Matendo 26:1-32
26 Agripa+ akamwambia Paulo: “Unaruhusiwa kujitetea.” Ndipo Paulo akanyoosha mkono+ wake na kuanza kujitetea:+
2 “Kuhusu mambo yote ninayoshtakiwa+ na Wayahudi, Mfalme Agripa, ninajihesabu mwenyewe kuwa mwenye furaha kwamba ninajitetea mbele yako leo,
3 hasa kwa kuwa wewe una ujuzi juu ya desturi+ zote na vilevile mabishano kati ya Wayahudi. Kwa hiyo ninakuomba unisikie kwa subira.
4 “Kwa kweli, juu ya maisha+ ya tangu ujana na kuendelea ambayo niliishi tangu mwanzo kati ya taifa langu na katika Yerusalemu, Wayahudi wote
5 ambao walinifahamu tangu mwanzo wanajua, kama tu wangetaka kutoa ushahidi, kwamba kulingana na usahihi kabisa wa madhehebu+ ya namna yetu ya ibada mimi niliishi nikiwa Farisayo.+
6 Lakini sasa kwa sababu ya tumaini+ la ahadi+ iliyotolewa na Mungu kwa mababu zetu nimeitwa kwenye hukumu;
7 lakini makabila yetu kumi na mawili yanatumaini kufikia utimizo wa ahadi hii kwa kumtolea utumishi mtakatifu kwa juhudi nyingi usiku na mchana.+ Kuhusu tumaini hili ninashtakiwa+ na Wayahudi, Ewe mfalme.
8 “Kwa nini mnaamua kwamba ni jambo lisiloaminika kwamba Mungu hufufua wafu?+
9 Mimi, kwa kweli nilifikiri ndani yangu mwenyewe kwamba ninapaswa kufanya matendo mengi ya upinzani juu ya jina la Yesu Mnazareti;
10 ambayo, kwa kweli, niliyafanya katika Yerusalemu, na wengi kati ya watakatifu niliwafunga gerezani,+ kwa kuwa nilikuwa nimepokea mamlaka kutoka kwa wakuu wa makuhani;+ na walipokuwa wanapaswa kuuawa, mimi nilipiga kura yangu dhidi yao.
11 Na kwa kuwaadhibu nyakati nyingi katika masinagogi+ yote nilijaribu kuwalazimisha wakane imani yao; na kwa kuwa nilikuwa nimejawa na wazimu kupita kiasi juu yao, nilifikia hatua ya kuwatesa hata katika majiji ya nje.
12 “Katikati ya jitihada hizo nilipokuwa nikisafiri kwenda Damasko+ nikiwa na mamlaka na utume kutoka kwa wakuu wa makuhani,
13 katikati ya mchana niliona barabarani, Ee mfalme, nuru inayopita wangavu wa jua ikimulika kutoka mbinguni kunizunguka na kuwazunguka wale waliokuwa wakisafiri pamoja nami.+
14 Na sisi sote tulipokuwa tumeanguka chini nikasikia sauti ikiniambia katika lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, kwa nini unanitesa? Kuendelea kuipiga teke michokoo hufanya iwe vigumu kwako.’+
15 Lakini nikasema, ‘Wewe ni nani, Bwana?’ Naye Bwana akasema, ‘Mimi ni Yesu, ambaye unatesa.+
16 Hata hivyo, inuka usimame kwa miguu yako.+ Kwa maana nimejionyesha kwako kwa sababu hii, ili nikuchague wewe uwe mtumishi na shahidi+ wa mambo ambayo umeona na pia mambo nitakayokuonyesha juu yangu;
17 huku mimi nikikukomboa kutoka kwa watu hawa na kutoka katika mataifa, ambao kwao ninakutuma wewe,+
18 kufungua macho+ yao, kuwageuza kutoka katika giza+ kuingia katika nuru+ na kutoka katika mamlaka ya Shetani+ na kumgeukia Mungu, kusudi wapokee msamaha wa dhambi+ na urithi+ kati ya wale waliotakaswa+ kwa imani yao kwangu.’
19 “Kwa sababu hii, Mfalme Agripa, mimi sikukosa kutii maono hayo ya kimbingu,+
20 lakini kwa wale walio katika Damasko+ kwanza na pia kwa wale walio katika Yerusalemu,+ na juu ya nchi yote ya Yudea, na kwa mataifa+ nilienda nikiuleta ujumbe kwamba wao wanapaswa kutubu na kumgeukia Mungu kwa kufanya matendo yanayostahili toba.+
21 Kwa sababu ya mambo haya Wayahudi walinikamata katika hekalu na kujaribu kuniua.+
22 Hata hivyo, kwa sababu nimeupata msaada+ kutoka kwa Mungu ninaendelea mpaka leo kutoa ushahidi kwa wadogo na wakubwa pia, lakini bila kusema lolote ila mambo ambayo Manabii+ na vilevile Musa+ walisema yatatukia,
23 kwamba Kristo angeteseka+ na, akiwa wa kwanza kufufuliwa+ kutoka kwa wafu, angetangaza nuru+ kwa watu hawa na pia kwa mataifa.”+
24 Sasa alipokuwa akisema mambo haya kwa kujitetea, Festo akasema kwa sauti kubwa: “Unashikwa na wazimu,+ Paulo! Kusoma kwingi kunakufanya uwe na wazimu!”
25 Lakini Paulo akasema: “Mimi sishikwi na wazimu, ewe Mtukufu Festo, bali ninasema maneno ya kweli na ya utimamu wa akili.
26 Kwa kweli, mfalme ambaye ninasema naye kwa uhuru wa kusema anajua vema juu ya mambo haya; kwa maana ninasadiki kwamba hakuna hata moja kati ya mambo haya ambalo hajui, kwa maana jambo hili halijafanywa pembeni.+
27 Je, wewe, Mfalme Agripa, unawaamini Manabii? Ninajua unawaamini.”+
28 Lakini Agripa akamwambia Paulo: “Kwa muda mfupi ungenishawishi niwe Mkristo.”
29 Ndipo Paulo akasema: “Kama ingekuwa kwa muda mfupi au kwa muda mrefu mimi ningetaka kwa Mungu kwamba si wewe tu bali pia wote wanaonisikia leo wapate kuwa watu wa namna niliyo mimi, ila tu bila vifungo hivi.”
30 Naye mfalme akasimama na pia gavana na Bernike na watu walioketi pamoja nao.
31 Lakini walipokuwa wakiondoka wakaanza kuongea wao kwa wao, wakisema: “Mtu huyu hafanyi lolote linalostahili kifo+ au vifungo.”
32 Zaidi ya hayo, Agripa akamwambia Festo: “Mtu huyu angaliweza kufunguliwa kama hakuwa amekata rufani+ kwa Kaisari.”