Matendo 18:1-28
18 Baada ya hayo akaondoka Athene na kuja Korintho.
2 Naye akamkuta Myahudi fulani anayeitwa Akila,+ mzaliwa wa Ponto ambaye alikuwa amekuja hivi karibuni kutoka Italia,+ na Prisila mke wake, kwa sababu Klaudio+ alikuwa ameagiza Wayahudi wote waondoke Roma. Kwa hiyo akawaendea
3 na kwa sababu ya kuwa wa kazi ileile akakaa nyumbani kwao, nao wakafanya kazi,+ kwa maana kazi yao ilikuwa ya kutengeneza mahema.
4 Hata hivyo, yeye alikuwa akitoa hotuba katika sinagogi+ kila sabato na alikuwa akiwashawishi Wayahudi na Wagiriki.
5 Basi, Sila+ na Timotheo+ pia waliposhuka kutoka Makedonia, Paulo akaanza kushughulika sana na lile neno, akiwatolea Wayahudi ushahidi ili kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo.+
6 Lakini walipoendelea kupinga na kutukana,+ akayakung’uta mavazi+ yake na kuwaambia: “Damu+ yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe. Mimi ni safi.+ Tangu sasa na kuendelea nitaenda kwa watu wa mataifa.”+
7 Basi akahama huko na kuingia katika nyumba ya mwanamume anayeitwa Titio Yusto, mwabudu wa Mungu, ambaye nyumba yake ilikuwa inashikana na sinagogi.
8 Lakini Krispo+ ofisa-msimamizi wa sinagogi akawa mwamini katika Bwana, na ndivyo na watu wote wa nyumba yake. Na wengi kati ya Wakorintho waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.
9 Zaidi ya hayo, wakati wa usiku Bwana akamwambia Paulo+ kupitia maono: “Usiogope, bali endelea kusema wala usinyamaze,
10 kwa sababu mimi nipo pamoja na wewe+ na hakuna mtu atakayekushambulia ili kukutendea jambo baya; kwa maana nina watu wengi katika jiji hili.”
11 Kwa hiyo akakaa huko bila kuondoka kwa mwaka mmoja na miezi sita, akifundisha kati yao neno la Mungu.
12 Sasa Galio alipokuwa liwali+ wa Akaya, Wayahudi wakasimama kwa umoja dhidi ya Paulo na kumwongoza kwenye kiti cha hukumu,+
13 wakisema: “Mtu huyu huongoza watu kinyume cha sheria+ kwenye sadikisho lingine katika kumwabudu Mungu.”
14 Lakini Paulo alipokuwa akitaka kufungua kinywa chake, Galio akawaambia Wayahudi: “Kama kwa kweli lingekuwa ni kosa fulani au tendo baya la uhalifu, enyi Wayahudi, ningekuwa na sababu ya kuwavumilia ninyi.
15 Lakini kama ni mabishano juu ya maneno na majina+ na sheria+ kati yenu, amueni ninyi wenyewe. Mimi sitaki kuwa mwamuzi wa mambo haya.”
16 Ndipo akawafukuza kutoka mbele ya kiti cha hukumu.
17 Kwa hiyo wote wakamshika Sosthene+ ofisa-msimamizi wa sinagogi na kuanza kumpiga mbele ya kiti cha hukumu. Lakini Galio hakujihangaisha hata kidogo na mambo hayo.
18 Hata hivyo, baada ya kukaa siku kadhaa zaidi, Paulo aliwaaga akina ndugu naye akaendelea kusafiri kwenda Siria, na pamoja naye Prisila na Akila, kwa kuwa nywele za kichwa chake zilikuwa zimekatwa+ katika Kenkrea,+ kwa maana alikuwa ameweka nadhiri.
19 Kwa hiyo wakafika Efeso, naye akawaacha huko; lakini yeye mwenyewe akaingia ndani ya sinagogi+ akajadiliana na Wayahudi.
20 Ijapokuwa waliendelea kumwomba akae kwa muda mrefu zaidi, hakukubali
21 bali akawaaga+ na kuwaambia: “Nitarudi kwenu tena, ikiwa Yehova anapenda.”+ Naye akasafiri baharini kutoka Efeso
22 na kushuka mpaka Kaisaria. Naye akapanda kwenda, akalisalimu kutaniko, na kushuka kwenda Antiokia.
23 Na alipokuwa amekaa huko kwa wakati fulani akaondoka na kwenda kutoka mahali mpaka mahali kupitia nchi ya Galatia+ na Frigia,+ akiwatia nguvu+ wanafunzi wote.
24 Sasa Myahudi fulani anayeitwa Apolo,+ mzaliwa wa Aleksandria, mwanamume mfasaha, akafika Efeso; naye alikuwa mwenye ujuzi mwingi sana wa Maandiko.+
25 Mwanamume huyu alikuwa amefundishwa njia ya Yehova kwa mdomo, kwa kuwa alikuwa amewaka roho,+ akaanza kusema na kuyafundisha kwa usahihi mambo juu ya Yesu, lakini akiwa anaufahamu ubatizo+ wa Yohana tu.
26 Na mwanamume huyo akaanza kusema kwa ujasiri katika sinagogi. Prisila na Akila+ walipomsikia, wakamchukua na kumfafanulia kwa usahihi zaidi njia ya Mungu.
27 Tena, kwa sababu alikuwa akitaka kuvuka aingie Akaya, akina ndugu wakawaandikia wanafunzi, wakiwahimiza wamkaribishe kwa fadhili. Kwa hiyo alipofika huko, akawasaidia+ sana wale waliokuwa wameamini kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu;
28 kwa maana kwa juhudi nyingi alithibitisha kikamili hadharani kuwa Wayahudi ni wenye makosa, huku akionyesha kwa Maandiko+ kwamba Yesu alikuwa ndiye Kristo.+