Hesabu 36:1-13

  • Sheria kuhusu kuwaoa warithi wa kike (1-13)

36  Viongozi wa familia za wazao wa Gileadi mwana wa Makiri+ mwana wa Manase wa koo za wana wa Yosefu wakaja kuzungumza na Musa na wakuu, yaani, viongozi wa makabila ya Waisraeli.  Wakawaambia: “Yehova alimwamuru bwana wetu awagawie Waisraeli nchi kwa kura+ ili wairithi; na bwana wetu aliamriwa na Yehova achukue urithi wa Selofehadi ndugu yetu na kuwapa binti zake.+  Lakini wakiolewa na wanaume wa kabila lingine la Waisraeli, urithi wa wanawake hao utaondolewa kutoka katika urithi wa baba zetu na kuongezwa kwenye urithi wa kabila ambamo wataolewa, kwa hiyo urithi huo utaondolewa kutoka katika urithi wetu tuliopokea kwa kura.  Waisraeli wanapofanya Mwadhimisho wa Miaka 50,+ urithi wa wanawake hao utaongezwa kwenye urithi wa kabila walimoolewa, na hivyo urithi wao utaondolewa kutoka katika urithi wa kabila la baba zetu.”  Ndipo Musa akawaamuru hivi Waisraeli kama Yehova alivyoagiza: “Kabila la wana wa Yosefu linasema ukweli.  Yehova ameamuru hivi kuhusu mabinti wa Selofehadi: ‘Wanaweza kuolewa na mtu yeyote wampendaye. Lakini wanapaswa kuolewa na mwanamume anayetoka katika ukoo wa kabila la baba yao.  Hakuna urithi wa Waisraeli unaopaswa kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila lingine, kwa sababu Waisraeli wanapaswa kushikilia urithi wa kabila la mababu zao.  Na kila binti aliye na urithi miongoni mwa makabila ya Waisraeli anapaswa kuolewa na mzao wa kabila la baba yake,+ ili Waisraeli waendelee kumiliki urithi wa mababu zao.  Hakuna urithi unaopaswa kuhamishwa kutoka kabila moja kwenda kabila lingine, kwa sababu makabila ya Waisraeli yanapaswa kushikilia urithi wao.’” 10  Mabinti wa Selofehadi walifanya kama Yehova alivyomwamuru Musa.+ 11  Basi Mala, Tirsa, Hogla, Milka, na Noa, mabinti wa Selofehadi,+ waliolewa na wana wa ndugu za baba yao. 12  Wakawa wake za wanaume kutoka katika koo za Manase mwana wa Yosefu, ili urithi wao ubaki katika kabila la baba yao. 13  Hizo ndizo amri na sheria ambazo* Yehova aliwapa Waisraeli kupitia Musa katika jangwa tambarare la Moabu karibu na Yordani, huko Yeriko.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”