Matendo 3:1-26
3 Basi Petro na Yohana walikuwa wakipanda kwenda hekaluni kwa ajili ya saa ya sala, saa tisa,+
2 na mwanamume fulani aliyekuwa kilema tangu alipokuwa katika tumbo la uzazi la mama yake+ alikuwa akibebwa, nao walikuwa wakimweka kila siku karibu na mlango wa hekalu ulioitwa Mzuri,+ ili kuomba zawadi za rehema kutoka kwa wale waliokuwa wakiingia katika hekalu.+
3 Alipowaona Petro na Yohana wakiwa karibu kuingia ndani ya hekalu akaanza kuomba apate zawadi za rehema.+
4 Lakini Petro, pamoja na Yohana, wakamtazama+ na kusema: “Tuangalie sisi.”
5 Kwa hiyo akawaangalia, akitarajia kupata kitu fulani kutoka kwao.
6 Hata hivyo, Petro akasema: “Fedha na dhahabu sina, lakini kile nilicho nacho ndicho ninachokupa:+ Katika jina la Yesu Kristo Mnazareti,+ tembea!”+
7 Ndipo akamshika mkono wa kuume na kumwinua.+ Papo hapo nyayo za miguu yake na vifundo vya miguu yake vikafanywa imara;+
8 naye akaruka juu,+ akasimama na kuanza kutembea, kisha akaingia pamoja nao katika hekalu,+ akitembea na kuruka-ruka na kumsifu Mungu.
9 Na watu wote+ wakamwona akitembea na kumsifu Mungu.
10 Zaidi ya hayo, wakaanza kumtambua, kwamba huyu ndiye mtu aliyekuwa akiketi kwa ajili ya zawadi za rehema penye Lango Zuri+ la hekalu, nao wakajawa na mshangao na shangwe+ kwa sababu ya jambo lililokuwa limetukia kwake.
11 Basi, kwa kuwa mtu huyo alikuwa akiwashikilia Petro na Yohana, watu wote waliwakimbilia pamoja kwenye eneo lililoitwa mistari ya nguzo za Sulemani,+ wakiwa wamepotewa na akili kwa sababu ya mshangao.
12 Petro alipoona jambo hilo, akawaambia watu hao: “Watu wa Israeli, kwa nini mnastaajabu juu ya hili, au kwa nini mnatutazama kana kwamba tumemfanya atembee kwa nguvu za kibinafsi au kwa ujitoaji-kimungu?+
13 Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo,+ Mungu wa mababu zetu, amemtukuza+ Mtumishi+ wake, Yesu, ambaye ninyi mlimpeleka+ na kumkana mbele ya uso wa Pilato, alipokuwa ameamua kumfungua.+
14 Ndiyo, ninyi mlimkana huyo aliye mtakatifu na mwadilifu,+ nanyi mkaomba mpewe kwa hiari mwanamume, muuaji,+
15 lakini mlimuua Wakili Mkuu wa uzima.+ Lakini Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, uhakika ambao sisi ni mashahidi+ wake.
16 Kwa sababu hiyo, kwa imani yetu katika jina lake, jina lake limemfanya awe mwenye nguvu mtu huyu ambaye mnamwona na kumjua, na imani kupitia kwake imempa mtu huyu afya hii kamili mbele ya macho yenu nyote.
17 Na sasa, akina ndugu, ninajua kwamba mlitenda kwa kutojua,+ kama vile watawala+ wenu pia walivyotenda.
18 Lakini katika njia hiyo Mungu ametimiza mambo aliyotangaza kimbele kupitia kinywa cha manabii wote, kwamba Kristo wake angeteseka.+
19 “Kwa hiyo, tubuni+ na mgeuke+ ili dhambi zenu zipate kufutwa,+ ili majira ya kuburudisha+ yapate kuja kutoka kwa uso wa Yehova
20 na kwamba apate kumtuma Kristo aliyewekwa rasmi kwa ajili yenu, Yesu,
21 ambaye mbingu, kwa kweli,+ lazima imweke ndani yake mpaka nyakati za kurudishwa+ kwa mambo yote ambayo Mungu alisema kupitia kinywa cha manabii+ wake watakatifu wa nyakati za kale.
22 Kwa kweli, Musa alisema, ‘Yehova Mungu atawainulia kutoka kati ya ndugu zenu nabii kama mimi.+ Msikilizeni huyo kulingana na mambo yote anayowaambia ninyi.+
23 Kwa kweli, nafsi yoyote isiyomsikiliza Nabii huyo itaangamizwa kutoka kati ya watu.’+
24 Na kwa kweli, manabii wote tangu Samweli na kuendelea na wale waliofuata, wengi kadiri ambavyo wamesema, wamezitangaza waziwazi pia siku hizi.+
25 Ninyi ndio wana+ wa manabii na wa agano ambalo Mungu aliagana pamoja na mababu zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Na katika uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.’+
26 Baada ya kumwinua Mtumishi wake, Mungu alimtuma kwenu kwanza+ ili kuwabariki ninyi kwa kugeuzia mbali kila mmoja kutoka kwenye matendo yenu maovu.”