Hesabu 10:1-36

  • Tarumbeta za fedha (1-10)

  • Kuondoka Sinai (11-13)

  • Utaratibu wa kuondoka (14-28)

  • Hobabu aombwa awaongoze Waisraeli (29-34)

  • Sala aliyotoa Musa walipokuwa wakianza safari (35, 36)

10  Kisha Yehova akamwambia Musa:  “Jitengenezee tarumbeta mbili+ za fedha; zitengeneze kwa kutumia nyundo, nawe uzitumie kuwakusanya watu na kuvunja kambi.  Tarumbeta zote mbili zikipigwa, ni lazima Waisraeli wote wakusanyike mbele yako kwenye mlango wa hema la mkutano.+  Tarumbeta moja tu ikipigwa, ni wakuu peke yao watakaokusanyika mbele yako, yaani, viongozi wa maelfu katika Israeli.+  “Mkipiga tarumbeta kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa mashariki+ wanapaswa kuanza safari.  Mkipiga tarumbeta mara ya pili kwa mlio unaobadilika-badilika, wale wanaopiga kambi upande wa kusini+ wanapaswa kuanza safari. Tarumbeta inapaswa kupigwa kwa njia hiyo kila mara kambi moja inapoanza safari.  “Mnapowakusanya watu wote, mnapaswa kuzipiga tarumbeta+ kwa mlio usiobadilika-badilika.  Wana wa Haruni, makuhani, wanapaswa kuzipiga tarumbeta;+ na hiyo itakuwa sheria ya kudumu katika vizazi vyenu vyote.  “Ikiwa maadui wanaowakandamiza watawashambulia katika nchi yenu, mnapaswa kupiga mwito wa vita kwa tarumbeta hizo,+ na Yehova Mungu wenu atawakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu. 10  “Pia, katika siku zenu za kushangilia+—wakati wa sherehe zenu+ na mwanzoni mwa miezi yenu—mtazipiga tarumbeta hizo mnapotoa* dhabihu zenu za kuteketezwa+ na dhabihu zenu za ushirika;+ zitanifanya mimi Mungu wenu niwakumbuke. Mimi ni Yehova Mungu wenu.”+ 11  Basi katika mwaka wa pili, mwezi wa pili, siku ya 20 ya mwezi huo,+ lile wingu liliinuka kutoka juu ya hema+ la Ushahidi. 12  Kwa hiyo Waisraeli wakaanza kuondoka katika nyika ya Sinai kulingana na utaratibu uliowekwa wa kuondoka,+ na wingu hilo likasimama katika nyika ya Parani.+ 13  Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwao kuondoka kama Yehova alivyokuwa amewaagiza kupitia Musa.+ 14  Kwa hiyo kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Yuda liliondoka kwanza kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Nashoni+ mwana wa Aminadabu. 15  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Isakari alikuwa Nethaneli+ mwana wa Zuari. 16  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Zabuloni alikuwa Eliabu+ mwana wa Heloni. 17  Hema la ibada lilipofunguliwa,+ wana wa Gershoni+ na wana wa Merari,+ waliobeba hema hilo, walianza safari. 18  Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya Rubeni liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elisuri+ mwana wa Shedeuri. 19  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Simeoni alikuwa Shelumieli+ mwana wa Zurishadai. 20  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Gadi alikuwa Eliasafu+ mwana wa Deueli. 21  Kisha Wakohathi, waliobeba vyombo vya mahali patakatifu,+ wakaondoka. Hema la ibada lilipaswa kusimamishwa kabla hawajafika. 22  Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Efraimu liliondoka kulingana na vikosi vyake,* na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Elishama+ mwana wa Amihudi. 23  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Manase alikuwa Gamalieli+ mwana wa Pedazuri. 24  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Benjamini alikuwa Abidani+ mwana wa Gidioni. 25  Kisha kundi la makabila matatu katika kambi ya wana wa Dani liliondoka kulingana na vikosi vyake,* nao walikuwa kikosi cha nyuma cha kulinda kambi zote, na kiongozi wa kundi hilo alikuwa Ahiezeri+ mwana wa Amishadai. 26  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Asheri alikuwa Pagieli+ mwana wa Okrani. 27  Kiongozi wa kikosi cha kabila la wana wa Naftali alikuwa Ahira+ mwana wa Enani. 28  Huo ndio utaratibu ambao Waisraeli na vikosi vyao walifuata* kila mara walipoanza safari.+ 29  Kisha Musa akamwambia Hobabu mwana wa Reueli,*+ Mmidiani, baba mkwe wake: “Tunaenda mahali ambapo Yehova alisema, ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’+ Basi twende pamoja,+ nasi tutakutendea mema, kwa sababu Yehova ameahidi kuwapa Waisraeli mambo mema.”+ 30  Lakini akamwambia: “Sitaenda. Nitarudi katika nchi yangu na kwa watu wangu wa ukoo.” 31  Musa akamwambia: “Tafadhali usituache, kwa maana unajua mahali tunapopaswa kupiga kambi nyikani, nawe unaweza kutuonyesha njia.* 32  Ukienda pamoja nasi,+ jambo lolote jema ambalo Yehova atatutendea, bila shaka tutakutendea wewe pia.” 33  Basi wakasafiri kwa siku tatu kutoka kwenye mlima wa Yehova,+ na sanduku+ la agano la Yehova lilisafirishwa mbele yao kwa siku hizo tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.+ 34  Nalo wingu la Yehova+ lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka mahali walipokuwa wamepiga kambi. 35  Kila mara Sanduku hilo lilipoanza kusafirishwa, Musa alisema: “Inuka, Ee Yehova,+ acha maadui wako watawanyike, na wale wanaokuchukia wakimbie kutoka mbele zako.” 36  Na lilipowekwa chini, alisema: “Rudi, Ee Yehova, kwa maelfu yasiyohesabika* ya Waisraeli.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “juu ya.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yake.”
Tnn., “majeshi yao yalifuata.”
Yaani, Yethro.
Tnn., “kuwa macho yetu.”
Au “makumi ya maelfu kwa maelfu.”