Methali 9:1-18
9 Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;Imechonga nguzo zake saba.
2 Imetayarisha kabisa nyama yake;*Imechanganya divai yake;Imepanga pia meza yake.
3 Imewatuma vijakazi wakeIli waite kwa sauti kutoka vileleni juu ya jiji:+
4 “Yeyote ambaye ni mjinga, na aje humu.”
Humwambia yule asiye na busara:*
5 “Njoo, ule mkate wanguNa unywe divai niliyochanganya.
6 Acha ujinga wako* uishi;+Tembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”+
7 Anayemrekebisha mtu mwenye dhihaka hualika aibu,+Na yeyote anayemkaripia mtu mwovu ataumia.
8 Usimkaripie mtu mwenye dhihaka, kwa maana atakuchukia.+
Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.+
9 Mfundishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima.+
Mfundishe mwadilifu, naye atazidi kuelimika.
10 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+Na kumjua Aliye Mtakatifu Zaidi+ ni uelewaji.
11 Kwa maana nitafanya siku zako ziwe nyingi,+Na miaka ya maisha yako itaongezwa.
12 Ukipata hekima, unapata hekima kwa faida yako mwenyewe,Lakini ukiwa mwenye dhihaka, utaibeba dhihaka hiyo peke yako.
13 Mwanamke mpumbavu ana kelele.+
Yeye ni mjinga na hajui chochote.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yakeKwenye kiti sehemu zilizoinuka jijini,+
15 Akiwaita kwa sauti wale wanaopita karibu naye,Waendao moja kwa moja kwenye njia yao:
16 “Yeyote ambaye ni mjinga, aje hapa.”
Huwaambia wale wasio na busara:*+
17 “Maji yaliyoibwa ni matamu,Na chakula kinacholiwa sirini kinapendeza.”+
18 Lakini hawajui kwamba wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo,Na kwamba wageni wake wamo katika vina vya Kaburi.*+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Amechinja nyama yake.”
^ Tnn., “aliyepungukiwa moyoni.”
^ Au “Waache wajinga.”
^ Tnn., “waliopungukiwa moyoni.”