Kwa Waroma 13:1-14

  • Kujitiisha chini ya mamlaka (1-7)

  • Upendo unatimiza Sheria (8-10)

  • Mutembee kama wakati wa muchana (11-14)

13  Kila mutu ajitiishe* kwa mamlaka zenye kuwa kubwa,+ kwa maana hakuna mamlaka isipokuwa kwa ruhusa ya Mungu;+ mamlaka zenye ziko zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.+ 2  Kwa hiyo, mutu yeyote mwenye anapinga mamlaka amepinga mupango wa Mungu; wale wenye wameupinga watajiletea hukumu wao wenyewe. 3  Kwa maana wale watawala ni kitu cha kuogopesha, hapana kwa tendo la muzuri, lakini kwa tendo la mubaya.+ Je, unataka usiogope mamlaka? Endelea kufanya mambo ya muzuri,+ na itakusifu wewe; 4  kwa maana hiyo ni mutumishi wa Mungu kwako kwa faida yako. Lakini kama unafanya mambo ya mubaya, ogopa, kwa maana haibebe upanga bila sababu. Hiyo ni mutumishi wa Mungu, mulipiza-kisasi ili kuonyesha kasirani kali* juu ya ule mwenye anazoea kufanya mambo ya mubaya. 5  Kwa hiyo kuko sababu ya lazima kwenu kujitiisha, haiko kwa sababu ya ile kasirani kali tu, lakini pia kwa sababu ya zamiri yenu.+ 6  Ndiyo sababu munalipa kodi pia; kwa maana wao ni watumishi wa Mungu kwa watu wote, na wanatumika bila kuacha kwa kusudi hili. 7  Mupatie wote haki zao: ule mwenye anataka kodi, kodi;+ ule mwenye anataka ushuru, ushuru; ule mwenye anataka woga, woga;+ ule mwenye anataka heshima, heshima.+ 8  Musikuwe na deni lolote kwa mutu yeyote isipokuwa kupendana;+ kwa maana kila mutu mwenye anamupenda mwanadamu mwenzake ametimiza sheria.+ 9  Kwa maana sheria zenye kusema, “Haupaswe kufanya uzinifu,+ haupaswe kuua,+ haupaswe kuiba,+ haupaswe kutamani,”+ na amri ingine yoyote yenye iko, zinatajwa kwa kifupi katika maneno haya: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.”+ 10  Upendo haumufanyie jirani mambo ya mubaya;+ kwa hiyo, upendo ndio utimizo wa sheria.+ 11  Na mufanye hivi kwa sababu munajua kipindi hiki, kwamba tayari ni saa ya ninyi kuamuka kutoka katika usingizi,+ kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu kuliko wakati tulianza kuamini. 12  Usiku umeendelea sana; muchana umekaribia. Kwa hiyo, tutupe matendo ya giza+ na tuvae silaha za mwangaza.+ 13  Tutembee kwa adabu+ kama wakati wa muchana, hapana katika karamu za kupitisha mipaka na ulevi, hapana katika uasherati na mwenendo mupotovu wa bila haya,*+ hapana katika mizozo na wivu.+ 14  Lakini muvae Bwana Yesu Kristo,+ na musikuwe munapanga mbele ya wakati kwa ajili ya tamaa za mwili.+

Maelezo ya Chini

Ao “Kila nafsi ijitiishe.”
Ao “kuleta azabu.”
Ao “matendo ya mwenendo wa bila haya.” Uwingi wa neno la Kigiriki a·selʹgei·a. Angalia Maana ya Maneno.