Matendo 21:1-40

21  Sasa tulipokuwa tumejiondoa kwao na kusafiri baharini, tulikwenda kwa mwendo wa moja kwa moja tukaja mpaka Kosi, lakini siku iliyofuata tukaja mpaka Rode, na kutoka huko mpaka Patara.  Na tulipokuwa tumepata mashua iliyokuwa ikivuka kwenda Foinike, tukapanda ndani, tukasafiri kwenda zetu.  Baada ya kuja mahali tulipoweza kuona kisiwa cha Kipro+ tukakiacha nyuma upande wa kushoto, tukasafiri mpaka Siria,+ tukafika Tiro, kwa maana mashua ilipaswa ipakue shehena yake huko.+  Baada ya kuwatafuta, tuliwapata wanafunzi na kukaa huko siku saba. Lakini kupitia roho+ wakarudiarudia kumwambia Paulo asikanyage Yerusalemu.  Kwa hiyo tulipokuwa tumekamilisha hizo siku, tukatoka na kuanza kwenda; lakini hao wote, pamoja na wanawake na watoto, wakatupeleka mpaka nje ya jiji. Tukapiga magoti+ pwani, tukasali  na kuagana,+ nasi tukapanda ndani ya mashua lakini wao wakarudi nyumbani kwao.  Ndipo tukakamilisha safari ya baharini kutoka Tiro tukafika Tolemai, nasi tukawasalimu akina ndugu na kukaa siku moja pamoja nao.  Siku iliyofuata tukaondoka tukafika Kaisaria,+ nasi tukaingia katika nyumba ya Filipo mweneza-injili, aliyekuwa mmoja wa wale watu saba,+ nasi tukakaa pamoja naye.  Mtu huyu alikuwa na binti wanne, mabikira, waliotoa unabii.+ 10  Lakini tulipokuwa tukikaa siku kadhaa, nabii fulani anayeitwa Agabo+ akashuka kutoka Yudea, 11  naye akaja mahali tulipokuwa na kuuchukua mshipi wa Paulo, akafunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema: “Hivi ndivyo inavyosema roho takatifu, ‘Mwanamume ambaye mshipi huu ni wake, Wayahudi watamfunga+ hivi katika Yerusalemu na kumtia+ mikononi mwa watu wa mataifa.’ ” 12  Sasa tuliposikia jambo hilo, sisi na pia watu wa mahali hapo tukaanza kumsihi asipande+ kwenda Yerusalemu. 13  Ndipo Paulo akajibu: “Mnafanya nini kwa kulia+ na kunifanya dhaifu moyoni?+ Muwe na hakika, niko tayari si kufungwa tu bali pia kufa+ Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.” 14  Alipokataa kushawishika, tukakubali kimyakimya maneno haya: “Mapenzi+ ya Yehova na yatendeke.” 15  Sasa baada ya siku hizo tukajitayarisha kwa ajili ya safari, tukaanza kupanda kwenda Yerusalemu.+ 16  Lakini wengine kati ya wanafunzi kutoka Kaisaria+ wakaenda pamoja nasi pia, ili kutuleta kwa mtu ambaye nyumbani mwake tulipaswa kukaribishwa, Mnasoni wa Kipro, mwanafunzi wa zamani. 17  Tulipoingia Yerusalemu,+ akina ndugu wakatukaribisha kwa furaha.+ 18  Lakini siku iliyofuata Paulo akaingia pamoja nasi kwa Yakobo;+ na wanaume wote wazee walikuwapo. 19  Naye akawasalimu na kuanza kusimulia+ kirefu juu ya mambo ambayo Mungu alifanya katikati ya mataifa kupitia kwa huduma yake.+ 20  Baada ya kusikia jambo hilo wakaanza kumtukuza Mungu, nao wakamwambia: “Unaona, ndugu, jinsi kulivyo na maelfu mengi ya waamini walio kati ya Wayahudi; nao wote ni wenye bidii kuhusu Sheria.+ 21  Lakini wamesikia uvumi ukitolewa juu yako kwamba wewe umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wote kati ya mataifa uasi-imani wa kumwacha Musa,+ ukiwaambia wasiwatahiri+ watoto wao wala kujiendesha katika desturi za kisherehe. 22  Basi, ni nini kinachopaswa kufanywa juu ya hilo? Kwa vyovyote vile watasikia umefika. 23  Kwa hiyo fanya jambo hili tunalokuambia: Tuna wanaume wanne wenye nadhiri juu yao wenyewe. 24  Wachukue watu hawa pamoja nawe+ ujitakase kisherehe pamoja nao na kuwagharimia,+ ili wapate kunyolewa+ vichwa vyao. Na kwa hiyo kila mtu atajua kwamba uvumi mwingi walioambiwa juu yako si kitu, bali kwamba unatembea kwa utaratibu, wewe mwenyewe pia ukishika Sheria.+ 25  Kwa habari ya wale waamini kutoka kati ya mataifa, tumetuma watu, tukitoa uamuzi wetu kwamba wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu+ na pia damu+ na vitu vilivyonyongwa,+ na uasherati.”+ 26  Ndipo Paulo akawachukua wanaume hao pamoja naye siku iliyofuata akajitakasa kisherehe pamoja nao+ na kuingia ndani ya hekalu, kutoa taarifa juu ya siku ambazo zingetimizwa+ kwa huo utakaso wa kisherehe, mpaka toleo+ litolewe kwa ajili ya kila mmoja wao.+ 27  Sasa zile siku saba+ zilipokuwa karibu kumalizika, Wayahudi kutoka Asia walipomwona katika hekalu wakaanza kuuvuruga umati wote,+ nao wakamkamata, 28  wakipaaza sauti: “Wanaume wa Israeli, saidieni! Huyu ndiye mwanamume anayefundisha kila mtu kila mahali dhidi ya watu+ na Sheria na mahali hapa na, zaidi ya hayo, hata aliwaingiza Wagiriki katika hekalu naye amepatia unajisi mahali hapa patakatifu.”+ 29  Kwa maana hapo kwanza walikuwa wamemwona Trofimo+ Mwefeso katika jiji akiwa pamoja naye, lakini walikuwa wakiwazia Paulo alikuwa amemwingiza katika hekalu. 30  Na jiji lote likawa na mchafuko,+ na watu wakaanza kukimbia pamoja; nao wakamkamata Paulo wakamkokota nje ya hekalu.+ Na mara moja milango ikafungwa. 31  Na walipokuwa wakitafuta kumuua, kiongozi wa kikosi cha askari-jeshi akaletewa habari kwamba Yerusalemu lote lilikuwa katika mvurugo;+ 32  naye mara moja akachukua askari-jeshi na maofisa-jeshi na kuwakimbilia huko chini.+ Walipomwona kiongozi huyo wa kijeshi+ na askari-jeshi, wakaacha kumpiga Paulo. 33  Ndipo kiongozi wa kijeshi akaja karibu akamkamata na kutoa amri afungwe minyororo miwili;+ naye akaanza kuuliza huyo ni nani na alikuwa amefanya nini. 34  Lakini wengine katika umati wakaanza kupaaza sauti kuhusu jambo moja, na wengine kuhusu lingine.+ Kwa hiyo, kwa kuwa hangeweza kujua jambo lolote la hakika kwa sababu ya fujo hizo, akaamuru aletwe kwenye makao ya askari-jeshi.+ 35  Lakini alipofika juu ya ngazi, akachukuliwa na wale askari-jeshi kwa sababu ya jeuri ya umati; 36  kwa maana umati wa watu uliendelea kufuata, ukipaaza sauti: “Mwondolee mbali!”+ 37  Na alipokuwa karibu kuingizwa katika makao ya askari-jeshi, Paulo akamwambia kiongozi wa kijeshi: “Je, ninaruhusiwa kukuambia jambo fulani?” Akasema: “Je, unaweza kusema Kigiriki? 38  Je, kwa kweli wewe si yule Mmisri ambaye kabla ya siku hizi alichochea uasi+ na kuwaongoza kuingia nyikani wale wanaume elfu nne wenye kutumia visu?” 39  Ndipo Paulo akasema: “Mimi, kwa kweli, ni Myahudi+ wa Tarso+ katika Kilikia, raia wa jiji ambalo si lenye kukosa umashuhuri. Kwa hiyo ninakuomba, uniruhusu niseme na watu hawa.” 40  Baada ya kutoa ruhusa, Paulo, akiwa amesimama juu ya ngazi, akawapungia+ watu mkono wake. Kulipokuwa na kimya kikubwa, akawahutubia kwa lugha ya Kiebrania,+ akisema:

Maelezo ya Chini