Matendo 15:1-41
15 Na watu fulani wakashuka kutoka Yudea+ na kuanza kuwafundisha ndugu: “Msipotahiriwa+ kulingana na desturi ya Musa,+ hamwezi kuokolewa.”
2 Lakini kulipokuwa kumetokea mtengano usio mdogo na bishano kati ya Paulo na Barnaba pamoja nao, wakapanga Paulo na Barnaba na wengine kati yao wapande kwenda kwa mitume na wanaume wazee katika Yerusalemu+ kuhusu bishano hilo.
3 Basi, baada ya kusindikizwa na kutaniko,+ watu hao wakaenda zao wakipitia Foinike na pia Samaria, wakieleza kirefu kugeuka kwa watu wa mataifa,+ nao walikuwa wakitokeza shangwe kubwa kwa akina ndugu wote.+
4 Walipofika Yerusalemu walikaribishwa kwa fadhili+ na kutaniko na mitume na wanaume wazee, nao wakaeleza mambo mengi ambayo Mungu alikuwa ameyafanya kupitia kwao.+
5 Lakini, baadhi ya wale wa madhehebu ya Mafarisayo waliokuwa wameamini wakasimama kutoka kwenye viti vyao na kusema: “Ni lazima kuwatahiri+ na kuwaamuru washike sheria ya Musa.”+
6 Na mitume na wanaume wazee wakakusanyika pamoja ili waliangalie jambo hilo.+
7 Basi bishano+ kubwa lilipokuwa limetukia, Petro akasimama na kuwaambia: “Wanaume, akina ndugu, ninyi mnajua vema kwamba tangu siku za zamani Mungu alichagua kati yenu kwamba kupitia kinywa changu watu wa mataifa wasikie neno la habari njema na kuamini;+
8 na Mungu, anayeujua moyo,+ alitoa ushahidi kwa kuwapa wao roho takatifu,+ kama vile alivyotupa sisi pia.
9 Naye hakufanya tofauti hata kidogo kati yetu na wao,+ bali aliisafisha mioyo yao kwa imani.+
10 Kwa hiyo, sasa kwa nini mnamjaribu Mungu kwa kuweka juu ya shingo za wanafunzi nira+ ambayo mababu zetu wala sisi hatukuweza kubeba?+
11 Kinyume chake, sisi tunaamini kwamba tutaokolewa kupitia fadhili zisizostahiliwa+ za Bwana Yesu katika njia ileile kama watu hao pia.”+
12 Ndipo umati mzima ukanyamaza, nao wakaanza kuwasikiliza Barnaba na Paulo wakieleza ishara nyingi na mambo mengi ya ajabu ambayo Mungu alifanya kupitia kwao katikati ya mataifa.+
13 Walipomaliza kusema, Yakobo akajibu, akisema: “Wanaume, akina ndugu, nisikieni.+
14 Simioni+ ameeleza kikamili jinsi Mungu kwa mara ya kwanza alivyoelekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.+
15 Na maneno ya Manabii yanakubaliana na jambo hili, kama vile ambavyo imeandikwa,
16 ‘Baada ya mambo hayo nitarudi na kukijenga upya kibanda cha Daudi ambacho kimeanguka chini; nami nitayajenga upya mabomoko yake na kukisimamisha tena,+
17 ili watu wanaobaki wamtafute Yehova kwa bidii, pamoja na watu wa mataifa yote, watu wanaoitwa kwa jina langu, asema Yehova, anayefanya mambo haya,+
18 yanayojulikana tangu zamani za kale.’+
19 Kwa hiyo nimeamua kutowataabisha wale wa kutoka katika mataifa wanaomgeukia Mungu,+
20 bali kuwaandikia wajiepushe na vitu vilivyochafuliwa na sanamu,+ na uasherati,+ na kile kilichonyongwa,+ na damu.+
21 Kwa maana tangu nyakati za kale katika jiji baada ya jiji Musa amekuwa na wale wanaomhubiri, kwa sababu yeye husomwa kwa sauti kubwa katika masinagogi kila siku ya sabato.”+
22 Ndipo mitume na wanaume wazee pamoja na kutaniko lote wakapendelea kutuma wanaume waliochaguliwa kutoka kati yao mpaka Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba, yaani, Yuda aliyeitwa Barsaba+ na Sila, wanaume wenye kuongoza kati ya akina ndugu;
23 na kwa mkono wao wakaandika:
“Mitume na wanaume wazee, akina ndugu, kwa wale ndugu katika Antiokia+ na Siria na Kilikia+ ambao ni wa kutoka kwa mataifa: Salamu!
24 Kwa kuwa tumesikia kwamba baadhi ya wale waliotoka kati yetu wamewataabisha ninyi kwa maneno mengi,+ wakijaribu kupindua nafsi zenu, ijapokuwa sisi hatukuwapa maagizo yoyote,+
25 sisi tumefikia kauli moja+ nasi tumependelea kuchagua wanaume tuwatume kwenu pamoja na wapendwa wetu, Barnaba na Paulo,+
26 watu ambao wametoa nafsi zao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.+
27 Kwa hiyo tunawatuma Yuda na Sila,+ ili wao pia wapate kueleza mambo hayohayo kwa maneno.+
28 Kwa maana roho takatifu+ na sisi wenyewe tumependelea tusiwaongezee ninyi mzigo+ zaidi, ila mambo haya ya lazima,
29 kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu+ na damu+ na vitu vilivyonyongwa+ na uasherati.+ Mkijiepusha kwa uangalifu na mambo haya,+ mtafanikiwa. Afya njema kwenu!”
30 Basi, watu hawa walipoachwa waende, wakashuka kwenda Antiokia, nao wakaukusanya umati pamoja na kuwapa barua hiyo.+
31 Baada ya kuisoma, walishangilia juu ya kitia-moyo hicho.+
32 Nao Yuda na Sila, kwa kuwa wao wenyewe walikuwa manabii+ pia, wakawatia moyo akina ndugu kwa hotuba nyingi na kuwatia nguvu.+
33 Kwa hiyo, baada ya kukaa huko kwa muda fulani, ndugu hao wakawaacha waende kwa amani+ kwa wale waliokuwa wamewatuma.
34 ——
35 Hata hivyo, Paulo na Barnaba wakaendelea kukaa Antiokia+ wakifundisha na kutangaza habari njema ya neno la Yehova, wakiwa pamoja na wengine wengi pia.+
36 Sasa baada ya siku kadhaa Paulo akamwambia Barnaba: “Zaidi ya mambo yote, na turudi tuwatembelee akina ndugu katika kila moja la majiji ambamo tulitangaza neno la Yehova tuone jinsi walivyo.”+
37 Barnaba alikuwa ameazimia kumchukua Yohana pia, aliyeitwa Marko.+
38 Lakini Paulo hakuona kwamba inafaa kumchukua huyo pamoja nao, kwa kuwa alikuwa amewaacha kule Pamfilia+ na hakuwa ameenda pamoja nao kwenye kazi.
39 Ndipo kukatokea hasira kali, hivi kwamba wakatengana; Barnaba+ akamchukua Marko pamoja naye na kusafiri kwenda Kipro.+
40 Paulo akamchagua Sila+ akaondoka kwenda zake baada ya kuwa amekabidhiwa na akina ndugu kwenye fadhili zisizostahiliwa za Yehova.+
41 Lakini akapitia Siria na Kilikia, akiyatia nguvu makutaniko.+