Mezali 5:1-23
5 Mwana wangu, sikiliza hekima yangu.
Sikiliza kwa uangalifu* utambuzi wangu,+
2 Ili uweze kulinda uwezo wako wa kufikiriNa kulinda ujuzi kwa midomo yako.+
3 Kwa maana midomo ya mwanamuke mwenye kupotoka* inaangusha matone-matone kama sega la asali,+Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+
4 Lakini mwishowe ni muchungu kama pakanga+Na mwenye makali kama upanga wenye kukata pande zote mbili.+
5 Miguu yake inashuka kwenye kifo.
Hatua zake zinaongoza moja kwa moja katika Kaburi.*
6 Hafikiriake njia ya uzima.
Njia yake inaenda huku na huku, lakini hajue kwenye inaelekea.
7 Sasa, wana wangu, munisikilizeNa musiache mambo yenye ninasema.
8 Mukae mbali naye;Musikaribie muingilio wa nyumba yake,+
9 Ili musipatie wengine heshima yenu+Wala kuvuna miaka ya ukali;+
10 Ili wageni wasimalize mali* zenu+Na ili vitu vyenye mulifanyia kazi ya jasho visiende katika nyumba ya mugeni.
11 Mukifanya vile, mutalia kwa maumivu kwenye mwisho wa maisha yenuWakati nyama yenu na mwili wenu vitakuwa zaifu+
12 Na utasema: “Nilichukia sana nizamu!
Moyo wangu ulizarau sana karipio!
13 Sikusikiliza sauti ya wafundishaji wanguWala kusikiliza kwa uangalifu walimu wangu.
14 Nilikuwa karibu kuangamia kabisaKatikati ya kutaniko lote.”*+
15 Kunywa maji ya tangi lako mwenyeweNa maji yenye kutiririka* ya kisima chako mwenyewe.+
16 Je, chemchemi zako zisambae inje,Na mito yako midogo ya maji katika viwanja vya watu wote?+
17 Yakuwe yako peke yako,Na yasikuwe ya wageni pamoja na wewe.+
18 Chemchemi yako ibarikiwe,*Na ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako,+
19 Paa-dike mwenye kupendeza, mbuzi wa milima* mwenye kuvutia.+
Maziwa yake yakushibishe* nyakati zote.
Upendo wake ukuvutie sana kila wakati.+
20 Basi mwana wangu, sababu gani uvutiwe sana na mwanamuke mwenye kupotoka*Ao kukumbatia kifua cha mwanamuke mwasherati?*+
21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;Anachunguza njia zake zote.+
22 Muovu ananaswa na makosa yake mwenyewe,Na atashikwa katika kamba za zambi yake mwenyewe.+
23 Atakufa kwa sababu ya kukosa nizamuNa kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake wenye kupita kiasi.
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Tegea sikio lako.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “nguvu.”
^ Tnn., “Katikati ya mukusanyiko na kutaniko.”
^ Ao “safi.”
^ Ao “Chanzo chako cha maji kibarikiwe.”
^ Ao “mbuzi wa pori.”
^ Ao “yakuleweshe.”