Mezali 10:1-32
10 Mezali za Sulemani.+
Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+Lakini mwana mupumbavu ni huzuni kwa mama yake.
2 Mali zenye zilipatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,Lakini haki ndiyo inaokoa katika kifo.+
3 Yehova hataacha mwenye haki akae* na njaa,+Lakini ataima waovu mambo yenye wanatamani sana.
4 Mikono yenye uvivu italeta umaskini,+Lakini mikono yenye bidii inaleta utajiri.+
5 Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto,Lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.+
6 Baraka ziko juu ya kichwa cha mwenye haki,+Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.
7 Kumbukumbu la* mwenye haki litabarikiwa,+Lakini jina la muovu litaoza.+
8 Mutu mwenye moyo wa hekima atakubali mafundisho,*+Lakini mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
9 Mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu atatembea kwa usalama,+Lakini mwenye kupotosha njia zake atajulikana.+
10 Mwenye kufinya jicho lake kwa udanganyifu anatokeza huzuni,+Na ule mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima,+Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.+
12 Chuki ndiyo inachochea ugomvi,Lakini upendo unafunika makosa yote.+
13 Hekima inapatikana kwenye midomo ya mutu mwenye utambuzi,+Lakini fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa mutu mwenye hana akili ya muzuri.*+
14 Watu wenye hekima wanaweka ujuzi kama hazina,+Lakini kinywa cha mupumbavu kinaalika uharibifu.+
15 Mali ya* tajiri ni muji wake wenye ngome.
Uharibifu wa maskini ni umaskini wao.+
16 Kazi ya mwenye haki inaongoza kwenye uzima;Lakini mazao ya muovu yanaongoza kwenye zambi.+
17 Mwenye kutii nizamu ni njia yenye inapeleka kwenye uzima,*Lakini mwenye anapuuza karipio anapoteza wengine.
18 Mwenye kuficha chuki yake anasema uongo,+Na mwenye kueneza habari zenye kuumiza* ni mujinga.
19 Wakati maneno ni mengi, kosa haliwezi kuepukwa,+Lakini mutu yeyote mwenye anazuia midomo yake anatenda kwa busara.+
20 Ulimi wa mwenye haki uko kama feza ya muzuri kabisa,+Lakini moyo wa muovu uko na mafaa kidogo.
21 Midomo ya mwenye haki inakulisha* wengi,+Lakini wapumbavu wanakufa kwa sababu ya kukosa akili.+
22 Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri,+Naye haongeze maumivu* yoyote pamoja nayo.
23 Kujiingiza katika mwenendo wa haya ni kama muchezo kwa mujinga,Lakini hekima ni ya mutu mwenye utambuzi.+
24 Kile muovu anaogopa kitamufikia;Lakini tamaa ya mwenye haki itatimizwa.+
25 Wakati zoruba itapita, muovu hatakuwa tena,+Lakini mwenye haki ni musingi milele.+
26 Kama siki* kwenye meno na moshi katika macho,Ni vile mutu muvivu iko* kwa ule mwenye kumutuma.*
27 Kumuogopa Yehova kunarefusha maisha,+Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+
28 Tumaini* la wenye haki linaleta shangwe,+Lakini tumaini la waovu litapotea.+
29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mutu mwenye hana lawama,+Lakini ni uharibifu kwa watenda maovu.+
30 Mwenye haki hataangushwa hata siku moja,+Lakini waovu hawatakaa tena katika dunia.+
31 Kinywa cha mwenye haki kinatokeza* hekima,Lakini ulimi wenye kupotoka utakatwa.
32 Midomo ya mwenye haki inajua mambo yenye kupendeza,Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.
Maelezo ya Chini
^ Ao “nafsi ya mwenye haki ikae.”
^ Ao “Sifa ya.”
^ Tnn., “amri.”
^ Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
^ Ao “Kitu cha maana cha.”
^ Ao pengine, “iko kwenye njia yenye inapeleka kwenye uzima.”
^ Ao “habari zenye haziko hakika.”
^ Ao “inaongoza.”
^ Ao “huzuni; magumu.”
^ Ao “vinaigre.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “bwana wake wa kazi.”
^ Ao “Tarajio.”
^ Ao “kinazaa tunda la.”