Mezali 26:1-28

  • Maelezo kuhusu watu wavivu (13-16)

  • Usijiingize katika ugomvi wenye haukuangalie (17)

  • Epuka mizaha (18, 19)

  • Kwenye hakuna kuni, moto unazimika (20, 21)

  • Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu (22)

26  Kama vile teluji* wakati wa kipindi cha joto na mvua wakati wa mavuno,Vilevile heshima haistahili mujinga.+   Kama vile ndege iko* na sababu ya kukimbia na mbaruwayu sababu ya kuruka,Vilevile laana haiwezi kuja bila sababu fulani.*   Mujeledi ni kwa ajili ya farasi, lijamu* ni kwa ajili ya punda,+Na fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa watu wajinga.+   Usijibu mujinga kulingana na upumbavu wake,Ili usikuwe kama yeye.*   Jibu mujinga kulingana na upumbavu wake,Ili asifikiri kwamba iko* na hekima.+   Kama mutu mwenye anajivunja miguu yake mwenyewe na kujiumiza mwenyewe*Ni vile pia mutu mwenye anatia mambo katika mikono ya mujinga.   Kama miguu yenye kuyumba-yumba* ya kilema,Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.+   Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,Ni vile pia kumupatia mutu mujinga utukufu.+   Kama mumea wa miiba katika mukono wa mulevi,Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga. 10  Kama mupiga-mishale mwenye anaumiza ovyo-ovyo,*Ni vile pia mutu mwenye anapatia mujinga ao wapita-njia kazi. 11  Kama vile imbwa anarudilia matapiko yake,Mujinga anarudilia upumbavu wake.+ 12  Je, umemuona mutu mwenye anafikiri kama iko* na hekima?+ Kuko tumaini zaidi kwa mujinga kuliko kwa mutu huyo. 13  Muvivu anasema: “Mwana-simba iko* katika barabara,Simba iko* katika kiwanja cha watu wote!”+ 14  Mulango unaendelea kuzunguka kwenye bawaba zake,*Na muvivu kwenye kitanda chake.+ 15  Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,Lakini amechoka sana kuurudisha katika kinywa chake.+ 16  Muvivu anafikiri kwamba iko* na hekima zaidiKuliko watu saba (7) wenye wanajibu kwa busara. 17  Kama mutu mwenye kukamata masikio ya imbwaNi vile pia mupita-njia mwenye anakasirishwa* na ugomvi wenye hauko wake.+ 18  Kama mwenda-wazimu mwenye anatupa silaha zenye kuwaka moto, mishale, na kifo* 19  Ni vile pia mutu mwenye anamudanganya jirani yake na kusema, “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”+ 20  Kwenye hakuna kuni, moto unazimika,Na kwenye hakuna muchongezi, ugomvi unaisha.+ 21  Kama vile makaa yanaongezwa kwenye makaa yenye kuwaka na kuni kwenye motoNi vile mutu wa ugomvi anachochea ugomvi.+ 22  Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu;*Yanamezwa na kushuka mara moja katika tumbo.+ 23  Kama feza yenye kupakwa juu ya chombo cha udongoNi vile pia maneno ya upendo kutoka katika* moyo muovu.+ 24  Mwenye anachukia wengine anaficha chuki hiyo kwa midomo yake,Lakini ndani anaweka udanganyifu. 25  Hata kama anasema maneno yenye kupendeza, usimuamini,Kwa maana kuko mambo saba (7) yenye kuchukiza katika moyo wake.* 26  Hata kama chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,Uovu wake utafunuliwa katika kutaniko. 27  Mwenye anachimba shimo ataangukia ndani,Na kila mutu mwenye anaviringisha jiwe—litamurudilia.+ 28  Ulimi wenye kusema uongo unachukia watu wenye uliponda,Na kinywa chenye kusifu-sifu kinaleta uharibifu.+

Maelezo ya Chini

Ao “neige.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “Vilevile laana yenye mutu hastahili haimupatake.”
Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
Ao “Ili usijifanye kuwa kama yeye.”
Ao “eko.”
Tnn., “kunywa jeuri.”
Ao “yenye kuninginia.”
Ao “mwenye anaumiza kila mutu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “maegemeo yake.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “mwenye anajiingiza katika.”
Ao “mishale yenye kuua.”
Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”
Tnn., “Midomo yenye shauku pamoja na.”
Ao “Kwa maana moyo wake ni wenye kuchukiza kabisa.”