Yobu 33:1-33

  • Elihu anamukaripia Yobu kwa sababu yeye anajiona kuwa mwenye haki (1-33)

    • Bei ya ukombozi inapatikana (24)

    • Kuwa tena na nguvu za wakati wa ujana (25)

33  “Lakini sasa, Yobu, tafazali sikia maneno yangu;Sikiliza kila kitu chenye ninasema.  2  Angalia, tafazali! Ninapaswa kufungua kinywa changu;Ulimi wangu unapaswa* kusema.  3  Maneno yangu yanatangaza unyoofu wa moyo wangu,+Na midomo yangu inasema kwa uaminifu mambo yenye ninajua.  4  Roho ya Mungu iliniumba,+Na pumuzi ya Mweza-Yote ilinileta kwenye uzima.+  5  Unijibu basi kama unaweza;Toa mawazo yako mbele yangu; ukuwe tayari kujitetea.  6  Angalia! Mimi niko tu kama wewe mbele ya Mungu wa kweli;Mimi pia niliumbwa kwa udongo.+  7  Kwa hiyo woga wangu usikuogopesheNa mukazo wowote kutoka kwangu usikulemee.  8  Lakini ulisema katika masikio yangu,Ndiyo, niliendelea kusikia maneno haya,  9  ‘Niko safi, sina zambi;+Niko safi, sina kosa.+ 10  Lakini Mungu anapata sababu za kunipinga;Ananiona kuwa adui yake.+ 11  Anatia miguu yangu katika mikatale;Anachunguza njia zangu zote.’+ 12  Lakini unakosea kwa kusema vile, kwa hiyo nitakujibu;Mungu ni mukubwa kuliko mwanadamu mwenye anaweza kufa.+ 13  Sababu gani unamulaumu Yeye?+ Je, ni sababu hajajibu maneno yako yote?+ 14  Kwa maana Mungu anasema mara moja na mara ya pili,Lakini hakuna mutu mwenye anasikiliza, 15  Katika ndoto, maono ya usiku,+Wakati wanadamu wanashikwa na usingizi muzitoWakati wanalala kwenye vitanda vyao. 16  Kisha anafungua masikio yao+Na anaingiza* maagizo yake ndani yao, 17  Ili kumuepusha mutu asifanye zambi+Na kulinda mwanadamu ili asikuwe na kiburi.+ 18  Mungu anaepusha nafsi yake isiingie ndani ya shimo,*+Na uzima wake usiharibiwe kwa upanga.* 19  Mutu anakaripiwa pia kupitia maumivu kwenye kitanda chakeNa kupitia maumivu yenye kuendelea ya mifupa yake, 20  Kwa hiyo nafsi yake inachukia* sana mukate,Na anakataa* hata chakula kizuri.+ 21  Nyama ya mwili wake inakonda hata haitambuliwe,Na mifupa yake yenye ilikuwa haionekane inatoka sasa inje.* 22  Nafsi yake inakaribia* shimo;*Uzima wake unakaribia wale wenye kuleta kifo. 23  Kama kuko mujumbe* kwa ajili yake,Muteteaji mumoja kati ya elfu moja (1 000),Ili amuambie mwanadamu mambo yenye kunyooka, 24  Kisha Mungu anamuonyesha wema na kusema,‘Musiache aingie ndani ya shimo!*+ Nimepata bei ya ukombozi!+ 25  Mwili wake ukuwe teketeke* kuliko wakati wa ujana;+Akuwe tena na nguvu za siku za ujana wake.’+ 26  Atamulilia Mungu,+ mwenye atamukubali,Na ataona uso Wake na kupiga vigelegele vya shangwe,Na Yeye atamurudishia mwanadamu mwenye anaweza kufa haki Yake. 27  Mutu huyo ataambia* watu,‘Nimefanya zambi+ na kupotosha mambo yenye kuwa sawa,Lakini sikupokea kile chenye nilistahili.* 28  Amekomboa nafsi yangu isiingie* ndani ya shimo,*+Na uzima wangu utaona mwangaza.’ 29  Kwa kweli, Mungu anafanya mambo yote hayaMara mbili, mara tatu (3), kwa ajili ya mwanadamu, 30  Ili kumutosha* katika shimo,*Kusudi aweze kuangaziwa na mwangaza wa uzima.+ 31  Kaza uangalifu, Yobu! Unisikilize! Nyamaza, na mimi nitaendelea kusema. 32  Kama uko na jambo la kusema, unijibu. Sema, kwa maana ninataka kukutetea. 33  Kama hauna jambo la kusema, unisikilize;Nyamaza, na mimi nitakufundisha hekima.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Ulimi wangu pamoja na kaakaa langu vinapaswa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Tnn., “anatia muhuri juu ya.”
Ao “kaburi.”
Ao “kwa silaha.”
Ao “nafsi yake inakataa.”
Tnn., “uzima wake unachukia.”
Ao “inaonekana waziwazi.”
Ao “Uzima wake unakaribia.”
Ao “kaburi.”
Ao “malaika.”
Ao “kaburi.”
Ao “wenye afya ya muzuri zaidi.”
Tnn., “ataimbia.”
Ao pengine, “Haikuniletea faida.”
Ao “uzima wangu usiingie.”
Ao “kaburi.”
Ao “kutosha nafsi yake.”
Ao “kaburi.”