Mezali 19:1-29
19 Ni muzuri zaidi kuwa maskini na kutembea katika uaminifu-mushikamanifu+Kuliko kuwa mujinga na kusema uongo.+
2 Mutu mwenye hana ujuzi haiko mutu muzuri,*+Na mutu mwenye kutenda bila kufikiri* anatenda zambi.
3 Upumbavu wa mutu ndio unapotosha njia yake,Na moyo wake unamukasirikia sana Yehova.
4 Mali inavuta marafiki wengi,Lakini hata rafiki ya maskini atamuacha.+
5 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,+Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua hataponyoka.+
6 Wengi wanatafuta kukubaliwa na mutu mwenye cheo,*Na kila mutu ni rafiki ya mutu mwenye kutoa zawadi.
7 Ndugu wote wa mutu maskini wanamuchukia;+Marafiki wake wanamuepuka hata zaidi!+
Anawafuatilia ili awaombe mambo fulani, lakini hakuna mwenye anamusikiliza.
8 Kila mutu mwenye anapata akili ya muzuri* anajipenda mwenyewe.*+
Kila mutu mwenye anapendezwa sana na utambuzi atapata mafanikio.*+
9 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua ataangamia.+
10 Mupumbavu hastahili kuishi maisha ya raha;Namna gani mutumishi kutawala wakubwa!+
11 Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake,+Na ni uzuri kwake kuachilia* kosa.+
12 Kasirani kali ya mufalme ni kama mungurumo wa simba,*+Lakini kukubaliwa naye ni kama umande juu ya majani.
13 Mwana mujinga anamuletea baba yake shida,+Na bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye haiache kuvuya hata kidogo.+
14 Nyumba na mali vinaritiwa kutoka kwa baba,Lakini bibi mwenye busara anatoka kwa Yehova.+
15 Uvivu unaleta usingizi muzito,Na mutu muregevu atakuwa na njaa.+
16 Mwenye anashika amri analinda uzima wake;*+Mwenye hahangaikie njia zake atakufa.+
17 Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova,+Na Yeye atamulipa* kwa sababu ya mambo yenye anatenda.+
18 Patia mwana wako nizamu wakati kungali tumaini,+Na usimufanye* akufe.+
19 Mutu mwenye kukasirika-kasirika atalipia kosa lake;Ukijaribu kumuokoa, utalazimika kufanya vile tena na tena.+
20 Sikiliza shauri na ukubali nizamu,+Ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.+
21 Moyo wa mwanadamu uko na mipango mingi,Lakini shauri* la Yehova ndilo litadumu.+
22 Kitu chenye kutamanika ndani ya mutu ni upendo wake mushikamanifu;+Na ni muzuri zaidi kuwa maskini kuliko kuwa muongo.
23 Kumuogopa Yehova kunaongoza kwenye uzima;+Ule mwenye kuwa na woga huo atapumuzika muzuri, hatapatwa na mambo yenye kuumiza.+
24 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,Lakini hajikaze hata kuurudisha katika kinywa chake.+
25 Piga mwenye zihaka,+ ili mwenye hana uzoefu akuwe mwerevu,+Karipia mwenye uelewaji, ili aongeze ujuzi wake.+
26 Mwenye anatendea baba yake mubaya na kufukuza mama yakeNi mwana mwenye kuleta haya na aibu.+
27 Mwana wangu, ukiacha kusikiliza nizamu,Utakengeuka na kuacha maneno ya ujuzi.
28 Shahidi mwenye hana mafaa yoyote anachekelea haki,+Na kinywa cha waovu kinameza-meza uovu.+
29 Hukumu inangojea wenye zihaka,+Na mugongo wa wajinga unangojea kupigwa.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Nafsi yenye haina ujuzi haiko nafsi ya muzuri.”
^ Tnn., “mwenye anaenda haraka kwa miguu yake.”
^ Ao “mutu mukarimu.”
^ Ao “anapenda nafsi yake.”
^ Tnn., “mema.”
^ Tnn., “anapata moyo.”
^ Tnn., “kupita juu ya.”
^ Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
^ Ao “musumbufu.”
^ Ao “nafsi yake.”
^ Ao “atamupatia zawabu.”
^ Ao “usitamani.” Tnn., “usiinue nafsi yako ili.”
^ Ao “kusudi.”