Cha Kwanza cha Samweli 24:1-22
24 Wakati tu Sauli alirudia kisha kufuatilia Wafilisti, walimuambia: “Angalia! Daudi iko* katika jangwa la En-gedi.”+
2 Kwa hiyo Sauli akachukua wanaume elfu tatu (3 000) wenye walichaguliwa katika Israeli yote na akaenda kumutafuta Daudi na watu wake kwenye miteremuko mikali yenye miamba ya mbuzi wa milima.
3 Sauli akafika kwenye mazizi* ya majiwe ya kondoo pembeni ya barabara, mahali kwenye kulikuwa pango, na akaingia ndani ili ajisaidie,* wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa katika sehemu za ndani kabisa nyuma ya pango hilo.+
4 Watu wa Daudi wakamuambia: “Hii ndiyo siku yenye Yehova anakuambia, ‘Angalia! Ninamutia adui yako katika mukono wako,+ na unaweza kumutendea jambo lolote lenye linaonekana kuwa la muzuri kwako.’” Kwa hiyo Daudi akasimama na kukata kimya-kimya upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono.
5 Lakini kisha wakati fulani, moyo wa Daudi ukaendelea* kumulaumu+ kwa sababu alikuwa amekata upindo wa koti ya Sauli yenye haina mikono.
6 Akaambia watu wake: “Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwa maoni ya Yehova kwamba nimutendee jambo kama hilo bwana wangu, mutiwa-mafuta wa Yehova, kwa kuinua mukono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.”+
7 Kwa hiyo Daudi akazuia* watu wake kwa maneno hayo, na hakuwaruhusu wamushambulie Sauli. Kuhusu Sauli, alisimama kutoka katika pango na kuenda zake.
8 Kisha Daudi akasimama na kutoka katika pango na kumuita Sauli: “Bwana wangu mufalme!”+ Wakati Sauli aliangalia nyuma, Daudi aliinamisha uso wake mupaka chini na kuinama uso chini.
9 Daudi akamuuliza Sauli: “Sababu gani unasikiliza maneno ya watu wenye wanasema, ‘Angalia! Daudi anataka kukufanya mubaya’?+
10 Siku hii ya leo macho yako mwenyewe yameona namna Yehova alikutia katika mukono wangu ndani ya pango. Lakini wakati mutu fulani alisema nikuue,+ nilikusikilia huruma na kusema, ‘Sitainua mukono wangu juu ya bwana wangu, kwa maana yeye ni mutiwa-mafuta wa Yehova.’+
11 Na angalia, baba yangu, ndiyo, ona upindo wa koti yako yenye haina mikono katika mukono wangu; kwa sababu wakati nilikata upindo wa koti lako lenye halina mikono, sikukuua. Sasa unaweza kuona na kuelewa kwamba sikusudie kukufanya mubaya wala kukuasi, na sijakutendea zambi,+ lakini wewe unaniwinda ili uondoe uzima wangu.*+
12 Yehova ahukumu katikati yangu na wewe,+ na Yehova akulipize kisasi kwa ajili yangu,+ lakini mukono wangu hautakuja juu yako.+
13 Kama vile mezali ya zamani inasema, ‘Uovu unatoka kwa waovu,’ lakini mukono wangu hautakuja juu yako.
14 Mufalme wa Israeli ametoka ili kumutafuta nani? Unamufuatilia nani? Imbwa mwenye kufa? Kiroboto* mumoja?+
15 Yehova akuwe muamuzi, na atahukumu katikati yangu na wewe, na ataona na kutetea kesi yangu ya hukumu+ na kunihukumu na kuniokoa katika mukono wako.”
16 Wakati Daudi alimaliza kumuambia maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwana wangu?”+ Na Sauli akaanza kulia kwa sauti kubwa.
17 Akamuambia Daudi: “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi, kwa maana umenitendea muzuri na mimi nimekulipa uovu.+
18 Ndiyo, leo umeniambia kuhusu mema yenye ulitenda kwa kukosa kuniua wakati Yehova alinitia katika mukono wako.+
19 Kwa maana ni mutu gani anamupata adui yake na kumuacha aende zake bila kumufanya mubaya? Yehova atakupatia zawabu ya mema+ kwa sababu ya mambo yenye umenifanyia leo.
20 Na sasa angalia! Ninajua hakika kwamba utatawala ukiwa mufalme+ na kwamba ufalme wa Israeli utadumu katika mukono wako.
21 Sasa uniapie katika jina la Yehova+ kwamba hautafuta wazao wangu* kisha mimi na kwamba hautaharibu jina langu kutoka katika nyumba ya baba yangu.”+
22 Kwa hiyo Daudi akamuapia Sauli, kisha Sauli akaenda kwenye nyumba yake.+ Lakini Daudi na watu wake wakapanda kuenda kwenye ngome.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “eko.”
^ Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
^ Tnn., “afunike miguu yake.”
^ Ao “zamiri ya Daudi ikaendelea.”
^ Ao pengine, “akasambaza.”
^ Ao “nafsi yangu.”
^ Kiroboto ni kidudu kidogo chenye kuruka ambacho kinaishi katika mavumbi na kwenye wanyama.
^ Tnn., “mbegu yangu.”