Cha Kwanza cha Samweli 24:1-22

  • Daudi hamuue Sauli (1-22)

    • Daudi anamuheshimia mutiwa-mafuta wa Yehova (6)

24  Wakati tu Sauli alirudia kisha kufuatilia Wafilisti, walimuambia: “Angalia! Daudi iko* katika jangwa la En-gedi.”+  Kwa hiyo Sauli akachukua wanaume elfu tatu (3 000) wenye walichaguliwa katika Israeli yote na akaenda kumutafuta Daudi na watu wake kwenye miteremuko mikali yenye miamba ya mbuzi wa milima.  Sauli akafika kwenye mazizi* ya majiwe ya kondoo pembeni ya barabara, mahali kwenye kulikuwa pango, na akaingia ndani ili ajisaidie,* wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa katika sehemu za ndani kabisa nyuma ya pango hilo.+  Watu wa Daudi wakamuambia: “Hii ndiyo siku yenye Yehova anakuambia, ‘Angalia! Ninamutia adui yako katika mukono wako,+ na unaweza kumutendea jambo lolote lenye linaonekana kuwa la muzuri kwako.’” Kwa hiyo Daudi akasimama na kukata kimya-kimya upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono.  Lakini kisha wakati fulani, moyo wa Daudi ukaendelea* kumulaumu+ kwa sababu alikuwa amekata upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono.  Akaambia watu wake: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwa maoni ya Yehova kwamba nimutendee jambo kama hilo bwana wangu, mutiwa-mafuta wa Yehova, kwa kuinua mukono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.”+  Kwa hiyo Daudi akazuia* watu wake kwa maneno hayo, na hakuwaruhusu wamushambulie Sauli. Kuhusu Sauli, alisimama kutoka katika pango na kuenda zake.  Kisha Daudi akasimama na kutoka katika pango na kumuita Sauli: “Bwana wangu mufalme!”+ Wakati Sauli aliangalia nyuma, Daudi aliinamisha uso wake mupaka chini na kuinama uso chini.  Daudi akamuuliza Sauli: “Sababu gani unasikiliza maneno ya watu wenye wanasema, ‘Angalia! Daudi anataka kukufanya mubaya’?+ 10  Siku hii ya leo macho yako mwenyewe yameona namna Yehova alikutia katika mukono wangu ndani ya pango. Lakini wakati mutu fulani alisema nikuue,+ nilikusikilia huruma na kusema, ‘Sitainua mukono wangu juu ya bwana wangu, kwa maana yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.’+ 11  Na angalia, baba yangu, ndiyo, ona upindo wa koti yako yenye haina mikono katika mukono wangu; kwa sababu wakati nilikata upindo wa koti lako lenye halina mikono, sikukuua. Sasa unaweza kuona na kuelewa kwamba sikusudie kukufanya mubaya wala kukuasi, na sijakutendea zambi,+ lakini wewe unaniwinda ili uondoe uzima wangu.*+ 12  Yehova ahukumu katikati yangu na wewe,+ na Yehova akulipize kisasi kwa ajili yangu,+ lakini mukono wangu hautakuja juu yako.+ 13  Kama vile mezali ya zamani inasema, ‘Uovu unatoka kwa waovu,’ lakini mukono wangu hautakuja juu yako. 14  Mufalme wa Israeli ametoka ili kumutafuta nani? Unamufuatilia nani? Imbwa mwenye kufa? Kiroboto* mumoja?+ 15  Yehova akuwe muamuzi, na atahukumu katikati yangu na wewe, na ataona na kutetea kesi yangu ya hukumu+ na kunihukumu na kuniokoa katika mukono wako.” 16  Wakati Daudi alimaliza kumuambia maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwana wangu?”+ Na Sauli akaanza kulia kwa sauti kubwa. 17  Akamuambia Daudi: “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi, kwa maana umenitendea muzuri na mimi nimekulipa uovu.+ 18  Ndiyo, leo umeniambia kuhusu mema yenye ulitenda kwa kukosa kuniua wakati Yehova alinitia katika mukono wako.+ 19  Kwa maana ni mutu gani anamupata adui yake na kumuacha aende zake bila kumufanya mubaya? Yehova atakupatia zawabu ya mema+ kwa sababu ya mambo yenye umenifanyia leo. 20  Na sasa angalia! Ninajua hakika kwamba utatawala ukiwa mufalme+ na kwamba ufalme wa Israeli utadumu katika mukono wako. 21  Sasa uniapie katika jina la Yehova+ kwamba hautafuta wazao wangu* kisha mimi na kwamba hautaharibu jina langu kutoka katika nyumba ya baba yangu.”+ 22  Kwa hiyo Daudi akamuapia Sauli, kisha Sauli akaenda kwenye nyumba yake.+ Lakini Daudi na watu wake wakapanda kuenda kwenye ngome.+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Tnn., “afunike miguu yake.”
Ao “zamiri ya Daudi ikaendelea.”
Ao pengine, “akasambaza.”
Ao “nafsi yangu.”
Kiroboto ni kidudu kidogo chenye kuruka ambacho kinaishi katika mavumbi na kwenye wanyama.
Tnn., “mbegu yangu.”