Matendo 23:1-35
23 Paulo akaikazia macho Sanhedrini, akasema: “Wanaume, akina ndugu, nimejiendesha mbele za Mungu kwa dhamiri+ iliyo safi kikamilifu mpaka leo hii.”
2 Ndipo kuhani mkuu Anania akawaagiza wale waliosimama kando yake wampige+ kinywani.
3 Ndipo Paulo akamwambia: “Mungu atakupiga wewe, ewe ukuta uliopakwa chokaa.+ Je, wakati uleule mmoja unaketi kunihukumu kupatana na Sheria+ na, kwa kuvunja Sheria,+ unaamuru nipigwe?”
4 Wale waliosimama kando wakasema: “Je, wewe unamtukana kuhani mkuu wa Mungu?”
5 Na Paulo akasema: “Akina ndugu, sikujua yeye ni kuhani mkuu. Kwa maana imeandikwa, ‘Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako.’ ”+
6 Sasa Paulo alipojua kwamba sehemu moja ilikuwa ya Masadukayo+ lakini ile nyingine ya Mafarisayo, akapaaza sauti katika Sanhedrini hiyo: “Wanaume, akina ndugu, mimi ni Farisayo,+ mwana wa Mafarisayo. Ninahukumiwa+ juu ya tumaini la ufufuo+ wa wafu.”
7 Kwa sababu alisema jambo hilo, mtengano+ ukatokea kati ya Mafarisayo na Masadukayo, na umati ukagawanyika.
8 Kwa maana Masadukayo+ husema hakuna ufufuo+ wala malaika wala roho, lakini Mafarisayo huyatangaza yote hadharani.
9 Kwa hiyo watu wakaanza kupiga mayowe+ kwa sauti kubwa, na wengine kati ya waandishi wa chama cha Mafarisayo wakasimama na kuanza kushindana vikali, wakisema: “Sisi hatuoni kosa lolote katika mtu huyu;+ lakini ikiwa roho au malaika alisema naye,+ —.”
10 Basi mtengano ulipokuwa mkubwa, kiongozi wa kijeshi akaogopa kwamba wangemrarua Paulo vipande-vipande, naye akaamuru jeshi la askari+ lishuke liende kumnyakua kutoka katikati yao na kumleta ndani ya makao ya askari-jeshi.+
11 Lakini usiku uliofuata Bwana akasimama kando yake+ na kusema: “Jipe moyo!+ Kwa maana kama vile ambavyo umekuwa ukitoa ushahidi+ kamili katika Yerusalemu juu ya mambo yanayonihusu, vivyo hivyo utatoa ushahidi katika Roma pia.”+
12 Sasa kulipokuwa mchana, Wayahudi wakafanya hila+ na kujifunga wenyewe kwa laana,+ wakisema hawangekula wala kunywa mpaka wawe wamemuua Paulo.+
13 Kulikuwa na zaidi ya watu 40 waliofanya hila hiyo iliyofungwa kwa kiapo;
14 nao wakaenda kwa wakuu+ wa makuhani na wanaume wazee na kusema: “Sisi tumejifunga wenyewe chini ya laana kwa uzito kutoonja chakula mpaka tuwe tumemuua Paulo.
15 Kwa hiyo, basi, ninyi pamoja na Sanhedrini mfanyeni kiongozi wa kijeshi aelewe ni kwa nini anapaswa kumshusha chini kwenu kana kwamba mnakusudia kuhakikisha kwa usahihi zaidi mambo yanayomhusu.+ Lakini kabla hajafika karibu tutakuwa tayari kumuua.”+
16 Hata hivyo, mwana wa dada ya Paulo akasikia juu ya kuvizia kwao,+ naye akaja na kuingia katika makao ya askari-jeshi hao akamweleza Paulo jambo hilo.
17 Basi Paulo akamwita mmoja wa maofisa-jeshi na kusema: “Mpeleke kijana huyu kwa kiongozi wa kijeshi, kwa maana ana jambo fulani la kumweleza.”
18 Kwa hiyo mtu huyu akamchukua na kumpeleka kwa kiongozi wa kijeshi na kusema: “Mfungwa Paulo aliniita na kuniomba nimlete kijana huyu kwako, kwa kuwa ana jambo la kukuambia.”
19 Kiongozi wa kijeshi akamshika+ mkono, akaondoka, na kuanza kumuuliza faraghani: “Unataka kuniambia nini?”
20 Akasema: “Wayahudi wamepatana kukuomba umshushe Paulo kwenye Sanhedrini kesho kana kwamba wanakusudia kujua jambo fulani kwa usahihi zaidi juu yake.+
21 Zaidi ya mambo yote, usiwaache wakushawishi, kwa maana wanaume wao zaidi ya 40 wanamvizia,+ nao wamejifunga wenyewe kwa laana kutokula wala kunywa mpaka wawe wamemuua;+ nao sasa wako tayari, wakingojea ahadi kutoka kwako.”
22 Kwa hiyo huyo kiongozi wa kijeshi akamwacha huyo kijana aende baada ya kumwagiza: “Usipayuke-payuke kwa yeyote kwamba umenieleza mambo hayo.”
23 Naye akawaita watu fulani wawili kati ya maofisa-jeshi na kusema: “Tayarisheni askari-jeshi 200 ili waende moja kwa moja mpaka Kaisaria, pia wapanda-farasi 70 na watu 200 wachukua-mikuki, saa tatu ya usiku.
24 Pia, andaeni wanyama wa kubeba mizigo ili wampandishe Paulo na kumpeleka salama kwa Feliksi gavana.”
25 Naye akaandika barua ya namna hii:
26 “Klaudio Lisia kwa mtukufu, Gavana Feliksi:+ Salamu!
27 Mwanamume huyu alikamatwa na Wayahudi nao walikuwa karibu kumuua, lakini nikaja ghafula nikiwa pamoja na jeshi la askari na kumwokoa,+ kwa sababu nilipata kujua kwamba yeye ni Mroma.+
28 Nami nikitaka kuhakikisha sababu waliyokuwa wakimshtakia, nikamleta ndani ya Sanhedrini yao.+
29 Niliona ameshtakiwa juu ya maswali ya Sheria yao,+ lakini hajashtakiwa hata jambo moja la kustahili kifo au vifungo.+
30 Lakini kwa sababu hila+ itakayofanywa juu ya mwanamume huyu imefunuliwa kwangu, ninamtuma kwako mara moja, na kuwaamuru washtaki wamshtaki mbele yako.”+
31 Kwa hiyo askari-jeshi+ hao wakamchukua Paulo kulingana na walivyoagizwa wakamleta wakati wa usiku mpaka Antipatri.
32 Siku iliyofuata wakaruhusu wapanda-farasi waende pamoja naye, nao wakarudi kwenye makao ya askari-jeshi.
33 Hao wapanda-farasi wakaingia katika Kaisaria+ na kumkabidhi gavana hiyo barua na pia wakamleta Paulo mbele yake.
34 Basi akaisoma na kuuliza alikuwa ametoka jimbo gani, akapata kujua hakika+ kwamba alikuwa ametoka Kilikia.+
35 “Nitasikia kesi yako vilivyo,” akasema, “washtaki wako watakapofika pia.”+ Naye akaamuru kwamba awekwe chini ya ulinzi katika jumba la kimaliki la Herode.