Methali 21:1-31
21 Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova.+
Yeye huuelekeza mahali popote anapopenda.+
2 Njia zote za mwanadamu huonekana kuwa sawa machoni pake,+Lakini Yehova huichunguza mioyo.*+
3 Kutenda mambo manyoofu na ya hakiHumpendeza Yehova zaidi kuliko dhabihu.+
4 Macho ya kiburi na moyo wenye majivuno—Taa inayowaongoza waovu ni dhambi.+
5 Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio,*+Lakini wote walio na haraka kwa hakika watakuwa maskini.+
6 Kupata hazina kwa ulimi unaosema uwongoNi kama ukungu unaotoweka, mtego unaoangamiza.*+
7 Ukatili wa waovu utawafagilia mbali,+Kwa maana wanakataa kutenda haki.
8 Njia ya mtu mwenye hatia imepinda,Lakini matendo ya mtu safi yamenyooka.+
9 Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paaKuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+
10 Mtu mwovu hutamani maovu;+Hamtendei kwa fadhili jirani yake.+
11 Mwenye dhihaka anapoadhibiwa, asiye na uzoefu hupata hekima zaidi,Na mtu mwenye hekima anapopata ufahamu, anapata ujuzi.*+
12 Aliye Mwadilifu huichunguza nyumba ya mwovu;Huwapindua waovu na kuwaangamiza.+
13 Yeyote anayeziba sikio lake asisikie kilio cha mtu wa hali ya chiniYeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+
14 Zawadi ya siri hutuliza hasira,+Na rushwa iliyofichwa* hutuliza ghadhabu kali.
15 Mwadilifu hushangilia kutenda haki,+Lakini hilo ni jambo baya sana kwa watenda maovu.
16 Mtu anayetangatanga kutoka kwenye njia ya ufahamuAtapumzika katika kundi la wale waliokufa ambao hawana uwezo.+
17 Anayependa raha* atakuwa maskini;+Anayependa divai na mafuta hatakuwa tajiri.
18 Mwovu ni fidia ya mwadilifu,Na mwenye hila atachukuliwa badala ya mnyoofu.+
19 Ni afadhali kuishi nyikaniKuliko kuishi na mke mgomvi* anayekasirika haraka.+
20 Hazina yenye thamani na mafuta hupatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+Lakini mtu mpumbavu atatumia vibaya* vitu alivyo navyo.+
21 Yeyote anayefuatia uadilifu na upendo mshikamanifuAtapata uzima, uadilifu, na utukufu.+
22 Mtu mwenye hekima anaweza kupanda katika* jiji la watu wenye nguvuNa kudhoofisha nguvu wanazotumaini.+
23 Anayelinda kinywa chake na ulimi wakeAnajiepusha na taabu.+
24 Mtu mwenye kimbelembele, anayejigamba kwa kiburi, hivyo ndivyo unavyomwitaMtu anayetenda kwa kimbelembele bila kujali.+
25 Anachotamani mtu mvivu kitamuua,Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+
26 Anatamani kwa pupa mchana kutwa,Lakini mwadilifu hutoa, hawanyimi wengine chochote.+
27 Dhabihu ya mwovu inachukiza.+
Sembuse anapoitoa akiwa na nia ovu!*
28 Shahidi anayesema uwongo ataangamia,+Lakini mtu anayesikiliza atatoa ushahidi kwa mafanikio.*
29 Mtu mwovu huvaa uso wa ushupavu,+Lakini njia ya mtu mnyoofu ni hakika.*+
30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+
31 Farasi hutayarishwa kwa ajili ya siku ya vita,+Lakini wokovu ni wa Yehova.+
Maelezo ya Chini
^ Au “huzichunguza nia.”
^ Au “manufaa.”
^ Au labda, “kwa wale wanaotafuta kifo.”
^ Au “msumbufu.”
^ Au “anajua la kufanya.”
^ Tnn., “iliyo kifuani.”
^ Au “anasa.”
^ Au “msumbufu.”
^ Tnn., “atavimeza.”
^ Au “kulishinda.”
^ Au “akiwa na mwenendo wa aibu!”
^ Tnn., “atazungumza milele.”
^ Au “mtu mnyoofu huifanya njia yake iwe hakika.”