Yobu 28:1-28
28 “Kuko mahali pa kuchimba fezaNa mahali pa zahabu yenye wanasafisha;+
2 Chuma kinatoshwa katika udongo,Na shaba inayeyushwa* kutoka katika miamba.+
3 Mwanadamu anashinda giza;Anachunguza sana ndani ya weusi na giza,Akitafuta jiwe lenye samani.*
4 Anachimba shimo mbali na makao ya watu,Mahali kwenye kumesahauliwa, mbali na mahali kwenye watu wanatembea;Watu fulani wanashuka ndani ya shimo na wanayumba-yumba wakiwa wenye kuninginia.
5 Chakula kinakomaa juu ya udongo;Lakini kule chini, kuko musukosuko kama wa moto.*
6 Katika majiwe hayo kuko yakuti,Na mavumbi yake yako na zahabu.
7 Hakuna ndege mwenye kuwinda mwenye anajua njia ya kuenda kule;Jicho la mwewe mweusi halijaiona.
8 Wanyama wa pori wenye nguvu hawajakanyanga juu yake;Mwana-simba hajatembea kule kwa kuvizia-vizia.
9 Mwanadamu anagonga mwamba mugumu kwa mukono wake;Anapindua milima kwenye misingi yake.
10 Anachimba mifereji ya maji+ ndani ya mwamba;Macho yake yanaona kila kitu chenye samani.
11 Anafunga chemchemi za mitoNa analeta kwenye mwangaza kitu chenye kufichwa.
12 Lakini hekima—inaweza kupatikana wapi,+Na chanzo cha uelewaji kiko wapi?+
13 Hakuna mwanadamu mwenye anajua samani yake,+Na haipatikane katika inchi ya wazima.
14 Maji yenye kuenda chini sana yanasema, ‘Haiko ndani yangu!’
Na bahari inasema, ‘Haiko ndani yangu!’+
15 Haiwezi kununuliwa kwa zahabu safi;Wala feza haiwezi kupimwa kuwa bei yake.+
16 Haiwezi kununuliwa kwa zahabu ya Ofiri+Wala kwa majiwe ya shohamu na yakuti yenye kuwa vigumu kupatikana.
17 Zahabu na kioo haviwezi kulinganishwa nayo;Wala chombo chochote cha zahabu safi* hakiwezi kubadilishwa nayo.+
18 Marijani na fuwele havistahili kutajwa,+Kwa maana mufuko wenye kujaa hekima ni wenye samani kubwa kuliko mufuko wenye kujaa lulu.
19 Topazi+ ya Kushi haiwezi kulinganishwa nayo;Haiwezi kununuliwa hata kwa zahabu safi.
20 Lakini hekima inatoka wapi,Na ni nini chanzo cha uelewaji?+
21 Imefichwa mbali na macho ya kila kiumbe chenye uzima+Na kufichwa mbali na ndege wa mbinguni.
22 Uharibifu na kifo vinasema,‘Masikio yetu yamesikia tu habari zake.’
23 Mungu anaelewa njia ya kuipata;Yeye peke yake ndiye anajua kwenye inakaa,+
24 Kwa maana yeye anaangalia mupaka kwenye miisho ya dunia,Na anaona kila kitu chini ya mbingu.+
25 Wakati aliweka nguvu* ya upepo+Na kupima maji,+
26 Wakati aliweka sheria kwa ajili ya mvua+Na kuweka njia kwa ajili ya wingu la zoruba yenye kunguruma,+
27 Kisha aliona hekima na kuifasiria;Aliisimamisha na kuipima.
28 Na alimuambia mwanadamu:
‘Angalia! Kumuogopa Yehova—ndiyo hekima,+Na kuacha ubaya ni uelewaji.’”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “inamwangwa.”
^ Tnn., “jiwe.”
^ Inaonekana kwamba maneno haya yanahusu uchimbaji wa majiwe yenye samani.
^ Ao “yenye ilisafishwa.”
^ Tnn., “uzito.”