Methali 17:1-28

  • Usilipe uovu kwa wema (13)

  • Ondoka kabla ugomvi haujaanza (14)

  • Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote (17)

  • “Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri” (22)

  • Mtu mwenye utambuzi huyazuia maneno yake (27)

17  Ni afadhali kipande kikavu cha mkate mahali penye amani*+Kuliko nyumba iliyojaa karamu* pamoja na ugomvi.+   Mtumishi mwenye ufahamu atamtawala mwana anayetenda kwa aibu;Atapokea urithi kama ndugu za mwana huyo.   Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu,+Lakini Yehova ndiye mchunguzaji wa mioyo.+   Mtu mwovu husikiliza maneno yanayoumiza,Na mtu mdanganyifu husikiliza ulimi unaodhuru.+   Yeyote anayemdhihaki maskini anamtukana Muumba wake,+Na yeyote anayeshangilia msiba wa mwingine hatakosa kuadhibiwa.+   Wajukuu ni taji kwa waliozeeka,Na akina baba* ni utukufu wa wana* wao.   Maneno manyoofu* hayamfai mpumbavu.+ Sembuse maneno ya uwongo kwa mtawala!*+   Zawadi ni kama kito chenye thamani kwa* aliye nayo;+Humletea mafanikio, kila mahali anapoenda.+   Yeyote anayesamehe* kosa hutafuta upendo,+Lakini yule anayeendelea kuongea kuhusu jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.+ 10  Kemeo humgusa moyo zaidi mtu mwenye uelewaji+Kuliko kumpiga mpumbavu mara mia moja.+ 11  Mtu mwovu hutafuta uasi tu,Lakini mjumbe mkatili atatumwa kumwadhibu.+ 12  Ni afadhali kukutana na dubu aliyenyang’anywa watoto wakeKuliko kukutana na mtu mpumbavu katika ujinga wake.+ 13  Mtu yeyote akilipa uovu kwa wema,Uovu hautaondoka katika nyumba yake.+ 14  Kuanzisha vita ni kama kufungua lango la mafuriko;*Kabla ugomvi haujalipuka, ondoka.+ 15  Yeyote anayetangaza kwamba mwovu hana hatia na yeyote anayemshutumu mwadilifu+—Wote wawili wanamchukiza Yehova. 16  Kuna faida gani kwa mpumbavu kuwa na uwezo wa kupata hekimaIlhali hana moyo wa kuipata?*+ 17  Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote+Naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+ 18  Mtu ambaye hana busara* humpa mwingine mkono na kukubaliKuweka dhamana mbele ya jirani yake.+ 19  Mtu anayependa ugomvi anapenda dhambi.+ Yeyote anayeliinua juu lango lake anaalika msiba.+ 20  Mtu aliyepotoka moyoni hatapata mafanikio,*+Na yule anayesema maneno ya udanganyifu ataanguka kwenye maangamizi. 21  Baba anayezaa mtoto mpumbavu atahuzunika;Na baba ya mtoto asiye na akili hana shangwe.+ 22  Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri,*+Lakini roho iliyopondeka humfyonza mtu nguvu.*+ 23  Mtu mwovu atachukua rushwa kwa siri*Ili apotoshe njia ya haki.+ 24  Hekima iko mbele kabisa ya uso wa mtu mwenye utambuzi,Lakini macho ya mpumbavu hutangatanga mpaka kwenye miisho ya dunia.+ 25  Mwana mpumbavu humletea huzuni baba yakeNa kumletea maumivu ya moyo* yule aliyemzaa.+ 26  Si vema kumwadhibu* mwadilifu,Na kuwapiga viboko watu wanaoheshimiwa si jambo linalofaa. 27  Mtu mwenye ujuzi huyazuia maneno yake,+Na mtu mwenye utambuzi atabaki mtulivu.*+ 28  Hata mjinga anayekaa kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,Na yule anayefunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “dhabihu.”
Au “utulivu.”
Au “wazazi.”
Au “watoto.”
Au “kiongozi.”
Au “mazuri.”
Au “ni kito kinachomletea kibali.”
Tnn., “anayefunika.”
Au “kufungulia maji bwawani.” Tnn., “kufungulia maji.”
Au “Ilhali hana busara?”
Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
Tnn., “mema.”
Au “huikausha kabisa mifupa.”
Au “humsaidia mtu kupona.”
Tnn., “rushwa kutoka kifuani.”
Tnn., “Na kumletea uchungu.”
Au “kumtoza faini.”
Tnn., “atabaki na roho iliyotulia.”