pengine, “Haikuniletea faida.”
^ Ao “uzima wangu usiingie.”
^ Ao “kaburi.”
^ Ao “kutosha nafsi yake.”
^ Ao “kaburi.”