Ufunuo kwa Yohana 10:1-11

  • Malaika mwenye nguvu akiwa na kitabu kidogo cha kukunjwa (1-7)

    • “Hakutakuwa tena kukawia” (6)

    • Siri takatifu itafikishwa kwenye mwisho wake (7)

  • Yohana anakula kile kitabu kidogo cha kukunjwa (8-11)

10  Na nikaona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, amepambwa* wingu, na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto, 2  na katika mukono wake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa chenye kufunguliwa. Na akaweka muguu wake wa kuume juu ya bahari, lakini muguu wake wa kushoto juu ya dunia, 3  na akalalamika kwa sauti kubwa kama vile wakati simba ananguruma.+ Na wakati alilalamika kwa sauti kubwa, sauti za ile mingurumo saba (7)+ zikasema. 4  Sasa wakati ile mingurumo saba (7) ilisema, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Tia muhuri mambo yenye ile mingurumo saba ilisema, na usiyaandike.” 5  Malaika mwenye niliona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mukono wake wa kuume kuelekea mbinguni, 6  na akaapa kwa Ule mwenye anaishi milele na milele,+ mwenye aliumba mbingu na vitu vyenye kuwa ndani yake na dunia na vitu vyenye kuwa ndani na bahari na vitu vyenye kuwa ndani:+ “Hakutakuwa tena kukawia. 7  Lakini katika siku zenye ule malaika wa saba (7)+ atakuwa karibu kupiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ yenye Mungu alitangaza kuwa habari njema kwa watumwa wake mwenyewe wenye kuwa manabii+ kwa kweli itafikishwa kwenye mwisho wake.” 8  Na nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema tena na mimi na kuniambia: “Uende, ukamate kile kitabu cha kukunjwa chenye kufunguliwa chenye kuwa katika mukono wa malaika mwenye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+ 9  Nikaenda kwa ule malaika na kumuambia anipatie kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Akaniambia: “Kikamate na ukikule,+ na kitafanya tumbo lako likuwe na uchungu, lakini katika kinywa chako kitakuwa kitamu kama asali.” 10  Nikakamata kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka katika mukono wa ule malaika na nikakikula,+ na katika kinywa changu kilikuwa kitamu kama asali,+ lakini kisha kukikula, tumbo langu likakuwa na uchungu. 11  Na wakaniambia: “Unapaswa kutoa tena unabii juu ya vikundi vya watu na mataifa na luga na wafalme wengi.”

Maelezo ya Chini

Ao “amefunikwa.”