Matendo 14:1-28
14 Basi katika Ikoniamu+ wakaingia pamoja katika sinagogi+ la Wayahudi na kusema kwa namna ambayo iliufanya umati mkubwa wa Wayahudi na pia Wagiriki+ kuwa waamini.
2 Lakini Wayahudi ambao hawakuamini wakachochea+ na kuwa na uvutano mbaya juu ya nafsi za watu wa mataifa dhidi ya akina ndugu.+
3 Kwa hiyo wakatumia muda mrefu wakisema kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova, aliyetoa ushahidi kuhusu neno la fadhili zake zisizostahiliwa kwa kuruhusu ishara na mambo ya ajabu kutukia kupitia kwa mikono yao.+
4 Hata hivyo, umati wa jiji ukagawanyika, na baadhi yao walikuwa upande wa Wayahudi lakini wengine upande wa mitume.
5 Basi watu wa mataifa na pia Wayahudi pamoja na watawala wao walipojaribu kwa jeuri kuwatendea kwa dharau na kuwatupia mawe,+
6 wao, walipojulishwa jambo hilo, wakakimbilia+ majiji ya Likaonia, Listra na Derbe na nchi yenye kuzunguka;
7 na huko wakaendelea kutangaza habari njema.+
8 Sasa katika Listra mwanamume fulani aliyekuwa amelemaa miguu alikuwa ameketi, kilema tangu alipokuwa katika tumbo la uzazi la mama yake,+ naye alikuwa hajatembea kamwe.
9 Mtu huyo alikuwa akimsikiliza Paulo akisema, ambaye, alipomtazama na kuona kwamba ana imani+ ya kuponywa,
10 akasema kwa sauti kubwa: “Simama wima kwa miguu yako.” Naye akaruka na kuanza kutembea.+
11 Na umati, walipoona jambo ambalo Paulo alikuwa amefanya, wakapaaza sauti, wakisema katika lugha ya Kilikaonia: “Miungu+ imekuwa kama binadamu nayo imeshuka kwetu!”
12 Naye Barnaba wakamwita Zeu, lakini Paulo wakamwita Herme, kwa kuwa ndiye aliyekuwa akiongoza katika kusema.
13 Na kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya jiji, akaleta ng’ombe-dume na shada za maua kwenye malango naye alikuwa anataka kutoa dhabihu+ pamoja na umati.
14 Hata hivyo, mitume Barnaba na Paulo waliposikia jambo hilo, wakayararua mavazi yao ya nje na kuruka ndani ya umati, wakipaaza sauti
15 na kusema: “Wanaume, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu+ tulio na udhaifu+ uleule kama ninyi, nasi tunawatangazia ninyi habari njema, ili mgeuke kutoka kwa mambo haya ya bure+ mpate kumjia Mungu aliye hai,+ aliyefanya mbingu+ na dunia na bahari na vitu vyote vilivyomo.
16 Katika vizazi vilivyopita yeye aliwaruhusu mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao,+
17 ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema,+ akiwapa ninyi mvua+ kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.”+
18 Na bado kwa kusema mambo haya wakauzuia umati kwa shida, wasiwatolee dhabihu.
19 Lakini Wayahudi wakafika kutoka Antiokia na Ikoniamu wakaushawishi umati,+ nao wakampiga Paulo kwa mawe na kumkokota nje ya jiji, wakiwazia alikuwa amekufa.+
20 Hata hivyo, wanafunzi walipomzunguka, akasimama na kuingia ndani ya jiji. Na siku iliyofuata akaondoka pamoja na Barnaba kwenda Derbe.+
21 Na baada ya kulitangazia jiji hilo habari njema na kufanya wanafunzi+ wengi, wakarudi Listra na Ikoniamu na Antiokia,
22 wakizitia nguvu nafsi za wanafunzi,+ wakiwatia moyo kubaki katika imani na kusema: “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kupitia dhiki nyingi.”+
23 Zaidi ya hayo, wakawaweka rasmi wanaume wazee+ kwa ajili yao katika kila kutaniko, wakatoa sala pamoja na kufunga,+ na kuwakabidhi kwa Yehova+ ambaye walikuwa wamemwamini.
24 Nao wakapita katika Pisidia na kuingia Pamfilia,+
25 na, baada ya kulisema neno katika Perga, wakashuka kwenda Atalia.
26 Na kutoka huko wakasafiri kwenda Antiokia,+ walikokuwa wamekabidhiwa kwenye fadhili zisizostahiliwa za Mungu kwa ajili ya kazi waliyokuwa wameifanya kikamili.+
27 Walipokuwa wamefika na wakiwa wamelikusanya kutaniko pamoja, wakaeleza mambo mengi+ ambayo Mungu alikuwa amefanya kupitia kwao, na kwamba alikuwa amewafungulia mataifa mlango wa kuingia katika imani.+
28 Kwa hiyo wakatumia muda usio mdogo wakiwa pamoja na wanafunzi.