Matendo 12:1-25
12 Karibu na wakati huo Mfalme Herode alitumia mikono yake kuwatendea vibaya+ baadhi ya wale wa kutaniko.
2 Alimuua kwa upanga+ Yakobo ndugu ya Yohana.+
3 Alipoona kuwa jambo hilo limewapendeza Wayahudi,+ akamkamata Petro pia. (Ikawa kwamba hizo zilikuwa siku za keki zisizo na chachu.)+
4 Na alipomkamata, akamweka gerezani,+ akamkabidhi kwenye zamu nne za askari-jeshi wanne kila moja ili kumlinda, kwa kuwa alikusudia kumleta mbele ya watu baada ya pasaka.+
5 Kwa hiyo Petro alikuwa gerezani; lakini kutaniko lilikuwa likisali+ kwa Mungu kwa juhudi nyingi kwa ajili yake.
6 Sasa Herode alipokuwa karibu kumtoa, usiku huo Petro alikuwa amelala akiwa amefungwa kwa minyororo miwili katikati ya askari-jeshi wawili, na walinzi mbele ya mlango walikuwa wakililinda gereza.
7 Lakini, tazama! malaika wa Yehova akasimama+ kando, na nuru ikang’aa katika chumba cha gereza. Akampiga Petro ubavuni, akamwamsha,+ akisema: “Amka upesi!” Na minyororo yake ikaanguka+ kutoka kwenye mikono yake.
8 Malaika+ akamwambia: “Jifunge kiuno na uvae viatu vyako.” Akafanya hivyo. Mwishowe akamwambia: “Vaa vazi+ lako la nje uendelee kunifuata.”
9 Naye akatoka na kuendelea kumfuata, lakini hakujua kwamba lililokuwa likitukia kupitia malaika lilikuwa halisi. Kwa kweli, alidhani alikuwa akiona maono.+
10 Wakampita askari-mlinzi wa kwanza na wa pili wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea jijini, nalo likafunguka lenyewe mbele yao.+ Na baada ya kutoka wakapita katika barabara moja, na mara malaika akamwacha.
11 Na Petro akarudiwa na fahamu, akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Yehova alimtuma+ malaika wake na kunikomboa+ kutoka mkononi mwa Herode na kutoka katika yote ambayo Wayahudi wote walikuwa wakitarajia.”
12 Na baada ya kufikiria jambo hilo, akaenda kwenye nyumba ya Maria mama ya Yohana aliyeitwa Marko,+ ambamo watu wengi walikuwa wamekusanyika na wakisali.
13 Alipopiga hodi kwenye mlango wa njia ya lango, kijakazi anayeitwa Roda akaja kujibu,
14 na, alipoitambua sauti ya Petro, hakulifungua lango kwa sababu ya shangwe, bali akakimbia ndani na kueleza kwamba Petro alikuwa amesimama mbele ya njia ya lango.
15 Wakamwambia: “Una wazimu.” Lakini akasisitiza kwa nguvu ndivyo ilivyokuwa. Wakaanza kusema: “Ni malaika wake.”+
16 Lakini Petro akakaa hapo akibisha mlango. Walipofungua, wakamwona nao wakashangaa.
17 Lakini akawapungia+ mkono wanyamaze na kuwaambia kirefu jinsi Yehova alivyomtoa gerezani, naye akasema: “Waambieni Yakobo+ na akina ndugu mambo haya.” Ndipo akatoka, akasafiri kwenda mahali pengine.
18 Basi, mchana ulipofika,+ kulikuwa na msukosuko usio mdogo kati ya askari-jeshi kuhusu ni jambo gani kwa kweli lililokuwa limempata Petro.
19 Herode+ akamtafuta kwa bidii na, alipokosa kumpata, akawahoji walinzi na kuwaamuru wapelekwe kuadhibiwa;+ naye akashuka kwenda Yudea mpaka Kaisaria na kukaa huko kwa muda fulani.
20 Sasa yeye alitaka kupigana na watu wa Tiro na wa Sidoni. Kwa hiyo wakamjia kwa umoja na, baada ya kumshawishi Blasto, aliyekuwa msimamizi wa chumba cha kulala cha mfalme, wakaanza kutoa ombi la kutaka amani, kwa sababu nchi yao iligawiwa chakula+ kutoka katika kile cha mfalme.
21 Lakini siku fulani iliyowekwa Herode akajivika vazi la kifalme na kuketi juu ya kiti cha hukumu na kuanza kuwatolea hotuba ya watu wote.
22 Nao watu waliokusanyika wakaanza kupaaza sauti: “Ni sauti ya mungu, wala si ya mwanadamu!”+
23 Papo hapo malaika wa Yehova akampiga,+ kwa sababu hakumpa Mungu utukufu;+ naye akaliwa na wadudu akakata pumzi.
24 Lakini neno+ la Yehova likaendelea kukua na kuenea.+
25 Naye Barnaba+ na Sauli, baada ya kutimiza kikamili ile huduma ya misaada+ katika Yerusalemu, wakarudi na kumchukua pamoja nao Yohana,+ aliyeitwa Marko.