Kwa Waroma 3:1-31

  • “Mungu aonekane kuwa wa kweli” (1-8)

  • Wayahudi na Wagiriki pia wako chini ya zambi (9-20)

  • Watu wanatangazwa kuwa wenye haki kupitia imani (21-31)

    • Wote wamepungukiwa na utukufu wa Mungu (23)

3  Basi, Muyahudi anapita watu wengine na nini, ao ni nini faida ya kutahiriwa? 2  Anawapita sana katika kila njia. Kwanza kabisa, wao walipewa maneno matakatifu ya Mungu.+ 3  Basi, hali iko namna gani? Kama wengine walikosa imani, je, ukosefu wao wa imani utafanya uaminifu wa Mungu ukuwe bure? 4  Hapana kabisa! Lakini Mungu aonekane kuwa wa kweli,+ hata kama kila mwanadamu anaonekana kuwa muongo,+ kama vile imeandikwa: “Ili uonekane kuwa mwenye haki katika maneno yako na upate ushindi wakati unahukumiwa.”+ 5  Lakini, kama ukosefu wetu wa haki unaonyesha wazi haki ya Mungu, tuseme nini? Je, Mungu anakosa haki wakati anaonyesha kasirani yake kali? (Ninasema katika maneno ya wanadamu.) 6  Hapana! Kama ni vile, Mungu atahukumu ulimwengu namna gani?+ 7  Lakini kama kupitia uongo wangu kweli ya Mungu imeonyeshwa wazi zaidi kwa utukufu wake, sababu gani mimi pia ninahukumiwa kuwa mutenda-zambi? 8  Na sababu gani tusiseme, kama vile watu fulani wanaeleza kwa uongo kama tunasema, “Tufanye mambo ya mubaya ili mambo ya muzuri yakuje”? Hukumu juu ya watu hao inapatana na haki.+ 9  Basi tuseme nini? Je, sisi tuko katika hali ya muzuri zaidi? Hapana kabisa! Kwa maana pale juu tumetoa shitaka kama Wayahudi na vilevile Wagiriki wote wako chini ya zambi;+ 10  kama vile imeandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mumoja;+ 11  hakuna hata mumoja mwenye kuwa na ufahamu; hakuna hata mumoja mwenye anamutafuta Mungu. 12  Watu wote wameenda pembeni, wote wamekuwa wenye hawana mafaa yoyote; hakuna hata mumoja mwenye anaonyesha fazili, hakuna hata mumoja.”+ 13  “Koo yao ni kaburi lenye kuwa wazi, wamedanganya kwa ulimi wao.”+ “Sumu ya nyoka iko nyuma ya midomo yao.”+ 14  “Na kinywa chao kimejaa kulaani na uchungu.”+ 15  “Miguu yao inaenda haraka ili kumwanga damu.”+ 16  “Uharibifu na taabu viko katika njia zao, 17  na hawakujua njia ya amani.”+ 18  “Hakuna kumuogopa Mungu mbele ya macho yao.”+ 19  Sasa tunajua kwamba mambo yote yenye Sheria inasema, inaambia wale wenye kuwa chini ya Sheria, ili kila kinywa kinyamazishwe na ulimwengu wote ustahili azabu mbele ya Mungu.+ 20  Kwa hiyo hakuna mutu mwenye atatangazwa mbele yake kuwa mwenye* haki kupitia matendo ya sheria,+ kwa maana kupitia sheria tunapata ujuzi wenye hauna makosa* kuhusu zambi.+ 21  Lakini sasa haki ya Mungu imefunuliwa bila sheria,+ kama vile Sheria na Manabii vinatoa ushahidi,+ 22  ndiyo, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo, kwa wote wenye kuwa na imani. Kwa maana hakuna tofauti.+ 23  Kwa maana wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,+ 24  na ni zawadi ya bure+ kwamba wanatangazwa kuwa wenye haki kwa fazili zake zenye hazistahiliwe+ kupitia kuachiliwa huru kwa njia ya bei ya ukombozi yenye Kristo Yesu alilipa.+ 25  Mungu alimutoa kuwa toleo la kufunika zambi*+ kupitia imani katika damu yake.+ Ilikuwa vile ili kuonyesha haki yake mwenyewe, kwa sababu Mungu kwa uvumilivu wake alikuwa anasamehe zambi zenye zilifanywa wakati wenye ulipita. 26  Ilikuwa vile ili kuonyesha haki yake mwenyewe+ katika kipindi hiki, ili akuwe mwenye haki hata wakati anatangaza mutu mwenye kuwa na imani katika Yesu kuwa mwenye haki.+ 27  Basi, je, tuko na sababu ya kujisifu? Hatuna sababu. Kupitia sheria gani? Ile ya matendo?+ Hapana kabisa, lakini kupitia sheria ya imani. 28  Kwa maana tunaona kwamba mutu anatangazwa kuwa mwenye haki kwa imani hapana kupitia matendo ya sheria.+ 29  Ao je, yeye ni Mungu wa Wayahudi peke yao?+ Je, yeye haiko Mungu wa watu wa mataifa pia?+ Ndiyo, ni wa watu wa mataifa pia.+ 30  Kwa kuwa Mungu ni mumoja,+ atatangaza watu wenye kutahiriwa kuwa wenye haki+ kutokana na imani na watu wenye hawatahiriwe kuwa wenye haki+ kupitia imani yao. 31  Basi, je, tunafuta sheria kupitia imani yetu? Hapana kabisa! Tofauti na hilo, tunaunga mukono sheria.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mwili wenye utatangazwa mbele yake kuwa wenye.”
Ao “sahihi.”
Ao “la upatanisho.”