Mezali 27:1-27
27 Usijisifu juu ya kesho,Kwa maana haujue siku italeta nini.*+
2 Acha mutu mwingine* akusifu, hapana kinywa chako mwenyewe;Wengine,* hapana midomo yako mwenyewe.+
3 Jiwe ni nzito na muchanga ni muzito,Lakini usumbufu wenye unaletwa na mupumbavu ni muzito zaidi kuliko vyote viwili.+
4 Kuko ukali wa hasira na mafuriko ya kasirani kali,Lakini ni nani anaweza kuvumilia wivu?+
5 Karipio lenye kuwa wazi ni muzuri zaidi kuliko upendo wenye kufichwa.+
6 Vidonda vyenye kutokezwa na rafiki ni vya uaminifu,+Lakini busu za adui ni nyingi.*
7 Mwenye hamu yake ya kula imetoshelezwa anazarau* asali ya sega,Lakini kwa mwenye njaa, hata kitu kichungu ni kitamu.
8 Kama ndege mwenye anaenda* mbali na chicha yake*Ni vile pia mutu mwenye anaenda mbali na nyumba yake.
9 Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo;Ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.*+
10 Usimuache rafiki yako ao rafiki ya baba yako,Na usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku yenye uko na musiba;Jirani wa karibu anashindia ndugu wa mbali.+
11 Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu,+Ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.+
12 Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,+Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.*
13 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+
14 Wakati mutu anabariki jirani yake kwa sauti kubwa asubui sana,Itaonwa kuwa laana kwake.
15 Bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye inavuya bila kuacha katika siku ya mvua.+
16 Kila mutu mwenye anaweza kumuzuia anaweza kuzuia upepoNa anaweza kukamata mafuta kwa mukono wake wa kuume.
17 Kama vile chuma kinanoa chuma,Ni vile pia mutu ananoa rafiki* yake.+
18 Mwenye anatunza muti wa tini atakula matunda yake,+Na mwenye anatunza bwana wake ataheshimiwa.+
19 Kama vile maji yanaonyesha uso wa mutu,Ni vile pia moyo wa mutu unaonyesha moyo wa mwingine.
20 Kaburi na mahali pa uharibifu* havitosheke hata kidogo,+Wala macho ya mwanadamu hayatosheke hata kidogo.
21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+Vilevile mutu anapimwa kupitia sifa yenye anapokea.*
22 Hata kama unatwanga mupumbavu kwa mutwangioKama vile nafaka yenye kupondwa katika kinu,Upumbavu wake hautamutoka.
23 Unapaswa kujua muzuri hali ya kundi lako.
Tunza muzuri* kondoo wako,+
24 Kwa maana mali haidumu milele,+Wala taji halidumu vizazi vyote.
25 Majani ya mubichi yanaisha, na majani ya mupya yanatokea,Na majani ya milima yanakusanywa.
26 Wana-kondoo dume wanakupatia nguo zako,Na mbuzi-dume wanakupatia bei ya shamba.
27 Na kutakuwa maziwa ya kutosha ya mbuzi ya kukulisha wewe,Kukulisha familia yako, na kutegemeza watumishi wako wanamuke.
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “itazaa nini.”
^ Tnn., “mugeni.”
^ Tnn., “Mugeni.”
^ Ao pengine, “haziko za kweli; ni za kulazimishwa.”
^ Ao “Nafsi yenye kutosheka inazarau.” Tnn., “anakanyangia chini.”
^ Ao “mwenye anakimbia.”
^ Ao “nyumba yake; kiota chake.”
^ Ao “shauri la nafsi.”
^ Ao “azabu.”
^ Ao “mugeni.”
^ Ao “musumbufu.”
^ Tnn., “uso wa rafiki.”
^ Ao “Sheoli na Abadoni.”
^ Ao “Vilevile mutu ni kulingana na sifa yake.”
^ Ao “Weka moyo juu ya; Kazia uangalifu.”