Hamia kwenye habari

VIJANA HUULIZA

Kwa Nini Mimi Hujikata Kimakusudi?

Kwa Nini Mimi Hujikata Kimakusudi?

 Kujikata ni nini?

 Kujikata ni tendo la kujidhuru kimakusudi kwa kutumia vitu vyenye ncha kali. Hiyo ni aina mojawapo tu ya kujiumiza kimakusudi. Aina nyingine za kujiumiza kimakusudi zinatia ndani kujiunguza, kujikwaruza, au kujipiga. Makala hii inazungumzia kujikata kimakusudi, lakini kanuni zinazozungumziwa zinatumika katika aina zote za kujiumiza kimakusudi.

 Tahini ujuzi wako: Kweli au Si kweli.

  1.   Ni wasichana peke ndio hujikata kimakusudi.

  2.   Kujikata huvunja amri ya Biblia iliyo kwenye Mambo ya Walawi 19:28, inayosema: “Msijikatekate mwili wenu.”

 Majibu sahihi:

  1.   Si kweli. Ingawa inaonekana tatizo hilo limeenea miongoni mwa wasichana, pia wavulana fulani hujikata na hujihusisha katika ana nyingine za kujiumiza kimakusudi.

  2.   Si kweli. Mambo ya Walawi 19:28 linarejelea desturi ya wapagani wa kale, na si tendo la kujiumiza kimakusudi linalozungumziwa katika makala hii. Hata hivyo, ni jambo linalopatana na akili kufikia mkataa kwamba Muumba wetu mwenye upendo hataki tujiumize.​—1 Wakorintho 6:​12; 2 Wakorintho 7:1; 1 Yohana 4:8.

 Kwa nini watu hujikata kimakusudi?

 Tahini ujuzi wako: Ni sababu gani unayofikiri ni sahihi zaidi?

 Watu hujikata . . .

  1.   kwa sababu wanajaribu kushinda maumivu yao ya kihisia.

  2.   kwa sababu wanajaribu kujiua.

 Jibu sahihi: A. Watu wengi wanaojikata kimakusudi hawataki kufa. Wanataka tu kumaliza maumivu yao ya kihisia.

 Ona mambo ambayo vijana fulani wamesema kuhusu zoea lao ya kujikata kimakusudi.

 Celia: “Liliniletea kitulizo.”

 Tamara: “Ilionekana kwamba lilinipa kitulizo. Maumivu ya mwili yalikuwa afadhali kuliko maumivu ya kihisia.”

 Carrie: “Sikupenda kuwa na huzuni. Kujikata kulinifanya niache kukazia fikira huzuni yangu na badala yake nikazie fikira maumivu ya mwili.”

 Jerrine: “Kila mara nilipojikata kimakusudi, ni kana kwamba nilisahau matatizo yangu, na nikahisi kwamba sikuhitaji kuyashughulikia. Nilifurahia jambo hilo.”

 Ikiwa una tatizo hilo, unawezaje kuliacha?

 Kusali kwa Yehova Mungu kunaweza kuwa hatua muhimu ya kuacha zoea hilo. Biblia inasema: ‘Tupeni mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’​—1 Petro 5:7.

 Pendekezo: Anza kwa kutoa sala fupifupi, labda ukimwambia Yehova hivi: “Naomba unisaidie.” Baada ya muda, utaweza kujieleza zaidi na kumwaga hisia zako kwa “Mungu wa faraja yote.”​— 2 Wakorintho 1:​3, 4.

 Sala haipaswi kuonwa kuwa njia ya kutuliza tu hisia. Ni njia ya kuzungumza waziwazi na Baba yako wa mbinguni, ambaye anaahidi hivi: “Nitakusaidia kwelikweli. Nitakushika kwelikweli kwa mkono wangu wa kuume wa uadilifu.”​—Isaya 41:10.

 Wengi wanaosumbuliwa na zoea la kujikata kimakusudi wamepata faraja pia kwa kuongea na mzazi au mtu mzima mwingine wanayemtumaini. Ona maelezo yafuatayo kutoka kwa vijana watatu ambao walifanya hivyo.

 Maswali ya kutafakari

  • Unapokuwa tayari kutafuta msaada, unaweza kumwendea nani?

  • Unaweza kusema nini unaposali kwa Yehova Mungu kuhusu tatizo lako?

  • Unaweza kuorodhesha njia mbili (ambazo hazihusishi kujiumiza kimakusudi) unazoweza kutumia kuondoa mkazo na mahangaiko yako?