Matendo 28:1-31

28  Na tulipokuwa tumefika mahali salama, tukapata habari kwamba kisiwa hicho kilikuwa kikiitwa Malta.+  Na watu hao wenye kusema lugha ya kigeni wakatuonyesha fadhili+ za kibinadamu zisizo za kawaida, kwa maana waliwasha moto na kutukaribisha sote na kutupa msaada kwa sababu ya mvua iliyokuwa ikinyesha na kwa sababu ya baridi.+  Lakini Paulo alipokusanya tita la kuni na kuliweka juu ya moto, nyoka-kipiri akatoka kwa sababu ya joto na kujifunga kwenye mkono wake.  Watu hao wenye kusema lugha ya kigeni walipoona huyo kiumbe mwenye sumu akining’inia kwenye mkono wake, wakaanza kuambiana: “Hakika mtu huyu ni muuaji, na ingawa alifika mahali salama kutoka baharini, haki yenye kudai kisasi haikumruhusu aendelee kuishi.”  Hata hivyo, akamkung’uta kiumbe huyo mwenye sumu na kumtupa ndani ya moto, naye hakupatwa na dhara.+  Lakini wao walikuwa wakitarajia atavimba kwa sababu ya mwasho au kwa ghafula aanguke na kufa. Baada ya kungojea kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna jambo lolote baya lililompata, wakabadili maoni yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.+  Sasa katika ujirani wa mahali hapo mkuu wa kisiwa hicho, anayeitwa Publio, alikuwa na mashamba; naye akatukaribisha na kutupokea kwa hisani kwa siku tatu.  Lakini ikawa kwamba baba ya Publio alikuwa amelala akitaabishwa na homa na ugonjwa wa kuhara damu, na Paulo akaingia alimokuwa na kusali, akaweka mikono+ yake juu yake akamponya.+  Baada ya jambo hilo kutukia, watu wale wengine kisiwani waliokuwa na magonjwa wakaanza pia kuja kwake na kuponywa.+ 10  Nao pia wakatupa sisi zawadi nyingi na, tulipokuwa tukisafiri, wakapakia vitu kwa ajili ya mahitaji yetu. 11  Miezi mitatu baadaye tukasafiri kutoka Aleksandria+ kwa mashua iliyokuwa imekaa wakati wa majira ya baridi kali katika kisiwa hicho na yenye sanamu ya gubeti ya “Wana wa Zeu.” 12  Nasi tukaegesha katika bandari ya Sirakusa tukakaa siku tatu, 13  mahali ambapo kutoka hapo tulienda tukizunguka na kufika Regiamu. Na siku moja baadaye upepo wa kusini ukazuka nasi tukaingia Puteoli siku ya pili. 14  Tukawakuta akina ndugu hapo nao wakatusihi tukae pamoja nao kwa siku saba; na kwa njia hii tukaja kuelekea Roma. 15  Na kutoka huko akina ndugu, waliposikia habari juu yetu, wakaja kukutana nasi mpaka Soko la Apio na Mikahawa Mitatu na, alipowaona, Paulo akamshukuru Mungu na kujipa moyo.+ 16  Mwishowe, tulipoingia Roma, Paulo akaruhusiwa+ kukaa akiwa peke yake pamoja na askari-jeshi mwenye kumlinda. 17  Hata hivyo, siku tatu baadaye akawaita pamoja wale waliokuwa wakuu wa Wayahudi. Walipokuwa wamekusanyika, akaanza kuwaambia: “Wanaume, akina ndugu, ijapokuwa sikuwa nimefanya jambo lolote kinyume cha watu au desturi za mababu zetu,+ nilitolewa nikiwa mfungwa Yerusalemu na kutiwa mikononi mwa Waroma.+ 18  Na hawa, baada ya kufanya uchunguzi,+ walitaka kunifungua,+ kwa kuwa hakukuwa na sababu yoyote kwangu ya kuuawa.+ 19  Lakini Wayahudi walipoendelea kusema vibaya juu ya jambo hilo, nililazimika kukata rufani+ kwa Kaisari, lakini si kana kwamba nilikuwa na jambo lolote la kushtaki taifa langu. 20  Kwa kweli kwa sababu hii nilisihi niwaone na kusema nanyi, kwa maana nimefungwa mnyororo+ huu kwa sababu ya tumaini+ la Israeli.” 21  Wakamwambia: “Wala sisi hatujapokea barua zinazokuhusu wewe kutoka Yudea, wala hakuna yeyote wa akina ndugu ambaye amefika aliyetujulisha au kusema jambo lolote baya juu yako. 22  Lakini tunaona inafaa kusikia maoni yako kutoka kwako, kwa maana kweli kwa habari ya madhehebu+ hii tunajua kwamba kila mahali huwa inasemwa vibaya.”+ 23  Basi wakapanga siku fulani ya kuwa pamoja naye, nao wakaja kwake wakiwa hesabu kubwa zaidi katika makao yake. Naye akawaeleza jambo hilo kwa kutoa ushahidi kamili kuhusiana na ufalme wa Mungu+ na kwa kutumia ushawishi kwao kuhusu Yesu kutoka katika sheria ya Musa+ na pia Manabii,+ tangu asubuhi mpaka jioni. 24  Na wengine wakaanza kuamini+ mambo yaliyosemwa; wengine hawakuamini.+ 25  Kwa hiyo, kwa sababu walikosa kukubaliana, wakaanza kuondoka, huku Paulo akieleza jambo hili moja: “Roho takatifu kwa kufaa ilisema kupitia Isaya nabii kwa mababu zenu, 26  ikisema, ‘Nenda kwa watu hawa na kusema: “Kwa kusikia, mtasikia lakini msielewe kamwe; na, kutazama, mtatazama, lakini msione kamwe.+ 27  Kwa maana moyo wa watu hawa umekuwa mgumu, na kwa masikio yao wamesikia bila kuitikia, nao wamefunga macho yao; ili wasione kamwe kwa macho yao na kusikia kwa masikio yao na kuelewa kwa moyo wao na kugeuka, nami niwaponye.” ’+ 28  Kwa hiyo jueni kwamba njia hii ambayo Mungu anaitumia kuokoa, imepelekwa nje kwa mataifa;+ wao hakika wataisikiliza.”+ 29  —— 30  Kwa hiyo akakaa miaka miwili kamili katika nyumba yake mwenyewe ya kukodiwa,+ naye akawa akiwakaribisha kwa fadhili wale wote walioingia ndani kwake, 31  akiwahubiria ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yanayohusu Bwana Yesu Kristo kwa uhuru wa kusema+ ulio mkubwa zaidi, bila kizuizi.

Maelezo ya Chini