Matendo 2:1-47

2  Basi siku ya sherehe ya Pentekoste+ ilipokuwa ikiendelea walikuwa wote pamoja mahali pale pale,  na ghafula kukatokea kutoka mbinguni kelele kama ile ya upepo wenye nguvu unaovuma, nao ukaijaza nyumba yote ambamo walikuwa wameketi.+  Nao wakaona ndimi kama za moto,+ nazo zikagawanyika huku na huku, na mmoja ukaketi juu ya kila mmoja wao,  nao wote wakajazwa roho takatifu+ wakaanza kusema katika lugha+ tofauti, kama vile roho ilivyokuwa ikiwawezesha kusema.  Ikawa kwamba, kulikuwa na Wayahudi+ wakikaa katika Yerusalemu, watu wenye kumheshimu Mungu,+ kutoka kila taifa kati ya yale yaliyo chini ya mbingu.  Kwa hiyo, mvumo huo ulipotokea, umati ukaja pamoja nao ukashikwa na bumbuazi, kwa sababu kila mmoja aliwasikia wakisema katika lugha yake mwenyewe.  Kwa kweli, walishangaa na kuanza kustaajabu na kusema: “Tazama, wote hawa wanaosema ni Wagalilaya,+ sivyo?  Hata hivyo, imewezekanaje kwamba sisi, kila mmoja wetu, tunasikia lugha yake mwenyewe tuliyozaliwa nayo?  Waparthi na Wamedi+ na Waelami,+ na wakaaji wa Mesopotamia, na Yudea+ na Kapadokia,+ Ponto+ na wilaya ya Asia,+ 10  na Frigia+ na Pamfilia,+ Misri, na sehemu za Libya, ambayo ni kuelekea Kirene, na wakaaji wa muda wa kutoka Roma, Wayahudi na pia wageuzwa-imani,+ 11  Wakrete+ na Waarabu,+ tunawasikia wakisema katika lugha zetu juu ya mambo makuu ya Mungu.” 12  Ndiyo, wote wakashangaa na kustaajabu, wakiambiana: “Jambo hili linamaanisha nini?” 13  Hata hivyo, watu tofauti waliwadhihaki na kuanza kusema: “Wamejaa divai tamu.”+ 14  Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja+ na kupaaza sauti yake na kuwaambia hivi: “Watu wa Yudea nanyi nyote wakaaji wa Yerusalemu,+ acheni hili lijulikane kwenu nanyi tegeni sikio msikie maneno yangu. 15  Kwa kweli, watu hawa hawakulewa,+ kama mnavyofikiri, kwa maana ni saa tatu ya mchana. 16  Badala yake, hili ndilo lililosemwa kupitia nabii Yoeli, 17  ‘ “Na katika siku za mwisho,” Mungu asema, “Nitaimimina sehemu ya roho yangu+ juu ya kila namna ya mwili, nao wana wenu na binti zenu watatoa unabii nao wanaume wenu vijana wataona maono na wazee wenu wataota ndoto;+ 18  na hata juu ya watumwa wangu na juu ya wajakazi wangu nitaimimina sehemu ya roho yangu katika siku hizo, nao watatoa unabii.+ 19  Nami nitatoa maajabu mbinguni juu na ishara duniani chini, damu na moto na ukungu wa moshi;+ 20  jua+ litageuzwa kuwa giza na mwezi kuwa damu kabla ya kufika kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye fahari.+ 21  Na kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.” ’+ 22  “Watu wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu Mnazareti,+ mwanamume aliyeonyeshwa hadharani na Mungu kwenu kupitia kazi zenye nguvu+ na mambo ya ajabu na ishara ambazo Mungu alifanya kupitia kwake katikati yenu,+ kama vile ninyi wenyewe mnavyojua, 23  mwanamume huyu, kama aliyetolewa kwa shauri lililoamuliwa na kwa ujuzi wa kimbele wa Mungu,+ mlimfunga kwenye mti kwa mkono wa waasi-sheria na kumwondolea mbali.+ 24  Lakini Mungu alimfufua+ kwa kuyafungua maumivu makali ya kifo,+ kwa sababu haikuwezekana kiendelee kumshika.+ 25  Kwa maana Daudi anasema juu yake, ‘Yehova alikuwa mbele ya macho yangu daima; kwa sababu yuko upande wa mkono wangu wa kuume ili nisipate kutikiswa kamwe.+ 26  Kwa ajili ya hilo moyo wangu ulichangamka na ulimi wangu ukashangilia sana. Zaidi ya hayo, hata mwili wangu utakaa katika tumaini;+ 27  kwa sababu hutaiacha nafsi yangu katika Kaburi,* wala hutamruhusu mshikamanifu wako aone uharibifu.+ 28  Umefanya njia za uzima zijulikane kwangu, utanijaza uchangamfu mwingi kwa uso wako.’+ 29  “Wanaume, akina ndugu, inaruhusika kusema nanyi kwa uhuru wa kusema juu ya Daudi yule kichwa cha familia, kwamba alikufa+ na pia akazikwa na kaburi lake liko katikati yetu mpaka leo hii. 30  Kwa hiyo, kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemwapia kwa kiapo kwamba angemketisha mmoja kutoka kati ya uzao wa viuno vyake juu ya kiti chake cha ufalme,+ 31  aliona kimbele na kusema kuhusu ufufuo wa Kristo, kwamba hakuachwa katika Kaburi* wala mwili wake haukuona uharibifu.+ 32  Yesu huyo Mungu alimfufua, uhakika ambao sisi sote ni mashahidi.+ 33  Kwa hiyo kwa sababu aliinuliwa kwenye mkono wa kuume wa Mungu+ na kupokea roho takatifu iliyoahidiwa kutoka kwa Baba,+ amemimina hiki ambacho ninyi mnakiona na kukisikia. 34  Kwa kweli Daudi hakupanda mbinguni,+ bali yeye mwenyewe anasema, ‘Yehova alimwambia Bwana wangu: “Keti kwenye mkono wangu wa kuume,+ 35  mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.” ’+ 36  Kwa hiyo acha nyumba yote ya Israeli ijue kwa hakika kwamba Mungu alimfanya Bwana+ na pia Kristo, Yesu huyu ambaye ninyi mlimtundika mtini.”+ 37  Basi waliposikia hilo walichomwa moyoni,+ nao wakamwambia Petro na wale mitume wengine: “Wanaume, akina ndugu, tufanye nini?”+ 38  Petro akawaambia: “Tubuni,+ na acheni kila mmoja wenu abatizwe+ katika jina+ la Yesu Kristo kwa msamaha+ wa dhambi zenu, nanyi mtapokea zawadi ya bure+ ya roho takatifu. 39  Kwa maana ahadi+ ni kwenu na kwa watoto wenu na kwa wale wote walio mbali,+ wengi kadiri ambayo Yehova Mungu wetu huenda akawaita kwake.”+ 40  Na kwa maneno mengine mengi akatoa ushahidi kamili na kuendelea kuwahimiza, akisema: “Okoleweni kutoka katika kizazi hiki kilicho kombo.”+ 41  Kwa hiyo wale waliokubali neno lake kwa ukunjufu wa moyo wakabatizwa,+ na katika siku hiyo nafsi karibu elfu tatu zikaongezwa.+ 42  Nao wakaendelea kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume na kushirikiana,+ katika kula milo+ na katika sala.+ 43  Kwa kweli, woga ukaanza kuwa juu ya kila nafsi, na mambo mengi ya ajabu na ishara nyingi zikaanza kutukia kupitia mitume.+ 44  Wale wote waliopata kuwa waamini walikuwa pamoja katika kuwa na mambo yote kwa ushirika,+ 45  nao wakaanza kuuza miliki na mali zao+ na kuwagawia wote mapato hayo, kulingana na vile yeyote alivyokuwa na uhitaji.+ 46  Na siku baada ya siku walikuwa wakihudhuria daima kwenye hekalu kwa umoja,+ nao walikula milo yao katika nyumba za faragha na kushiriki chakula kwa shangwe+ kuu na weupe wa moyo, 47  wakimsifu Mungu na kupata kibali kwa watu wote.+ Wakati uleule Yehova akaendelea kuongezea+ kwao kila siku wale waliokuwa wakiokolewa.+

Maelezo ya Chini

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.
Hadesi. Tazama Nyongeza 4.