Mezali 19:1-29

  • Ufahamu unatuliza kasirani (11)

  • Bibi mugomvi ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye kuvuya (13)

  • Bibi mwenye busara anatoka kwa Yehova (14)

  • Tia mutoto nizamu wakati kungali tumaini (18)

  • Hekima ya kusikiliza shauri (20)

19  Ni muzuri zaidi kuwa maskini na kutembea katika uaminifu-mushikamanifu+Kuliko kuwa mujinga na kusema uongo.+   Mutu mwenye hana ujuzi haiko mutu muzuri,*+Na mutu mwenye kutenda bila kufikiri* anatenda zambi.   Upumbavu wa mutu ndio unapotosha njia yake,Na moyo wake unamukasirikia sana Yehova.   Mali inavuta marafiki wengi,Lakini hata rafiki ya maskini atamuacha.+   Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,+Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua hataponyoka.+   Wengi wanatafuta kukubaliwa na mutu mwenye cheo,*Na kila mutu ni rafiki ya mutu mwenye kutoa zawadi.   Ndugu wote wa mutu maskini wanamuchukia;+Marafiki wake wanamuepuka hata zaidi!+ Anawafuatilia ili awaombe mambo fulani, lakini hakuna mwenye anamusikiliza.   Kila mutu mwenye anapata akili ya muzuri* anajipenda mwenyewe.*+ Kila mutu mwenye anapendezwa sana na utambuzi atapata mafanikio.*+   Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua ataangamia.+ 10  Mupumbavu hastahili kuishi maisha ya raha;Namna gani mutumishi kutawala wakubwa!+ 11  Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake,+Na ni uzuri kwake kuachilia* kosa.+ 12  Kasirani kali ya mufalme ni kama mungurumo wa simba,*+Lakini kukubaliwa naye ni kama umande juu ya majani. 13  Mwana mujinga anamuletea baba yake shida,+Na bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye haiache kuvuya hata kidogo.+ 14  Nyumba na mali vinaritiwa kutoka kwa baba,Lakini bibi mwenye busara anatoka kwa Yehova.+ 15  Uvivu unaleta usingizi muzito,Na mutu muregevu atakuwa na njaa.+ 16  Mwenye anashika amri analinda uzima wake;*+Mwenye hahangaikie njia zake atakufa.+ 17  Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova,+Na Yeye atamulipa* kwa sababu ya mambo yenye anatenda.+ 18  Patia mwana wako nizamu wakati kungali tumaini,+Na usimufanye* akufe.+ 19  Mutu mwenye kukasirika-kasirika atalipia kosa lake;Ukijaribu kumuokoa, utalazimika kufanya vile tena na tena.+ 20  Sikiliza shauri na ukubali nizamu,+Ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.+ 21  Moyo wa mwanadamu uko na mipango mingi,Lakini shauri* la Yehova ndilo litadumu.+ 22  Kitu chenye kutamanika ndani ya mutu ni upendo wake mushikamanifu;+Na ni muzuri zaidi kuwa maskini kuliko kuwa muongo. 23  Kumuogopa Yehova kunaongoza kwenye uzima;+Ule mwenye kuwa na woga huo atapumuzika muzuri, hatapatwa na mambo yenye kuumiza.+ 24  Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,Lakini hajikaze hata kuurudisha katika kinywa chake.+ 25  Piga mwenye zihaka,+ ili mwenye hana uzoefu akuwe mwerevu,+Karipia mwenye uelewaji, ili aongeze ujuzi wake.+ 26  Mwenye anatendea baba yake mubaya na kufukuza mama yakeNi mwana mwenye kuleta haya na aibu.+ 27  Mwana wangu, ukiacha kusikiliza nizamu,Utakengeuka na kuacha maneno ya ujuzi. 28  Shahidi mwenye hana mafaa yoyote anachekelea haki,+Na kinywa cha waovu kinameza-meza uovu.+ 29  Hukumu inangojea wenye zihaka,+Na mugongo wa wajinga unangojea kupigwa.+

Maelezo ya Chini

Ao “Nafsi yenye haina ujuzi haiko nafsi ya muzuri.”
Tnn., “mwenye anaenda haraka kwa miguu yake.”
Ao “mutu mukarimu.”
Ao “anapenda nafsi yake.”
Tnn., “mema.”
Tnn., “anapata moyo.”
Tnn., “kupita juu ya.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “musumbufu.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “atamupatia zawabu.”
Ao “usitamani.” Tnn., “usiinue nafsi yako ili.”
Ao “kusudi.”