Mezali 5:1-23

  • Onyo juu ya wanamuke waasherati (1-14)

  • Furahi pamoja na bibi yako (15-23)

5  Mwana wangu, sikiliza hekima yangu. Sikiliza kwa uangalifu* utambuzi wangu,+   Ili uweze kulinda uwezo wako wa kufikiriNa kulinda ujuzi kwa midomo yako.+   Kwa maana midomo ya mwanamuke mwenye kupotoka* inaangusha matone-matone kama sega la asali,+Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+   Lakini mwishowe ni muchungu kama pakanga+Na mwenye makali kama upanga wenye kukata pande zote mbili.+   Miguu yake inashuka kwenye kifo. Hatua zake zinaongoza moja kwa moja katika Kaburi.*   Hafikiriake njia ya uzima. Njia yake inaenda huku na huku, lakini hajue kwenye inaelekea.   Sasa, wana wangu, munisikilizeNa musiache mambo yenye ninasema.   Mukae mbali naye;Musikaribie muingilio wa nyumba yake,+   Ili musipatie wengine heshima yenu+Wala kuvuna miaka ya ukali;+ 10  Ili wageni wasimalize mali* zenu+Na ili vitu vyenye mulifanyia kazi ya jasho visiende katika nyumba ya mugeni. 11  Mukifanya vile, mutalia kwa maumivu kwenye mwisho wa maisha yenuWakati nyama yenu na mwili wenu vitakuwa zaifu+ 12  Na utasema: “Nilichukia sana nizamu! Moyo wangu ulizarau sana karipio! 13  Sikusikiliza sauti ya wafundishaji wanguWala kusikiliza kwa uangalifu walimu wangu. 14  Nilikuwa karibu kuangamia kabisaKatikati ya kutaniko lote.”*+ 15  Kunywa maji ya tangi lako mwenyeweNa maji yenye kutiririka* ya kisima chako mwenyewe.+ 16  Je, chemchemi zako zisambae inje,Na mito yako midogo ya maji katika viwanja vya watu wote?+ 17  Yakuwe yako peke yako,Na yasikuwe ya wageni pamoja na wewe.+ 18  Chemchemi yako ibarikiwe,*Na ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako,+ 19  Paa-dike mwenye kupendeza, mbuzi wa milima* mwenye kuvutia.+ Maziwa yake yakushibishe* nyakati zote. Upendo wake ukuvutie sana kila wakati.+ 20  Basi mwana wangu, sababu gani uvutiwe sana na mwanamuke mwenye kupotoka*Ao kukumbatia kifua cha mwanamuke mwasherati?*+ 21  Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;Anachunguza njia zake zote.+ 22  Muovu ananaswa na makosa yake mwenyewe,Na atashikwa katika kamba za zambi yake mwenyewe.+ 23  Atakufa kwa sababu ya kukosa nizamuNa kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake wenye kupita kiasi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Tegea sikio lako.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nguvu.”
Tnn., “Katikati ya mukusanyiko na kutaniko.”
Ao “safi.”
Ao “Chanzo chako cha maji kibarikiwe.”
Ao “mbuzi wa pori.”
Ao “yakuleweshe.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.