Mezali 7:1-27
7 Mwana wangu, shika maneno yangu,Na uweke amri zangu kama hazina.+
2 Shika amri zangu na uishi;+Linda mafundisho* yangu kama mboni ya jicho lako.
3 Uvifunge kuzunguka vidole vyako;Uviandike kwenye kibao cha moyo wako.+
4 Ambia hekima, “Wewe ni dada yangu,”Na uite uelewaji “mutu wa jamaa yangu,”
5 Ili vikulinde na mwanamuke mwenye kupotoka,*+Na mwanamuke mwasherati* na maneno yake laini.*+
6 Nikiwa kwenye dirisha la nyumba yangu,Niliangalia chini kupitia kayungio ya dirisha langu,
7 Na wakati nilikuwa ninachunguza wajinga,*Nilitambua kati ya vijana, kijana mumoja mwanaume mwenye kukosa akili ya muzuri.*+
8 Alipita katika barabara karibu na makutano ya barabara katika njia yenye kupeleka kwa mwanamuke huyoNa alishika njia ya kuenda kwenye nyumba ya mwanamuke huyo
9 Mangaribi, wakati giza linaanza,+Wakati usiku na giza vinaingia.
10 Kisha nikamuona mwanamuke akikutana naye,Alikuwa amevaa kama* kahaba,+ mwenye moyo mujanja.
11 Ni mwenye makelele na iko* kichwa-nguvu.+
Habakiake* katika nyumba yake.
12 Wakati fulani iko* inje, wakati mwingine iko* katika viwanja vya watu wote,Anajificha karibu na kila makutano ya barabara.+
13 Kisha anamukamata kwa nguvu kijana huyo na kumupatia busu;Bila haya, mwanamuke huyo anamuambia:
14 “Nilipaswa kutoa zabihu za ushirika.+
Leo nilitimiza naziri zangu.
15 Ndiyo sababu nimekuja kukutana na wewe,Kukutafuta, na nimekupata!
16 Nimetandika matandiko ya muzuri kwenye kitanda changu,Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+
17 Nimenyunyiza* manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.+
18 Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui;Na tujifurahishe pamoja kwa mapendo,
19 Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;Ameenda safari ya mbali.
20 Alibeba mufuko wa feza,Na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.”
21 Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.+
Anamutongoza kwa maneno laini.
22 Mara moja kijana huyo anamufuata, kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa,Kama mupumbavu mwenye anaenda kupewa azabu katika mikatale,*+
23 Mupaka wakati mushale unatoboa maini yake;Kama ndege mwenye anakimbia kuingia katika mutego, hajue kwamba hilo litamufanya apoteze uzima wake.*+
24 Na sasa, wana wangu, munisikilize;Musikilize kwa uangalifu maneno yenye ninasema.
25 Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.
Musipotee njia na kufuata njia zake,+
26 Kwa maana amefanya wengi waanguke wakiwa wameuawa,+Na wale wenye ameua ni wengi sana.+
27 Nyumba yake inaongoza katika Kaburi;*Inashuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.
Maelezo ya Chini
^ Ao “sheria.”
^ Ao “yenye kushawishi.”
^ Ao “wenye hawana uzoefu.”
^ Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
^ Ao “Alikuwa na nguo ya.”
^ Tnn., “Miguu yake haibakiake.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
^ Ao “pingu.”
^ Ao “nafsi yake.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

