Matendo 11:1-30
11 Sasa mitume na ndugu waliokuwa katika Yudea wakasikia kwamba watu wa mataifa+ walikuwa pia wamepokea neno la Mungu.
2 Kwa hiyo Petro alipopanda mpaka Yerusalemu, waliokuwa wakiunga mkono kutahiriwa+ wakaanza kushindana naye,
3 wakisema aliingia ndani ya nyumba ya watu ambao hawakuwa wametahiriwa naye alikula pamoja nao.
4 Ndipo Petro akawaeleza waziwazi, akisema:
5 “Mimi nilikuwa katika jiji la Yopa nikisali, na katika njozi nikaona maono, chombo cha namna fulani kikishuka kama shuka kubwa la kitani, kikishushwa kwa ncha zake nne kutoka mbinguni, nacho kikaja moja kwa moja mahali nilipokuwa.
6 Nilipotazama ndani yake, nilichunguza na kuona viumbe vya dunia vyenye miguu minne na wanyama-mwitu na vitu vinavyotambaa na ndege wa mbinguni.+
7 Pia nikasikia sauti ikiniambia, ‘Simama, Petro, chinja ule!’+
8 Lakini nikasema, ‘Sivyo hata kidogo, Bwana, kwa sababu kitu najisi au kisicho safi hakijapata kamwe kuingia ndani ya kinywa changu.’+
9 Mara ya pili sauti kutoka mbinguni ikajibu, ‘Wewe acha kuviita najisi vitu ambavyo Mungu ametakasa.’+
10 Hilo likatokea mara ya tatu, na kila kitu kikavutwa juu tena kuingia mbinguni.+
11 Pia, tazama! wakati huohuo wanaume watatu walikuwa wamesimama karibu na nyumba tuliyokuwamo, wakiwa wametumwa kutoka Kaisaria kuja kwangu.+
12 Kwa hiyo roho+ ikaniambia niende pamoja nao, bila kuwa na shaka hata kidogo. Lakini ndugu sita hawa pia walikwenda pamoja nami, nasi tukaingia ndani ya nyumba ya mwanamume huyo.+
13 “Alitueleza jinsi alivyomwona malaika amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yopa wakamwite Simoni anayeitwa Petro,+
14 naye atasema nawe mambo ambayo yatakuwezesha wewe na watu wote wa nyumba yako kuokolewa.’+
15 Lakini nilipoanza kusema, roho takatifu ikawaangukia kama vile ilivyoanguka pia juu yetu mwanzoni.+
16 Ndipo nikayakumbuka maneno ya Bwana, jinsi alivyokuwa akisema, ‘Yohana alibatiza kwa maji,+ lakini ninyi mtabatizwa kwa roho takatifu.’+
17 Kwa hiyo, ikiwa Mungu aliwapa hao zawadi ileile ya bure kama vile alivyotupa sisi pia ambao tumemwamini Bwana Yesu Kristo,+ mimi ni nani hata niweze kumzuia Mungu?”+
18 Basi waliposikia mambo hayo, wakakubali kimyakimya,+ nao wakamtukuza Mungu,+ wakisema: “Kwa hiyo, basi, Mungu ameruhusu toba kwa kusudi la uzima kwa watu wa mataifa pia.”+
19 Kwa sababu hiyo wale waliokuwa wametawanywa+ na dhiki iliyotokea kwa sababu ya Stefano wakapita kwenda mpaka Foinike+ na Kipro+ na Antiokia, lakini hawakusema lile neno kwa yeyote ila kwa Wayahudi tu.+
20 Hata hivyo, kati yao kulikuwa na wanaume fulani wa Kipro na Kirene waliokuja Antiokia na kuanza kuongea na watu wenye kusema Kigiriki,+ wakitangaza habari njema ya Bwana Yesu.+
21 Zaidi ya hayo, mkono wa Yehova+ ulikuwa pamoja nao, na hesabu kubwa ya waliopata kuwa waamini wakageuka kumwelekea Bwana.+
22 Kutaniko lililokuwa katika Yerusalemu likasikia juu yao, nao wakamtuma Barnaba+ mpaka Antiokia.
23 Alipofika na kuziona fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu, akashangilia+ na kuanza kuwatia wote moyo waendelee katika Bwana wakiwa na azimio la moyoni;+
24 kwa maana alikuwa mwanamume mwema na mwenye kujaa roho takatifu na imani. Na umati mkubwa ukaongezwa kwa Bwana.+
25 Kwa hiyo akaenda zake mpaka Tarso+ ili kumtafuta Sauli+
26 na, baada ya kumpata, akamleta Antiokia. Hivyo ikatukia kwamba kwa mwaka mzima wakakusanyika pamoja nao katika kutaniko na kufundisha umati mkubwa, na kule Antiokia ndipo ambapo kwa mara ya kwanza wanafunzi kwa uongozi wa kimungu waliitwa Wakristo.+
27 Basi katika siku hizo manabii+ walishuka kutoka Yerusalemu mpaka Antiokia.
28 Mmoja kati yao anayeitwa jina Agabo+ akasimama na kuonyesha kupitia roho kwamba njaa kali ilikuwa karibu kuja juu ya dunia nzima inayokaliwa;+ ambayo, kama ilivyo, ilitukia wakati wa Klaudio.
29 Kwa hiyo wanafunzi wakaamua, kila mmoja kwa kadiri ambayo yeyote angeweza kutoa,+ wafanye huduma ya kupeleka misaada+ kwa akina ndugu waliokuwa wakikaa Yudea;
30 nao wakafanya hivyo, wakaipeleka kwa wanaume wazee kwa mkono wa Barnaba na Sauli.+