Ufunuo kwa Yohana 10:1-11

  • Malaika mwenye nguvu akiwa na kitabu kidogo cha kukunjwa (1-7)

    • “Hakutakuwa tena kukawia” (6)

    • Siri takatifu itafikishwa kwenye mwisho wake (7)

  • Yohana anakula kile kitabu kidogo cha kukunjwa (8-11)

10  Na nikaona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, amepambwa* wingu, na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto,  na katika mukono wake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa chenye kufunguliwa. Na akaweka muguu wake wa kuume juu ya bahari, lakini muguu wake wa kushoto juu ya dunia,  na akalalamika kwa sauti kubwa kama vile wakati simba ananguruma.+ Na wakati alilalamika kwa sauti kubwa, sauti za ile mingurumo saba (7)+ zikasema.  Sasa wakati ile mingurumo saba (7) ilisema, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Tia muhuri mambo yenye ile mingurumo saba ilisema, na usiyaandike.”  Malaika mwenye niliona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mukono wake wa kuume kuelekea mbinguni,  na akaapa kwa Ule mwenye anaishi milele na milele,+ mwenye aliumba mbingu na vitu vyenye kuwa ndani yake na dunia na vitu vyenye kuwa ndani na bahari na vitu vyenye kuwa ndani:+ “Hakutakuwa tena kukawia.  Lakini katika siku zenye ule malaika wa saba (7)+ atakuwa karibu kupiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ yenye Mungu alitangaza kuwa habari njema kwa watumwa wake mwenyewe wenye kuwa manabii+ kwa kweli itafikishwa kwenye mwisho wake.”  Na nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema tena na mimi na kuniambia: “Uende, ukamate kile kitabu cha kukunjwa chenye kufunguliwa chenye kuwa katika mukono wa malaika mwenye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+  Nikaenda kwa ule malaika na kumuambia anipatie kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kikamate na ukikule,+ na kitafanya tumbo lako likuwe na uchungu, lakini katika kinywa chako kitakuwa kitamu kama asali.” 10  Nikakamata kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka katika mukono wa ule malaika na nikakikula,+ na katika kinywa changu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini kisha kukikula, tumbo langu likakuwa na uchungu. 11  Na wakaniambia: “Unapaswa kutoa tena unabii juu ya vikundi vya watu na mataifa na luga na wafalme wengi.”

Maelezo ya Chini

Ao “amefunikwa.”