Cha Kwanza cha Samweli 31:1-13

  • Kifo cha Sauli na wana wake watatu (1-13)

31  Sasa Wafilisti walikuwa wanapigana na Israeli.+ Na watu wa Israeli wakakimbia kutoka mbele ya Wafilisti, na wengi wakaanguka wakiwa wameuawa kwenye Mulima Gilboa.+ 2  Wafilisti wakamukaribia sana Sauli na wana wake, na wakamupiga na kumuua Yonatani,+ Abinadabu, na Malki-shua, wana wa Sauli.+ 3  Pigano likakuwa kali sana juu ya Sauli, na wapiga-mishale wakamupata, na wapiga-mishale hao wakamuumiza sana.+ 4  Kisha Sauli akamuambia mubeba-silaha wake: “Chomoa upanga wako na unitoboe nao, ili watu hawa wenye hawatahiriwe+ wasikuje na kunitoboa na kunitendea bila huruma.”* Lakini mubeba-silaha wake hakutaka, kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akakamata upanga na kuuangukia.+ 5  Wakati mubeba-silaha wake aliona kwamba Sauli amekufa,+ yeye pia akaangukia upanga wake mwenyewe na akakufa pamoja naye. 6  Basi Sauli, wana wake watatu (3), mubeba-silaha wake, na watu wake wote wakakufa pamoja siku hiyo.+ 7  Wakati watu wa Israeli wenye walikuwa katika eneo la bonde* na katika eneo la Yordani waliona kwamba watu wa Israeli walikuwa wamekimbia na kwamba Sauli na wana wake wamekufa, wakaanza kuacha miji na kukimbia;+ kisha Wafilisti wakakuja na kukaa ndani. 8  Siku yenye ilifuata, wakati Wafilisti walikuja kuondoa vitu kwenye miili ya watu wenye waliuawa, walimukuta Sauli na wana wake watatu (3) wakiwa wameanguka kwenye Mulima Gilboa.+ 9  Basi wakamukata kichwa na kuvua silaha zake na kutuma ujumbe katika inchi yote ya Wafilisti ili kueneza habari+ katika nyumba* za sanamu zao+ na kati ya watu. 10  Kisha wakatia silaha zake katika nyumba ya sanamu za Ashtoreti na wakafungia maiti yake kwenye ukuta wa Bet-shani.+ 11  Wakati wakaaji wa Yabeshi-gileadi+ walisikia mambo yenye Wafilisti walikuwa wamemutendea Sauli, 12  wapiganaji-vita wote wakasimama na kusafiri usiku wote na kuondoa miili ya Sauli na wana wake kwenye ukuta wa Bet-shani. Wakarudia Yabeshi na kuiteketeza kwa moto kule. 13  Kisha wakakamata mifupa yao+ na kuizika chini ya muti wa mukwaju katika Yabeshi,+ na wakafunga kwa siku saba (7).

Maelezo ya Chini

Ao “mubaya.”
Ao “eneo tambarare la chini.”
Ao “mahekalu.”