Mezali 7:1-27

  • Shika amri za Mungu na uishi (1-5)

  • Kijana mwanaume mujinga anatongozwa (6-27)

    • “Kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa” (22)

7  Mwana wangu, shika maneno yangu,Na uweke amri zangu kama hazina.+  2  Shika amri zangu na uishi;+Linda mafundisho* yangu kama mboni ya jicho lako.  3  Uvifunge kuzunguka vidole vyako;Uviandike kwenye kibao cha moyo wako.+  4  Ambia hekima, “Wewe ni dada yangu,”Na uite uelewaji “mutu wa jamaa yangu,”  5  Ili vikulinde na mwanamuke mwenye kupotoka,*+Na mwanamuke mwasherati* na maneno yake laini.*+  6  Nikiwa kwenye dirisha la nyumba yangu,Niliangalia chini kupitia kayungio ya dirisha langu,  7  Na wakati nilikuwa ninachunguza wajinga,*Nilitambua kati ya vijana, kijana mumoja mwanaume mwenye kukosa akili ya muzuri.*+  8  Alipita katika barabara karibu na makutano ya barabara katika njia yenye kupeleka kwa mwanamuke huyoNa alishika njia ya kuenda kwenye nyumba ya mwanamuke huyo  9  Mangaribi, wakati giza linaanza,+Wakati usiku na giza vinaingia. 10  Kisha nikamuona mwanamuke akikutana naye,Alikuwa amevaa kama* kahaba,+ mwenye moyo mujanja. 11  Ni mwenye makelele na iko* kichwa-nguvu.+ Habakiake* katika nyumba yake. 12  Wakati fulani iko* inje, wakati mwingine iko* katika viwanja vya watu wote,Anajificha karibu na kila makutano ya barabara.+ 13  Kisha anamukamata kwa nguvu kijana huyo na kumupatia busu;Bila haya, mwanamuke huyo anamuambia: 14  “Nilipaswa kutoa zabihu za ushirika.+ Leo nilitimiza naziri zangu. 15  Ndiyo sababu nimekuja kukutana na wewe,Kukutafuta, na nimekupata! 16  Nimetandika matandiko ya muzuri kwenye kitanda changu,Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+ 17  Nimenyunyiza* manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.+ 18  Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui;Na tujifurahishe pamoja kwa mapendo, 19  Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;Ameenda safari ya mbali. 20  Alibeba mufuko wa feza,Na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.” 21  Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.+ Anamutongoza kwa maneno laini. 22  Mara moja kijana huyo anamufuata, kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa,Kama mupumbavu mwenye anaenda kupewa azabu katika mikatale,*+ 23  Mupaka wakati mushale unatoboa maini yake;Kama ndege mwenye anakimbia kuingia katika mutego, hajue kwamba hilo litamufanya apoteze uzima wake.*+ 24  Na sasa, wana wangu, munisikilize;Musikilize kwa uangalifu maneno yenye ninasema. 25  Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake. Musipotee njia na kufuata njia zake,+ 26  Kwa maana amefanya wengi waanguke wakiwa wameuawa,+Na wale wenye ameua ni wengi sana.+ 27  Nyumba yake inaongoza katika Kaburi;*Inashuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.

Maelezo ya Chini

Ao “sheria.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “yenye kushawishi.”
Ao “wenye hawana uzoefu.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “Alikuwa na nguo ya.”
Tnn., “Miguu yake haibakiake.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “pingu.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.