Ufunuo kwa Yohana 15:1-8

  • Malaika saba wenye kuwa na mapigo saba (1-8)

    • Wimbo wa Musa na wa Mwana-Kondoo (3, 4)

15  Na nikaona mbinguni alama ingine, kubwa na ya ajabu, malaika saba (7)+ wenye mapigo saba. Hayo ndiyo ya mwisho, kwa sababu kupitia hayo kasirani ya Mungu inafikia mwisho.+  Na nikaona kitu kama bahari ya kioo+ yenye kuchanganywa na moto, na wale wenye wanamushinda+ ule munyama wa pori na sanamu yake+ na ile namba ya jina lake+ walikuwa wamesimama pembeni ya ile bahari ya kioo, wakiwa wameshika vinubi vya Mungu.  Walikuwa wanaimba wimbo wa Musa+ mutumwa wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo,+ wakisema: “Matendo yako ni makubwa na ya ajabu,+ Yehova* Mungu, Mweza-Yote.+ Njia zako ni za haki na za kweli,+ Mufalme wa umilele.+  Ni nani mwenye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova,* na kutukuza jina lako, kwa kuwa wewe peke yako ni mushikamanifu?+ Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele yako,+ kwa sababu amri zako za haki zimefunuliwa.”  Kisha mambo hayo nikaona, na patakatifu pa hema ya ushahidi+ pakafunguliwa mbinguni,+  na wale malaika saba (7) wenye mapigo saba+ wakatokea katika patakatifu, wakiwa wamevaa nguo ya kitani safi, chenye kungaa na wakiwa wamevaa vitambaa vya zahabu kuzunguka vifua vyao.  Kimoja cha vile viumbe ine (4) vyenye uzima kikapatia wale malaika saba (7) mabakuli saba ya zahabu yenye kujaa kasirani ya Mungu,+ mwenye anaishi milele na milele.  Na patakatifu pakajaa moshi kwa sababu ya utukufu wa Mungu+ na kwa sababu ya nguvu zake, na hakuna mutu yeyote mwenye aliweza kuingia patakatifu mupaka wakati yale mapigo saba (7)+ ya wale malaika saba yalimalizika.

Maelezo ya Chini