Mezali 26:1-28
26 Kama vile teluji* wakati wa kipindi cha joto na mvua wakati wa mavuno,Vilevile heshima haistahili mujinga.+
2 Kama vile ndege iko* na sababu ya kukimbia na mbaruwayu sababu ya kuruka,Vilevile laana haiwezi kuja bila sababu fulani.*
3 Mujeledi ni kwa ajili ya farasi, lijamu* ni kwa ajili ya punda,+Na fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa watu wajinga.+
4 Usijibu mujinga kulingana na upumbavu wake,Ili usikuwe kama yeye.*
5 Jibu mujinga kulingana na upumbavu wake,Ili asifikiri kwamba iko* na hekima.+
6 Kama mutu mwenye anajivunja miguu yake mwenyewe na kujiumiza mwenyewe*Ni vile pia mutu mwenye anatia mambo katika mikono ya mujinga.
7 Kama miguu yenye kuyumba-yumba* ya kilema,Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.+
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,Ni vile pia kumupatia mutu mujinga utukufu.+
9 Kama mumea wa miiba katika mukono wa mulevi,Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.
10 Kama mupiga-mishale mwenye anaumiza ovyo-ovyo,*Ni vile pia mutu mwenye anapatia mujinga ao wapita-njia kazi.
11 Kama vile imbwa anarudilia matapiko yake,Mujinga anarudilia upumbavu wake.+
12 Je, umemuona mutu mwenye anafikiri kama iko* na hekima?+
Kuko tumaini zaidi kwa mujinga kuliko kwa mutu huyo.
13 Muvivu anasema: “Mwana-simba iko* katika barabara,Simba iko* katika kiwanja cha watu wote!”+
14 Mulango unaendelea kuzunguka kwenye bawaba zake,*Na muvivu kwenye kitanda chake.+
15 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,Lakini amechoka sana kuurudisha katika kinywa chake.+
16 Muvivu anafikiri kwamba iko* na hekima zaidiKuliko watu saba (7) wenye wanajibu kwa busara.
17 Kama mutu mwenye kukamata masikio ya imbwaNi vile pia mupita-njia mwenye anakasirishwa* na ugomvi wenye hauko wake.+
18 Kama mwenda-wazimu mwenye anatupa silaha zenye kuwaka moto, mishale, na kifo*
19 Ni vile pia mutu mwenye anamudanganya jirani yake na kusema, “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”+
20 Kwenye hakuna kuni, moto unazimika,Na kwenye hakuna muchongezi, ugomvi unaisha.+
21 Kama vile makaa yanaongezwa kwenye makaa yenye kuwaka na kuni kwenye motoNi vile mutu wa ugomvi anachochea ugomvi.+
22 Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu;*Yanamezwa na kushuka mara moja katika tumbo.+
23 Kama feza yenye kupakwa juu ya chombo cha udongoNi vile pia maneno ya upendo kutoka katika* moyo muovu.+
24 Mwenye anachukia wengine anaficha chuki hiyo kwa midomo yake,Lakini ndani anaweka udanganyifu.
25 Hata kama anasema maneno yenye kupendeza, usimuamini,Kwa maana kuko mambo saba (7) yenye kuchukiza katika moyo wake.*
26 Hata kama chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,Uovu wake utafunuliwa katika kutaniko.
27 Mwenye anachimba shimo ataangukia ndani,Na kila mutu mwenye anaviringisha jiwe—litamurudilia.+
28 Ulimi wenye kusema uongo unachukia watu wenye uliponda,Na kinywa chenye kusifu-sifu kinaleta uharibifu.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “neige.”
^ Ao “eko.”
^ Ao pengine, “Vilevile laana yenye mutu hastahili haimupatake.”
^ Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
^ Ao “Ili usijifanye kuwa kama yeye.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “kunywa jeuri.”
^ Ao “yenye kuninginia.”
^ Ao “mwenye anaumiza kila mutu.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “maegemeo yake.”
^ Ao “eko.”
^ Ao pengine, “mwenye anajiingiza katika.”
^ Ao “mishale yenye kuua.”
^ Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”
^ Tnn., “Midomo yenye shauku pamoja na.”
^ Ao “Kwa maana moyo wake ni wenye kuchukiza kabisa.”