Methali 1:1-33

  • Kusudi la methali (1-7)

  • Hatari za marafiki wabaya (8-19)

  • Hekima ya kweli hupaza sauti hadharani (20-33)

1  Methali za Sulemani+ mwana wa Daudi,+ mfalme wa Israeli:+   Ili mtu ajifunze* hekima+ na nidhamu;Ili aelewe maneno ya hekima;   Ili apate nidhamu+ inayoleta ufahamu,Uadilifu,+ busara,*+ na unyoofu;*   Ili kumfanya mjinga awe mwerevu;+Ili kumpa kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.+   Mtu mwenye hekima husikiliza na kujifunza zaidi;+Mtu mwenye uelewaji hupata mwelekezo stadi*+   Ili kuelewa methali na fumbo,*Maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.+   Kumwogopa* Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+ Ni wapumbavu tu wanaodharau hekima na nidhamu.+   Mwanangu, sikiliza nidhamu ya baba yako,+Wala usiyaache mafundisho* ya mama yako.+   Ni shada linalovutia kwenye kichwa chako+Na pambo maridadi shingoni mwako.+ 10  Mwanangu, watenda dhambi wakijaribu kukushawishi, usikubali.+ 11  Wakisema: “Njoo twende. Acha tuvizie ili kumwaga damu. Tutajificha na kuwashambulia bila sababu watu wasio na hatia. 12  Tutawameza wakiwa hai kama Kaburi* linavyomeza,Wazima-wazima, kama wale wanaoshuka shimoni. 13  Na tunyakue mali zao zote zenye thamani;Nyumba zetu tutazijaza nyara. 14  Unapaswa kujiunga nasi,*Nasi sote tutagawana sawasawa vitu tunavyoiba.”* 15  Mwanangu, usiwafuate. Iepushe miguu yako na njia yao.+ 16  Kwa maana miguu yao hukimbilia kutenda uovu;Wanaenda haraka kumwaga damu.+ 17  Kwa kweli ni kazi bure kutandaza wavu huku ndege akitazama. 18  Ndio sababu wanavizia ili kumwaga damu;Wanajificha ili wawaue* wengine. 19  Hizo ndizo njia za wale wanaotafuta faida isiyo ya haki,Ambayo itawaangamiza wale wanaoipata.+ 20  Hekima ya kweli+ hupaza sauti kubwa barabarani.+ Huendelea kuinua sauti yake katika viwanja vya jiji.+ 21  Hupaza sauti kwenye makutano ya barabara zenye watu wengi. Nayo husema hivi kwenye malango ya jiji:+ 22  “Ninyi wajinga mtaendelea kuupenda ujinga mpaka lini? Nanyi wadhihaki mtaendelea kufurahia dhihaka mpaka lini? Nanyi wapumbavu mtaendelea kuchukia ujuzi mpaka lini?+ 23  Sikilizeni karipio langu.*+ Ndipo nitakapowamiminia roho yangu;Nitawajulisha maneno yangu.+ 24  Kwa sababu niliwaita, lakini mkaendelea kukataa,Niliunyoosha mkono wangu, lakini hakuna yeyote aliyejali,+ 25  Mliendelea kupuuza ushauri wangu woteNa kukataa karipio langu, 26  Mimi pia nitawacheka mtakapopatwa na msiba;Nitawadhihaki jambo mnaloogopa litakapokuja,+ 27  Jambo mnaloogopa litakapokuja kama dhoruba,Na msiba wenu utakapofika kama upepo wa dhoruba,Wakati dhiki na taabu zitakapowapata. 28  Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitajibu;Watanitafuta kwa bidii, lakini hawatanipata,+ 29  Kwa sababu walichukia ujuzi,+Nao hawakuchagua kumwogopa Yehova.+ 30  Walikataa ushauri wangu;Waliyadharau makaripio yangu yote. 31  Basi watapata matokeo* ya njia yao,+Nao watashiba kabisa mashauri yao* wenyewe. 32  Kwa maana upotovu wa wajinga utawaua,Na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza. 33  Lakini yule anayenisikiliza ataishi kwa usalama+Naye hatahangaishwa na woga wa msiba.”+

Maelezo ya Chini

Au “ajue.”
Au “jambo lililo la haki.”
Au “kutokuwa na ubaguzi.”
Au “mwongozo wenye hekima.”
Au “mfano.”
Au “Kumheshimu.”
Au “usiiache sheria.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Liweke fungu lako pamoja na letu.”
Au “tutakuwa na mfuko mmoja (kibeti kimoja).”
Au “waangamize nafsi za.”
Au “Geukeni ninapowakaripia.”
Tnn., “watakula matunda.”
Au “njama zao; mipango yao.”