Kulingana na Yohana 17:1-26

  • Yesu asali mara ya mwisho akiwa na wanafunzi wake (1-26)

    • Uzima wa milele ndio huu, kumjua Mungu (3)

    • Wakristo si sehemu ya ulimwengu (14-16)

    • “Neno lako ni kweli” (17)

    • “Nimewajulisha jina lako” (26)

17  Yesu akasema mambo hayo, kisha akatazama mbinguni na kusema: “Baba, saa imefika. Mtukuze mwana wako ili mwana wako akutukuze,+  kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili,*+ ili awape uzima wa milele+ wote ambao umempa.+  Uzima wa milele ndio huu,+ wakujue wewe,* Mungu wa pekee wa kweli,+ na yule uliyemtuma, Yesu Kristo.+  Nimekutukuza duniani,+ kwa kuwa nimemaliza kazi uliyonipa nifanye.+  Sasa Baba, nitukuze kando yako kwa utukufu niliokuwa nao kando yako kabla ya ulimwengu kuwako.+  “Nimelifunua* jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwenguni.+ Walikuwa wako, nawe ukanipa, nao wamelishika* neno lako.  Sasa wamejua kwamba vitu vyote ulivyonipa vimetoka kwako;  kwa sababu nimewapa maneno uliyonipa,+ nao wameyakubali na kwa hakika wamejua kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wako,+ nao wameamini kwamba ulinituma.+  Ninaomba kwa ajili yao; siombi kwa ajili ya ulimwengu, bali ninawaombea wale ulionipa, kwa sababu ni wako; 10  na vitu vyangu vyote ni vyako na vyako ni vyangu,+ nami nimetukuzwa kati yao. 11  “Mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni,+ nami ninakuja kwako. Baba Mtakatifu, walinde+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa, ili wawe kitu kimoja* kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.*+ 12  Nilipokuwa pamoja nao nilikuwa nikiwatunza+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa; nami nimewalinda na hakuna hata mmoja wao aliyeangamizwa+ ila yule mwana wa maangamizi,+ ili andiko litimizwe.+ 13  Lakini sasa ninakuja kwako, nami ninasema mambo haya ulimwenguni ili wapate kikamili shangwe niliyo nayo.+ 14  Nimewapa neno lako, lakini ulimwengu umewachukia, kwa sababu wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu. 15  “Sikuombi uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.+ 16  Wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+ 17  Watakase* kupitia ile kweli;+ neno lako ni kweli.+ 18  Kama ulivyonituma ulimwenguni, mimi pia nimewatuma ulimwenguni.+ 19  Nami ninajitakasa kwa ajili yao, ili wao pia watakaswe kupitia ile kweli. 20  “Ninaomba si kwa ajili ya hawa tu, bali pia wale wanaoniamini kupitia neno lao, 21  ili wote wawe kitu kimoja,+ kama vile ambavyo wewe Baba umo katika muungano nami, nami nimo katika muungano nawe,+ ili wao pia wawe katika muungano nasi, ili ulimwengu uamini kwamba ulinituma. 22  Nimewapa utukufu ambao umenipa, ili wawe kitu kimoja kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.+ 23  Mimi katika muungano nao nawe katika muungano nami, ili wakamilishwe wawe kitu kimoja,* ili ulimwengu ujue kwamba ulinituma na uliwapenda wao kama vile ulivyonipenda. 24  Baba, ninataka wale ambao umenipa wawe pamoja nami mahali nilipo,+ ili waone utukufu wangu ambao umenipa, kwa sababu ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi wa ulimwengu.+ 25  Baba Mwadilifu, kwa kweli, ulimwengu haujakujua wewe,+ lakini mimi ninakujua,+ na hawa wamejua kwamba ulinituma. 26  Nimewajulisha jina lako nami nitalijulisha,+ ili upendo ulionipenda uwe ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”+

Maelezo ya Chini

Au “wanadamu wote; watu wote.”
Au “waendelee kupata ujuzi juu yako wewe.”
Au “Nimelijulisha.”
Au “wamelitii.”
Au “tulivyo na umoja.”
Au “wawe na umoja.”
Au “Uwaweke kando; Uwafanye wawe watakatifu.”
Au “waunganishwe kikamili.”