Matendo 13:1-52

13  Basi katika Antiokia kulikuwa na manabii+ na walimu katika kutaniko la mahali hapo, Barnaba na vilevile Simioni aliyeitwa Nigeri, na Lukio+ wa Kirene, na Manaeni aliyeelimishwa pamoja na Herode mtawala wa wilaya, na Sauli.  Walipokuwa wakimhudumia+ Yehova hadharani na kufunga, roho takatifu ikasema: “Kati ya watu wote wekeni kando Barnaba na Sauli+ kwa ajili yangu kwa kazi ambayo nimewaitia wao.”  Ndipo wakafunga na kusali na kuweka mikono+ yao juu yao, wakawaacha waende zao.  Basi watu hawa, waliotumwa na roho takatifu, wakashuka kwenda Seleukia, na kutoka huko wakasafiri kwa mashua kwenda Kipro.  Na walipofika Salami wakaanza kulitangaza neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa na Yohana+ akiwatumikia.  Walipokuwa wamepita katika kisiwa chote mpaka Pafo, wakakutana na mwanamume fulani, mlozi, nabii wa uwongo,+ Myahudi ambaye jina lake lilikuwa Bar-Yesu,  naye alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mwanamume mwenye akili. Akawaita Barnaba na Sauli, naye mtu huyu akataka kulisikia neno la Mungu.  Lakini Elima mlozi (hivyo, kwa kweli, ndivyo jina lake linavyotafsiriwa) akaanza kuwapinga,+ akitafuta kumgeuzia mbali yule liwali kutoka kwenye ile imani.  Sauli, ambaye pia ni Paulo, akiwa amejaa roho takatifu, akamtazama 10  na kusema: “Ewe mtu mwenye kujaa kila namna ya upunjaji na kila namna ya ulaghai, wewe mwana wa Ibilisi, wewe adui wa kila jambo la uadilifu, je, hutaacha kuzipotoa njia zilizo sawa za Yehova?+ 11  Hivyo, basi, tazama! mkono wa Yehova uko juu yako wewe, nawe utakuwa kipofu, usiweze kuiona nuru ya jua kwa kipindi fulani.” Mara moja ukungu mzito na giza vikamwangukia, naye akazunguka akitafuta watu wa kumwongoza wakiwa wamemshika mkono.+ 12  Ndipo yule liwali,+ alipoona jambo lililokuwa limetukia, akawa mwamini, kwa kuwa alistaajabishwa na fundisho la Yehova. 13  Hao watu, pamoja na Paulo, sasa wakasafiri baharini kutoka Pafo na kufika Perga katika Pamfilia.+ Lakini Yohana+ akawaacha na kurudi+ Yerusalemu. 14  Hata hivyo, wao wakaendelea kutoka Perga na kuja Antiokia katika Pisidia nao wakaingia ndani ya sinagogi+ siku ya sabato, wakaketi. 15  Baada ya kusoma Sheria+ na Manabii mbele ya watu wote maofisa-wasimamizi+ wa sinagogi wakawatuma watu kwao, wakisema: “Wanaume, akina ndugu, ikiwa kuna neno lolote la kitia moyo mlilo nalo kwa ajili ya watu, lisemeni.” 16  Kwa hiyo Paulo akasimama, akapunga+ mkono wake, akasema: “Wanaume, Waisraeli na ninyi wengine ambao mnamwogopa Mungu, sikieni.+ 17  Mungu wa watu hawa Israeli aliwachagua mababu zetu, naye akawainua watu hao walipokuwa wakikaa katika nchi ya kigeni katika nchi ya Misri na kuwatoa katika hiyo kwa mkono ulioinuliwa.+ 18  Na kwa kipindi cha karibu miaka 40+ akavumilia jinsi walivyotenda nyikani. 19  Baada ya kuyaangamiza mataifa saba katika nchi ya Kanaani, aligawanya nchi yao kwa kura:+ 20  yote haya wakati wa karibu miaka 450. “Na baada ya mambo hayo aliwapa waamuzi mpaka nabii Samweli.+ 21  Lakini tangu hapo na kuendelea wakadai mfalme,+ na Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mwanamume wa kabila la Benyamini,+ kwa miaka 40. 22  Na baada ya kumwondoa huyo,+ akawainulia Daudi kuwa mfalme,+ ambaye alitoa ushahidi kumhusu na kusema, ‘Nimemwona Daudi mwana wa Yese,+ mtu anayekubalika kwa moyo wangu,+ atakayefanya mambo yote ambayo ninatamani.’+ 23  Kutoka katika uzao+ wa mwanamume huyu kulingana na ahadi yake Mungu ameletea Israeli mwokozi,+ Yesu, 24  baada ya Yohana,+ kabla ya kuingia kwake Huyo,+ akiwa amekwisha kuhubiri hadharani kwa watu wote wa Israeli ubatizo unaoonyesha toba. 25  Lakini Yohana alipokuwa akitimiza mwendo wake, akawa akisema ‘Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yeye. Lakini, tazameni! mmoja anakuja baada yangu ambaye viatu vya miguu yake mimi sistahili kuvifungua.’+ 26  “Wanaume, akina ndugu, ninyi wana wa ukoo wa Abrahamu na wale wengine kati yenu ambao mnamwogopa Mungu, neno la wokovu huu limeletwa kwetu sisi.+ 27  Kwa maana wakaaji wa Yerusalemu na watawala wao hawakumjua Huyu,+ bali, walipokuwa wakitenda wakiwa waamuzi, walitimiza mambo yaliyosemwa na Manabii,+ mambo ambayo husomwa kwa sauti kubwa kila Sabato, 28  na, ijapokuwa hawakupata sababu yoyote ya kumuua+ walidai kwa Pilato kwamba auawe.+ 29  Basi, walipokuwa wametimiza mambo yote yaliyoandikwa juu yake,+ walimshusha chini kutoka kwenye mti+ na kumlaza katika kaburi.+ 30  Lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu;+ 31  na kwa siku nyingi akaonekana kwa wale ambao walikuwa wamepanda kwenda pamoja naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu, ambao sasa ni mashahidi wake kwa watu.+ 32  “Na kwa hiyo sisi tunawatangazia ninyi habari njema juu ya ahadi iliyotolewa kwa mababu,+ 33  kwamba Mungu ameitimiza kabisa kwetu sisi tulio watoto wao kwa kuwa alimfufua Yesu;+ hata kama vile ambavyo imeandikwa katika zaburi ya pili, ‘Wewe ni mwanangu, mimi nimekuwa Baba yako leo.’+ 34  Na jambo hilo la kwamba yeye alimfufua kutoka kwa wafu akikusudiwa asirudi tena kwenye uharibifu, yeye amelisema katika njia hii, ‘Nitawapa ninyi fadhili zenye upendo kwa Daudi ambazo ni za uaminifu.’+ 35  Kwa sababu hiyo anasema pia katika zaburi nyingine, ‘Hutamruhusu mshikamanifu wako aone uharibifu.’+ 36  Kwa maana Daudi,+ kwa upande mmoja, alitumikia mapenzi kamili ya Mungu katika kizazi chake mwenyewe na kulala katika kifo na alilazwa pamoja na mababu zake na kuona uharibifu.+ 37  Kwa upande mwingine, yule ambaye Mungu alimfufua hakuona uharibifu.+ 38  “Kwa hiyo acheni ijulikane kwenu, akina ndugu, kwamba kupitia Huyo msamaha wa dhambi unatangazwa kwenu;+ 39  na kwamba kutokana na mambo yote ambayo ninyi hamngeweza kutangazwa kuwa bila hatia kwa njia ya sheria ya Musa,+ kila mtu anayeamini anatangazwa kuwa bila hatia kwa njia ya Huyu.+ 40  Kwa hiyo hakikisheni kwamba yale yaliyosemwa katika Manabii hayaji juu yenu, 41  ‘Oneni, ninyi wenye kudharau, mstaajabie, na mtoweke, kwa sababu ninafanya tendo katika siku zenu, tendo ambalo hamtaliamini hata kidogo hata yeyote akiwaeleza kirefu.’ ”+ 42  Basi walipokuwa wakitoka, watu wakaanza kusihi waambiwe mambo hayo siku ya sabato inayofuata.+ 43  Kusanyiko la sinagogi lilipomalizika, wengi kati ya Wayahudi na kati ya wageuzwa-imani waliomwabudu Mungu wakawafuata Paulo na Barnaba,+ ambao walisema nao na kuanza kuwahimiza+ waendelee kubaki katika fadhili zisizostahiliwa za Mungu.+ 44  Siku ya Sabato iliyofuata karibu jiji lote lilikusanyika pamoja kulisikia neno la Yehova.+ 45  Wayahudi walipoona umati, walijawa na wivu+ na kuanza kuyapinga kwa kukufuru mambo yaliyokuwa yakisemwa na Paulo.+ 46  Na kwa hiyo, wakiongea kwa ujasiri, Paulo na Barnaba wakasema: “Ilikuwa lazima neno la Mungu lihubiriwe kwenu kwanza.+ Kwa kuwa mnalisukumia mbali+ kutoka kwenu na hamjioni kuwa mnastahili uzima wa milele, tazameni! tunawageukia mataifa.+ 47  Kwa kweli, Yehova ameweka amri juu yetu kwa maneno haya, ‘Nimewaweka ninyi kuwa nuru ya mataifa,+ ili muwe wokovu mpaka sehemu ya mwisho ya dunia.’ ”+ 48  Wale wa mataifa waliposikia jambo hilo, wakaanza kushangilia na kulitukuza neno la Yehova,+ na wale wote waliokuwa na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele wakawa waamini.+ 49  Zaidi ya hayo, neno la Yehova likaendelea kupelekwa kotekote katika nchi yote.+ 50  Lakini Wayahudi+ wakawachochea wanawake wenye kusifika waliomwabudu Mungu na wakuu wa jiji, nao wakazusha mateso+ juu ya Paulo na Barnaba na kuwatupa nje ya mipaka yao. 51  Hawa wakawakung’utia mavumbi kutoka miguuni pao+ na kwenda Ikoniamu. 52  Na wanafunzi wakaendelea kujawa na shangwe+ na roho takatifu.

Maelezo ya Chini