Mezali 27:1-27

  • Karipio kutoka kwa rafiki ni lenye faida (5, 6)

  • Mwana wangu, furahisha moyo wangu (11)

  • Chuma kinanoa chuma (17)

  • Jua kundi lako (23)

  • Mali haidumu milele (24)

27  Usijisifu juu ya kesho,Kwa maana haujue siku italeta nini.*+  2  Acha mutu mwingine* akusifu, hapana kinywa chako mwenyewe;Wengine,* hapana midomo yako mwenyewe.+  3  Jiwe ni nzito na muchanga ni muzito,Lakini usumbufu wenye unaletwa na mupumbavu ni muzito zaidi kuliko vyote viwili.+  4  Kuko ukali wa hasira na mafuriko ya kasirani kali,Lakini ni nani anaweza kuvumilia wivu?+  5  Karipio lenye kuwa wazi ni muzuri zaidi kuliko upendo wenye kufichwa.+  6  Vidonda vyenye kutokezwa na rafiki ni vya uaminifu,+Lakini busu za adui ni nyingi.*  7  Mwenye hamu yake ya kula imetoshelezwa anazarau* asali ya sega,Lakini kwa mwenye njaa, hata kitu kichungu ni kitamu.  8  Kama ndege mwenye anaenda* mbali na chicha yake*Ni vile pia mutu mwenye anaenda mbali na nyumba yake.  9  Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo;Ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.*+ 10  Usimuache rafiki yako ao rafiki ya baba yako,Na usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku yenye uko na musiba;Jirani wa karibu anashindia ndugu wa mbali.+ 11  Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu,+Ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.+ 12  Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,+Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.* 13  Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+ 14  Wakati mutu anabariki jirani yake kwa sauti kubwa asubui sana,Itaonwa kuwa laana kwake. 15  Bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye inavuya bila kuacha katika siku ya mvua.+ 16  Kila mutu mwenye anaweza kumuzuia anaweza kuzuia upepoNa anaweza kukamata mafuta kwa mukono wake wa kuume. 17  Kama vile chuma kinanoa chuma,Ni vile pia mutu ananoa rafiki* yake.+ 18  Mwenye anatunza muti wa tini atakula matunda yake,+Na mwenye anatunza bwana wake ataheshimiwa.+ 19  Kama vile maji yanaonyesha uso wa mutu,Ni vile pia moyo wa mutu unaonyesha moyo wa mwingine. 20  Kaburi na mahali pa uharibifu* havitosheke hata kidogo,+Wala macho ya mwanadamu hayatosheke hata kidogo. 21  Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+Vilevile mutu anapimwa kupitia sifa yenye anapokea.* 22  Hata kama unatwanga mupumbavu kwa mutwangioKama vile nafaka yenye kupondwa katika kinu,Upumbavu wake hautamutoka. 23  Unapaswa kujua muzuri hali ya kundi lako. Tunza muzuri* kondoo wako,+ 24  Kwa maana mali haidumu milele,+Wala taji halidumu vizazi vyote. 25  Majani ya mubichi yanaisha, na majani ya mupya yanatokea,Na majani ya milima yanakusanywa. 26  Wana-kondoo dume wanakupatia nguo zako,Na mbuzi-dume wanakupatia bei ya shamba. 27  Na kutakuwa maziwa ya kutosha ya mbuzi ya kukulisha wewe,Kukulisha familia yako, na kutegemeza watumishi wako wanamuke.

Maelezo ya Chini

Tnn., “itazaa nini.”
Tnn., “mugeni.”
Tnn., “Mugeni.”
Ao pengine, “haziko za kweli; ni za kulazimishwa.”
Ao “Nafsi yenye kutosheka inazarau.” Tnn., “anakanyangia chini.”
Ao “mwenye anakimbia.”
Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ao “shauri la nafsi.”
Ao “azabu.”
Ao “mugeni.”
Ao “musumbufu.”
Tnn., “uso wa rafiki.”
Ao “Sheoli na Abadoni.”
Ao “Vilevile mutu ni kulingana na sifa yake.”
Ao “Weka moyo juu ya; Kazia uangalifu.”