Cha Kwanza cha Samweli 21:1-15

  • Daudi anakula mikate ya wonyesho kule Nobu (1-9)

  • Daudi anajifanya kuwa mwenda-wazimu kule Gati (10-15)

21  Kisha wakati fulani Daudi akafika Nobu+ kwa kuhani Ahimeleki. Ahimeleki akaanza kutetemeka wakati alikutana na Daudi, na akamuambia: “Sababu gani uko peke yako na hakuna mutu pamoja na wewe?”+ 2  Daudi akamujibu kuhani Ahimeleki: “Mufalme aliniagiza nifanye jambo fulani, lakini alisema, ‘Usimujulishe mutu yeyote kuhusu kazi yenye ninakutuma ufanye na kuhusu maagizo yenye nimekupatia.’ Nilisikilizana na vijana wangu tukutane mahali fulani. 3  Sasa kama uko na mikate tano (5), unipatie tu mikate hiyo, ao kitu chochote chenye kitapatikana.” 4  Lakini kuhani akamuambia Daudi: “Kwa sasa hakuna mikate ya kawaida, lakini kuko mikate mitakatifu+⁠—ikiwa tu vijana wako wamejiepusha* na wanamuke.”+ 5  Daudi akamujibu kuhani: “Hakika tumejiepusha na wanamuke kama vile tulifanya mbele wakati nilienda katika mapambano ya kijeshi.+ Kama miili ya vijana hawa ni mitakatifu hata wakati kazi yenye walitumwa wafanye ni ya kawaida, je, haiko mitakatifu zaidi leo?” 6  Kwa hiyo kuhani akamupatia mikate mitakatifu,+ kwa sababu hapakukuwa mikate ingine isipokuwa mikate ya wonyesho, yenye ilikuwa imeondolewa mbele ya Yehova ili mikate mipya iwekwe pa nafasi yake siku hiyo yenye iliondolewa. 7  Sasa mumoja wa watumishi wa Sauli alikuwa kule siku hiyo, akiwa amezuiliwa mbele ya Yehova. Jina lake lilikuwa Doegi+ Mwedomu,+ mukubwa wa wachungaji wa Sauli. 8  Basi Daudi akamuambia Ahimeleki: “Je, uko na mukuki ao upanga hapa? Sikubeba upanga wangu wala silaha zangu, kwa sababu kazi yenye mufalme alituma ifanywe ilipaswa kufanywa haraka.” 9  Kwa hiyo kuhani akasema: “Upanga wa Goliati+ ule Mufilisti, mwenye ulipiga na kuua katika Bonde* la Ela,+ uko hapa, umefungwa kwa kitambaa nyuma ya efodi.+ Kama unataka kuukamata kwa ajili yako, uukamate, kwa sababu ndio upanga pekee wenye uko hapa.” Daudi akasema: “Hakuna upanga wenye uko kama huo. Unipatie upanga huo.” 10  Siku hiyo Daudi akaondoka na kuendelea kumukimbia Sauli,+ na mwishowe akafika kwa Mufalme Akishi wa Gati.+ 11  Watumishi wa Akishi wakamuambia Akishi: “Je, huyu haiko Daudi mufalme wa ile inchi? Je, haiko yeye ndiye waliimba kumuhusu wakati walicheza dansi, na kusema,‘Sauli amepiga na kuua maelfu yake,Na Daudi makumi yake ya maelfu’?”+ 12  Daudi akaweka maneno hayo katika moyo wake, na akamuogopa sana+ Mufalme Akishi wa Gati. 13  Kwa hiyo akajifanya kuwa mwenda-wazimu+ mbele yao na akatenda kama mwenda-wazimu kati yao.* Alikuwa anatia alama kwenye milango ya mulango mukubwa na kuacha mate yake yatiririke kwenye ndevu zake. 14  Mwishowe Akishi akaambia watumishi wake: “Munaona kwamba mutu huyu ni mwenda-wazimu! Sababu gani munamuleta kwangu? 15  Je, nimepungukiwa na wenda-wazimu ili nihitaji kuwa na mutu huyu mwenye kutenda kiwazimu mbele yangu? Je, mutu huyu ataingia katika nyumba yangu?”

Maelezo ya Chini

Ao “hawakufanya ngono.”
Ao “Eneo Tambarare la Chini.”
Tnn., “katika mukono wao.”