Matendo 10:1-48

10  Sasa katika Kaisaria kulikuwa na mwanamume fulani aliyeitwa jina Kornelio, ofisa-jeshi+ wa kikosi+ cha Italia, kama kilivyokuwa kikiitwa,  mtu mwenye kuheshimu+ na kumwogopa+ Mungu pamoja na watu wote wa nyumba yake, naye aliwapa watu+ zawadi nyingi za rehema na kuomba dua kwa Mungu sikuzote.+  Karibu tu na saa tisa+ ya mchana akaona wazi katika maono+ malaika+ wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”  Mtu huyo akamtazama na, akiogopa, akasema: “Ni nini, Bwana?” Akamwambia: “Sala+ na zawadi zako za rehema zimepanda kama ukumbusho mbele za Mungu.+  Kwa hiyo sasa tuma watu Yopa ukamwite Simoni anayeitwa Petro.  Mtu huyu ni mgeni wa Simoni, mtengenezaji wa ngozi, aliye na nyumba kando ya bahari.”+  Mara tu malaika aliyesema naye alipokuwa ameondoka, akawaita wawili kati ya watumishi wake wa nyumbani na askari-jeshi mwenye kumwogopa Mungu kutoka kati ya wale waliokuwa wakimhudumia daima,+  naye akawasimulia kila kitu na kuwatuma kwenda Yopa.+  Siku iliyofuata walipokuwa wakiendelea na safari yao na wakikaribia jiji hilo, Petro akapanda juu ya paa+ ya nyumba karibu saa sita ili kusali.+ 10  Lakini akaona njaa sana naye akataka kula. Walipokuwa wakitayarisha, akapata njozi+ 11  naye akaona mbingu imefunguliwa+ na chombo cha namna fulani kikishuka kama shuka kubwa la kitani, kikishushwa juu ya dunia kwa ncha zake nne; 12  na ndani yake mlikuwa namna zote za viumbe wenye miguu minne na vitu vinavyotambaa vya dunia na ndege wa mbinguni.+ 13  Na sauti ikamjia: “Simama, Petro, chinja ule!”+ 14  Lakini Petro akasema: “Sivyo hata kidogo, Bwana, kwa sababu sijakula kamwe kitu chochote kilichotiwa unajisi na kisicho safi.”+ 15  Na sauti ikasema tena naye, mara ya pili: “Wewe acha kuviita najisi+ vitu ambavyo Mungu ametakasa.” 16  Jambo hilo likatokea mara ya tatu, na mara hiyo kile chombo kikachukuliwa juu mbinguni.+ 17  Basi Petro alipokuwa amefadhaika sana ndani yake juu ya maana ya maono aliyokuwa ameona, tazama! wale watu waliotumwa na Kornelio walikuwa wameuliza kuhusu nyumba ya Simoni na walikuwa wamesimama hapo langoni.+ 18  Nao wakapaaza sauti na kuuliza kama Simoni anayeitwa Petro alikuwa mgeni humo. 19  Petro alipokuwa akiwaza akilini mwake kuhusu yale maono, roho+ ikasema: “Tazama! Wanaume watatu wanakutafuta. 20  Hata hivyo, simama, ushuke na kwenda pamoja nao, nawe usiwe na shaka hata kidogo, kwa sababu nimewatuma.”+ 21  Kwa hiyo Petro akashuka kutoka ghorofani mpaka kwa wanaume hao na kusema: “Tazameni! Mimi ndiye mnayetafuta. Kwa nini mko hapa?” 22  Wakasema: “Kornelio, ofisa-jeshi, mwanamume mwadilifu na mwenye kumwogopa Mungu+ na mwenye sifa njema+ katika taifa lote la Wayahudi, malaika mtakatifu alimpa maagizo ya Mungu kwamba atume watu ili uitwe uje nyumbani kwake apate kuyasikia mambo utakayosema.” 23  Kwa hiyo akawakaribisha na kuwapa makao. Siku iliyofuata akaondoka na kwenda pamoja nao, na baadhi ya akina ndugu waliokuwa wametoka Yopa wakaenda pamoja naye. 24  Siku ya pili yake akaingia Kaisaria. Bila shaka, Kornelio alikuwa akiwatarajia naye alikuwa amewaita pamoja jamaa zake na rafiki zake wa karibu sana. 25  Petro alipokuwa akiingia, Kornelio akakutana naye, akaanguka chini miguuni pake na kumsujudia. 26  Lakini Petro akamwinua, akisema: “Simama; mimi pia ni mwanadamu.”+ 27  Naye alipokuwa akiongea naye akaingia na kuwakuta watu wengi wakiwa wamekusanyika, 28  naye akawaambia: “Ninyi mnajua jinsi ilivyo kinyume cha sheria kwa Myahudi kujiunga na mtu wa jamii nyingine au kumkaribia;+ na bado Mungu amenionyesha sipaswi kumwita mtu yeyote kuwa najisi au si safi.+ 29  Kwa sababu hiyo nikaja, kwa kweli bila kupinga, nilipoitwa nije. Kwa hiyo ninawauliza ninyi ni sababu gani mliyoniitia.” 30  Basi Kornelio akasema: “Siku nne zilizopita kutoka saa hii nilikuwa nikisali katika nyumba yangu saa tisa,+ wakati, tazama! mwanamume aliyekuwa amevaa vazi linalong’aa+ alisimama mbele yangu 31  na kusema, ‘Kornelio, sala yako imesikiwa na kukubaliwa, nazo zawadi zako za rehema zimekumbukwa mbele za Mungu.+ 32  Kwa hiyo, tuma watu waende Yopa na kumwita Simoni, anayeitwa Petro.+ Mtu huyu ni mgeni katika nyumba ya Simoni, mtengenezaji wa ngozi, kando ya bahari.’+ 33  Kwa hiyo mara moja nikatuma watu kwako, nawe ukafanya vema kuja hapa. Na kwa hiyo wakati huu sisi sote tupo mbele za Mungu kuyasikia mambo yote ambayo umeamriwa na Yehova kusema.”+ 34  Ndipo Petro akafungua kinywa chake na kusema: “Kwa hakika ninaona kwamba Mungu hana ubaguzi,+ 35  bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.+ 36  Alituma+ neno kwa wana wa Israeli kuwatangazia habari njema ya amani+ kupitia Yesu Kristo: Huyu ni Bwana wa wengine wote.+ 37  Ninyi mnaijua habari iliyoongewa kotekote katika Yudea yote, kuanzia Galilaya baada ya ubatizo aliohubiri Yohana,+ 38  yaani, Yesu aliyekuwa ametoka Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa roho takatifu+ na nguvu, naye akaenda akipita katika nchi akitenda mema na kuwaponya wote waliokandamizwa na Ibilisi;+ kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.+ 39  Nasi ni mashahidi wa mambo yote aliyoyafanya katika nchi ya Wayahudi na pia katika Yerusalemu; lakini walimwangamiza pia kwa kumtundika mtini.+ 40  Mungu alimfufua Huyu katika siku ya tatu na kumfunua,+ 41  si kwa watu wote, bali kwa mashahidi waliowekwa kimbele na Mungu,+ kwetu sisi, tuliokula na kunywa pamoja naye+ baada ya kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu. 42  Pia, alituagiza sisi tuwahubirie+ watu na kutoa ushahidi kamili kwamba Huyu ndiye aliyeagizwa na Mungu kuwa mwamuzi wa walio hai na wafu.+ 43  Kwake yeye manabii wote hutoa ushahidi,+ kwamba kila mtu anayemwamini hupata msamaha wa dhambi kupitia jina lake.”+ 44  Petro alipokuwa bado akisema juu ya mambo haya roho takatifu ikawaangukia wote waliokuwa wakisikia lile neno.+ 45  Na waaminifu waliokuwa wamekuja pamoja na Petro ambao walikuwa kati ya wale waliotahiriwa wakashangaa, kwa sababu zawadi ya bure ya roho takatifu ilikuwa ikimiminwa pia juu ya watu wa mataifa.+ 46  Kwa maana waliwasikia wakisema katika lugha na wakimtukuza Mungu.+ Ndipo Petro akajibu: 47  “Je, mtu yeyote anaweza kuyakataza maji kwamba hawa wasibatizwe+ ambao wameipokea roho takatifu kama vile sisi tulivyoipokea?” 48  Ndipo akawaamuru wabatizwe katika jina la Yesu Kristo.+ Kisha wakamwomba akae pamoja nao siku kadhaa.

Maelezo ya Chini