Ufunuo kwa Yohana 15:1-8
15 Na nikaona mbinguni alama ingine, kubwa na ya ajabu, malaika saba (7)+ wenye mapigo saba. Hayo ndiyo ya mwisho, kwa sababu kupitia hayo kasirani ya Mungu inafikia mwisho.+
2 Na nikaona kitu kama bahari ya kioo+ yenye kuchanganywa na moto, na wale wenye wanamushinda+ ule munyama wa pori na sanamu yake+ na ile namba ya jina lake+ walikuwa wamesimama pembeni ya ile bahari ya kioo, wakiwa wameshika vinubi vya Mungu.
3 Walikuwa wanaimba wimbo wa Musa+ mutumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo,+ wakisema:
“Matendo yako ni makubwa na ya ajabu,+ Yehova* Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za haki na za kweli,+ Mufalme wa umilele.+
4 Ni nani mwenye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova,* na kutukuza jina lako, kwa kuwa wewe peke yako ni mushikamanifu?+ Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele yako,+ kwa sababu amri zako za haki zimefunuliwa.”
5 Kisha mambo hayo nikaona, na patakatifu pa hema ya ushahidi+ pakafunguliwa mbinguni,+
6 na wale malaika saba (7) wenye mapigo saba+ wakatokea katika patakatifu, wakiwa wamevaa nguo ya kitani safi, chenye kungaa na wakiwa wamevaa vitambaa vya zahabu kuzunguka vifua vyao.
7 Kimoja cha vile viumbe ine (4) vyenye uzima kikapatia wale malaika saba (7) mabakuli saba ya zahabu yenye kujaa kasirani ya Mungu,+ mwenye anaishi milele na milele.
8 Na patakatifu pakajaa moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu+ na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna mutu yeyote mwenye aliweza kuingia patakatifu mupaka wakati yale mapigo saba (7)+ ya wale malaika saba yalimalizika.